SUGU adai yeye ndiye muasisi wa Bongofleva

SUGU adai yeye ndiye muasisi wa Bongofleva

Tunapata wakati mgumu sana kwenye distribution ya miziki yetu kwenye digital platforms kwa sababu amapiano na afrobeats zinasomeka kama genre ila hakuna bongo flavour
 
Kabisa mkuu maana saleh jabir alikuwa ana_imitate nyimbo za mtoni na kugeuza za kiswazi ila sugu ndio aliyeiteka bongo fleva mid 90's.
 
Umenikumbusha ice ice baby wa vanilla ice na OPP wa naughty by nature. Salehe Jabiri ni muasisi wa muziki wa rapu.
Jamaa anapenda tu tambo lkn kiuhalisia yy sio muasisi wa Bongo flavor, nakumbuka walikuwepo Diplomatz ambao ndo wa kwanza kuja single A you down with diplomatz. Baadae walikuja na Album ambayo sugu alishirikishwa kwenye baadhi ya track.

Nina uhakika Sugu anatamba hvy coz wale Diplomatz walisambaratika wengi wakaenda kupiga shule baadhi ss hv ni watu mashuhuri zaidi. Ukiacha kina Balozi Dollo na Saigon!

Ni vile wana mambo yao hawawezi kuja kubishana na Sugu khs nani hasa mwanzilishi wa Bongo fleva!
 
Hakuna ubishi  Sugu ndiyo muasisi wa bongo fleva , ametokanayo mbali sana aisee, ni wakati sasa wa kupewa heshima yake
Sio Muasisi, japo ndio ametoka nayo mbali na ameikuza kupitia mashairi ila SIO MUASISI.
 
But Sugu ni overrated sana hakuna shaka kuwa ni rapa wa kawaida sana kiasi ambacho Solo Thang,Afande sele na Prof J wamemuacha mbali sana
Upo sahihi, na pia ni wa mwanzoni ila yeye sio Muasisi wala Muanzilishi.
 
L
BONGO FLEVA NI STORY YA SUGU, MIKE NA TAJI

JOSEPH Mbilinyi ‘2 Proud’, kazi yake “Ni Mimi" ndio wimbo wa kwanza wa Swahili Rap kusikika Radio One Stereo mwaka 1994. Vilevile akawa Rapper wa kwanza wa Swahili Rap kufanya mahojiano Radio One.

Mike Mhagama, alikuwa mtangazaji wa kwanza kugonga ngoma ya Swahili Rap. Mmiliki wa wimbo alikuwa 2 Proud a.k.a Mr II au kwa uzito zaidi mwite Sugu.

Taji Liundi ‘Master T', ndiye mtayarishaji wa kwanza wa shoo za Swahili Rap. Akawa DJ wa kwanza Bongo kucheza nyimbo za Swahili Rap. Akaasisi kipindi cha DJ Show, Radio One, kilichopiga ngoma mfululizo za Kiswahili.
Mkuu Wakwetu, kwanza asante kwa taarifa hii.
  1. Taji ni mdogo wangu Ilboru mimi nikiwa A-level, Taji alikuwa O-level
  2. Baada ya Ilboru nikaenda TSJ na kuajiriwa RTD mwaka 1990 wakati Taji bado yuko shule. Redio ndio ilikuwa moja tuu RTD
  3. Rap ya kwanza ya Kiswahili iliimbwa mwaka 1992 na dogo mmoja wa Upanga akiitwa Saleh Jabir wimbo wa Ice Ice Baby na OPP.
  4. Nilizipiga RAP hizo RTD external service na Idhaa ya Biashara kwenye kipindi cha Bwana Chair na Kusikia na BP maana kuzipiga Idhaa ya Taifa hazijathibitishwa.
  5. Mwaka 1993 dogo mmoja wa familia ya kitajiri aliyekuwa akisoma IST kwa jina la Adili Kumbuka na kundi la Kwanza Unit aliachia Swahili Rap ya kwanza iliyopigwa ukumbi wa Bills na mimi kuzipiga.
  6. December 1993 Mbogo mwingine kwa jina la Emmanuel Mkulila akiishi Pasadena US aliachia single ya Kiswahili ila ilikuwa ni R n B.x
  7. 1994 ndio Radio One ikaanzishwa na Sigu ndio akaibuka na kuirasimisha rasmi RAP na jina la Bongo Flava kuibuka.
  8. Album ya kwanza ya Sugu miongoni mwa thanks kule nyuma ya album enzi hizo ni cassete, jina langu lipo nyuma ya Album.
Kiukweli tumetoka mbali!.
P
 
L

Mkuu Wakwetu, kwanza asante kwa taarifa hii.
  1. Taji ni mdogo wangu Ilboru mimi nikiwa A-level, Taji alikuwa O-level
  2. Baada ya Ilboru nikaenda TSJ na kuajiriwa RTD mwaka 1990 wakati Tajiri bado yuko shule. Redio ndio ilikuwa moja tuu RTD
  3. Rap ya kwanza ya Kiswahili iliimbwa mwaka 1992 na dogo mmoja wa Upanga akiitwa Saleh Jabir wimbo wa Ice Ice Baby na OPP.
  4. Nilizipiga RAP hizo RTD external service na Idhaa ya Biashara kwenye kipindi cha Bwana Chair na Kusikia na BP maana kuzipiga Idhaa ya Taifa hazijathibitishwa.
  5. Mwaka 1993 dogo mmoja wa familia ya kitajiri aliyekuwa akisoma IST kwa jina la Adili Kumbuka na kundi la Kwanza Unit aliachia Swahili Rap ya kwanza iliyopigwa ukumbi wa Bills na mimi kuzipiga.
  6. December 1993 Mbogo mwingine kwa jina la Emmanuel Mkulila akiishi Pasadena US aliachia single ya Kiswahili ila ilikuwa ni R n B.x
  7. 1994 ndio Radio One ikaanzishwa na Sigu ndio akaibuka na kuirasimisha rasmi RAP na jina la Bongo Flava kuibuka.
  8. Album ya kwanza ya Sugu miongoni mwa thanks kule nyuma ya album enzi hizo ni cassete, jina langu lipo nyuma ya Album.
Kiukweli tumetoka mbali!.
P
Namba 2 hapo umeandika Tajiri, hivi full name yake ni Tajiri Liundi au umekosea tu?
 
Hisense smart 4k inch 55 iko creen inafaa kwa matumizii ya kuonesha banda la mpira au pia nyumbn beii million 1.1 ni check tumalizane location mbagara kijichi 0685 809 502
1664170411570.jpg
 
Back
Top Bottom