Mimi kitu kimoja tu kinanishangaza CDM bila matukio hawana nyimbo kabisa yaani wanasubiri matukio yatokee ndio wapate pa kutokea. na yasipotokea basi lazima wayatengeneze hata kama ni kwa kuvunja sheria maana bila hivyo wanajua hawawezi kutoka kabisa. Sasa najiuliiza hawawezi kuendesha shughuli zao wakaleta hoja mbadala za kuwakomboa watu na umasikini wao na wakaeleweka? hoja zao zote ukizichunguza ni za matukio tu ili wapate sympath ya wananchi.
Kulalamika kutwa kuchwa. Kwanini basi wasionyeshe mfano kwa yale serikali iliyoshindwa kutekeleza ili tujue kuwa wakipewa nchi wataweza? mfano mdogo tu waende kwenye vijiji ambavyo havina maji waangalie chanzo cha ukosefu wa maji ni nini wakitatue wananchi wapate maji unafikiri hao wanachi wataacha kuwapenda wakawachagua tena na tena?
Maana ukiangalia vyanzo vingi vya maji vimekauka kwa uharibifu wa mazingira uliosababishwa na wananchi wenyewe so hawataweza kuwaambia wananchi ukweli kuwa hapa tatizo ni uharibifu wa mazingira tufanye hivi na hivi ili tuyapate haya maji hofu yao ni kuwa wakifanya hivyo pengine wanaweza wakakosa kura 2015 kumbe kinyume chake wangependwa zaidi. ila kwa sababu wako kitamaa zaidi kuwa lazima waingie ikulu so ile sumu ya kupandikiza chuki lazima waieneze ndio maana katika hoja zao hakuna mpya zaidi ya zile zile za epa, richmond, meremeta, rada, kung'oa kucha, meno, mauaji ya mwango'si na mengine yafananayo. yaani ukiwachunguza kweli hawana jipya mpaka tena litokee tukio lingine wapate mtoko.
Halafu ukichunguza matukio yanayogusa wote kimya. yaani ni kama wamekosa upembuzi yakinifu.