Sudan Kusini imetoa agizo la kuzuia upatikanaji wa mitandao ya kijamii nchini

Sudan Kusini imetoa agizo la kuzuia upatikanaji wa mitandao ya kijamii nchini

Joined
Jun 26, 2024
Posts
16
Reaction score
16
Serikali ya Sudan Kusini imetoa agizo la kuzuia upatikanaji wa mitandao ya kijamii ikiwamo Facebook na Tiktok nchini humo kwa muda wa hadi miezi mitatu, huku ikitegemea udhibiti wa maudhui.

Agizo hilo limetolewa na Mamlaka ya Kitaifa ya Mawasiliano ya Sudan Kusini (NCA) Jumatano Januari 22, 2025, huku likitajwa kusababishwa na video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita ikionyesha wakimbizi wa Sudan Kusini wakishambuliwa na watu wanaosemekana kuwa wanajeshi wa Sudan.

Akizungumzia agizo hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NCA, Napoleon Adok amesema; "Tunaomba rasmi kuzuiwa kwa tovuti hizi za vyombo vya habari kwa angalau siku 30. Agizo hili linaweza kuondolewa mara tu hali itakapodhibitiwa. Maudhui yanayoonyeshwa yanakiuka sheria zetu za ndani na yanahatarisha usalama wa umma na afya ya akili, hasa vikundi vilivyo hatarini.”
 

Attachments

  • SUDAN BANS Social Media PLatforms.png
    SUDAN BANS Social Media PLatforms.png
    559.9 KB · Views: 3
Hii Tik Tok hapa Tz inasubiria nini kufungiwa? Inatuharibia kizazi chetu hiki
 
Hii Tik Tok hapa Tz inasubiria nini kufungiwa? Inatuharibia kizazi chetu hiki
Kama mzazi au mlezi wa mtoto unatakiwa kuhakikisha vifaa vya kidigitali vya mtoto/watoto vimewekewa ulinzi kuzuia maudhuhi yasiyo salama kwa mtoto. Una jukumu hilo na sio kusingizia TikTok. Nenda katika settings na zuia aina ya maudhui unayoona hayafai ili kizazi chako kibaki salama.
 

Attachments

  • TikTok Restrict Content.jpg
    TikTok Restrict Content.jpg
    30.9 KB · Views: 3
Back
Top Bottom