Suala la mafuta ya kula lisipotezewe

lulu za uru

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2015
Posts
2,557
Reaction score
3,221
Kuna wengine wakienda supermarkets pesa iko na kubaki inabaki wanawapa tipu wahudumu kwahiyo hata mafuta yauzwe 10,000 Lita moja wala haiwasumbui pesa iko sio tatizo ni hivi to whom it may concern.

Sijui ni Waziri wa kilimo au viwanda mafuta yako juu mno Au mko group ya pesa sio tatizo kwahiyo hakiwatachi? Jamani hebu kaeni mtafakari mnafanyaje walau hali..ikae.shwari kidogo, vifurushi juu, mafuta juu sasa tukaejekaeje?
 
Tatizo la mafuta ni kupandishwa kwa kodi ya "import duty" kwenye budget ya mwaka jana toka asilimia 10% mpaka 25% ukiagiza mafuta ghafi hapo bado VAT, ndio maana mafuta yalipanda bei sana, mfano Vat 18%, import duty 25% railway levy 1.5 % unapata ni ailimia 44.5 ya mzigo uliogiza bado gharama na ushuru wa bandali lazima bei iwe juu.
 
Kuna namna ingefanywa kwa udharura MF.kuhimiza wakulima wadogo kulima alizeti angalau kupunguza tatizo kidogo...
 
Ndoo ya lita 10 leo nimenunua kwa 67,000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…