Kwa kweli purchasing power imeshuka na hali ni ngumu. Badala ya mleta mada kumkejeli na kumkatisha tamaa sugu angependekeza baadhi ya njia za kupambana na hali ngumu kama vile (i) kubadili mbinu za marketing na kufanya marketing na finishing ya jengo kwa mahitaji ya soko la sasa (ii) kupendekeza jinsi ya kuomba na kupata nafuu ya malipo na nafuu ya riba inayotokana na kubadilika kwa hali ya uchumi na biashara (iii) aina ya bima anazohitaji (iv) matumizi ya teknolojia zinazopunguza gharama za uendeshaji...
E.t.c
Kwanza hajaona kama Sugu hana marketing strategy ambayo ni sahihi.
Pili mleta mada hajui terms za mkopo huo kama zitakuwa affordable ama la kwa Sugu. Hata wewe rafiki hapa hujui kama riba ndilo litakuw atatizo la Sugu au hata kama Sugu atakuwa na shida katika marejesho.
Sugu hajasema kama biashara yake na mkopo wake hauna bima au hata hajaulizwa ili mshadadiaji ajue kama anafanya investment isiyokuwa na kinga dhidi ya yasiyotarajiwa.
Gharama za uendeshaji wa Sugu ni zipi? Nani ana statement yake ya hiyo hotel aweke hapa tuone kama anaendesha ka hasara, au ana tumia irrelevant and inappropriate technology.
Kumpgia mtu ramli kwa ushabiki ni dhambi. Aongee na Sugu ili ajue ni changamoto gani anaforesee, afanye tathmini ya mpango wa biashara ya sugu, ndipo aweze ku foresee nini Sugu hakijui na ambacho kitaathiri biashara yake bila yeye kujua wala kutegemea halafu alete mjadala hapa.