SUBARU IPREZA

ndalibanyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2014
Posts
415
Reaction score
400
Habari zenu humu ndani! Ninampango was kuagiza toyota premio ya 2003 ZZT 240. Ila kuna hii gari SUBARU IMPREZA ya 2008, cc 1490 . naona inanunuliwa sana kwa sasa hapa kwetu tanzania kiukweli nami naipenda lakini sina uelewa sana juu ya hii gari, mnaoifahamu tafadhalini tujuzane juu ya spare parts na gharama zake, bila kusahau ulaji wa mafuta. Tafadhali nawasilisha.
 
Naona hata cc yake ni ya kawaida so labda spare yake ziwe ghali ila naona liko poa sana
 
Impreza ni zaidi ya hiyo premio kuanzia uimara,ubora, powerful na fuel consumption.
Ishu kubwa Kwenye Subaru ni spare parts Tu kama utajimudu Kwenye Hilo chukua Hilo ndinga ufurahie maisha
 
Hii subaru ni poa sana...Spea zipo original tu...kwa hiyo uwe na mbavu nene....shock up moja tu unanunua tatu za hiyo premio......ika ukifunga mpaka ife tena na hilo gari umelichoka...ni kama Nissan
 
Impreza ni zaidi ya hiyo premio kuanzia uimara,ubora, powerful na fuel consumption.
Ishu kubwa Kwenye Subaru ni spare parts Tu kama utajimudu Kwenye Hilo chukua Hilo ndinga ufurahie maisha
Aisee poa sana kuhusu spare kuna makala moja nilisoma ya mbele mbele huko, inasema ukimiliki gari inabid uwe na account ya akiba yake kwa taadhari yoyote inayoweza tokea ikiwemo service ya gari. Nadhan ukiwa na mfumo huu unaweza usiumie sana.
 
Hii subaru ni poa sana...Spea zipo original tu...kwa hiyo uwe na mbavu nene....shock up moja tu unanunua tatu za hiyo premio......ika ukifunga mpaka ife tena na hilo gari umelichoka...ni kama Nissan
Basi kumbe ipo poa kama tukizingatia ubora na uimara, shida nyingine premio ipo mayai sana afu inawai kuchoka sana vinginevyo inahitaji matunzo ya hali ya juu.
 
A
Hii subaru ni poa sana...Spea zipo original tu...kwa hiyo uwe na mbavu nene....shock up moja tu unanunua tatu za hiyo premio......ika ukifunga mpaka ife tena na hilo gari umelichoka...ni kama Nissan
Isee nashukuru sana kwa ushauri wako, nadhan itakuwa chaguo sahihi kwangu man nimevutiwa nayo pia
 
Naona hata cc yake ni ya kawaida so labda spare yake ziwe ghali ila naona liko poa sana
Kweli chief, naona kwa jinsi inavyokubalika kwa sasa hapa kwetu bongo nadhani haitakuja kusumbua katika kuuza kama ukitaka kubadirisha gari! Liquidity yake itakuwa poa tu. Asante
 
Kwenye swala la Spare za magari ya kijapani affordable ni Toyota tu maana zenyewe hizo zipo za grade tofauti i.e. Orgininal, Feki original etc magari mengine yote spare ni original tu sio Subaru, Mazda, Nissan, etc
 
Kwenye swala la Spare za magari ya kijapani affordable ni Toyota tu maana zenyewe hizo zipo za grade tofauti i.e. Orgininal, Feki original etc magari mengine yote spare ni original tu sio Subaru, Mazda, Nissan, etc
Nissan yangu..najichagulia fake au original...zimejaa tele hapa Arusha...naangalia tu wallet yangu inasomaje siku hiyo..

Spea za bei rahisi za nissan zimeshaanza kuenea sana...

Angalizo...kuwa makini..ukienda vibaya unapigwa spea feki kwa bei ya original.....watu wenyewe wameshakariri spea za Nissan ni ghali
 
Tupatie tu walau mifano mitatu ya spea feki ulizonunua mkuu itasaidia sana
 
Chukua Crown athlete bana
 
Tupatie tu walau mifano mitatu ya spea feki ulizonunua mkuu itasaidia sana
Miezi miwili iliyopita nimefunga brake pads ambazo si original..bei sawa na bure..
Wikii hii ninefunga wish bone bushes..
Cv joint zipo za bei uitakayo na nimeshawahi kufunga..
Spark plugs zipo za bei rahisi na original...ila kwenye injini simshauri mtu afunge spark plugs za bei rahisi...
Ball joint na vikorokoro kibao vimejaa tele.....ni wewe tu kuamua..

Nissan kwa upande wa vifaa vya ndani vinapatika sana OG na Fake...
Mziki upo kwenye vifaa vya njee ya body mf Taa, bumper, vioo nk...hapo ndiyo bei yenye mbavu nene
 
Kwaio hata za Nissan Fuga zinapatikana sio?
 
Kwaio hata za Nissan Fuga zinapatikana sio?
Siwezi kusema ndiyo au hapana....
Ninachoweza kusema magari ya japan haswa toyota na Nissani, utakuta model tofauti tofauti zinavaliana spea nyingi tu...

Kwa mfano Nissan yangu inavaliana spea zote za injini na Nissan Tiida, Wingroad, Juke, baadhi ya blue bird na baadhi ya Nissan Sunny
Na model hizo nilizotaja hapo zinavaliana spea zote nyeti kama vile bushes, cv joints, ball joints, brake pads, etc

Hata hiyo Nissan fuga spea zake zipo na itakuwa na spea inayovaliana na nissan nyinginezo..ndiyo maana kuna Nissan fuga namba B mpaka sasa zipo barabarani...hii inaashiria wamiliki wake wanapata spea ndiyo maana hayo magari yana survive..

Tatizo letu watz ni wavivu wa kutafuta machimbo ya vitu tunavyomiliki
 
Kwenye swala la Spare za magari ya kijapani affordable ni Toyota tu maana zenyewe hizo zipo za grade tofauti i.e. Orgininal, Feki original etc magari mengine yote spare ni original tu sio Subaru, Mazda, Nissan, etc
Suzuki...hasa escudo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…