Huu utani wa kidwanzi ameuanzisha huyo Mzungu pori wao na sisi mashabiki wa Yanga hatukubali kuitwa manyani , mambwa na matusi mengine ya hovyo hatuko tayari kudhalilishwa utu wetu.
Simba mwabieni huyo msemaji wenu asiyepiga mswaki na kutoa shombo wakati wa kuzungumza kwenye vyombo vya habari akiizungumzia Yanga ilhali yeye ni msemaji wa timu yenu aache Mara moja.
Sisi tunao wasemaji wetu na wala hatumhitaji yeye kwa namna yoyote na pia hatuhitaji kukerwa kamaanavyosema.
Kizazi kinachokubali kukerwa kimeisha hiki ni kizazi kingine namshauri asome alama za nyakati vinginevyo kama hakubaliani na hilo anaweza kurudi nyuma akaishi na kizazi kilichokuwa kinakubali KUKERWA.
Nasema kuwa wana Yanga hatutaki kukerwa na matusi yenu wekeni akilini tutaniane kawaida siyo kutukanwa.
Siku ambayo tulifungwa 4-1 msimu uliopita kuna shabiki mmoja wa simba alitutukania mama zetu, Dada zetu, shangazi zetu mashabiki wote wa Yanga tuliokuwa tunaangalia mpira kwenye kibanda umiza.
Wakulaumiwa ni manara ndiyo chanzo cha sisi mashabiki wa Yanga kuwa tunatukanwa hata huku mitaani , alaaniwe Haji Manara!