SUMATRA simamieni bei za Uber, bolt, ping na biashara za usafiri mtandaoni

Manifestation

Senior Member
Joined
Jan 22, 2020
Posts
193
Reaction score
323
Umefika wakati mamlaka ya usafiri kuangalia upya namna hizi kampuni za usafiri zinavyowahudumia wateja wao. Ukiangalia kampuni kama Uber wanatoa huduma nyingi kwa dereva na abiria kwa kumuwekea bima dereva na abiria iwapo anapata ajali wakati wa safari na bei zao ni za uhakika na zinaendana na mazingira halisi ya abiria na dereva.

Ila ukija kwenye mtandao inaitwa bolt/ taxify kwanza dereva/ abiria hana bima ya kumlinda Safarini pia bei zao haziendani na uhalisia na madereva hawapewi kamisheni yoyote huku vyombo vyao vikiumia sana.

Ni vizuri SUMATRA wakaingilia kati hizi biashara na kuwe na bei elekezi kulingana na kilometers alizotembea sio mtu anatoka Makumbusho mpaka Tabata Segerea kwa Shilingi 3000.
 
Asante Uber! Tax drivers wa bongo walijisahau mno! Toka Mwenge kwenda posta unaambiwa 20,000! Ukisikia utandawazi ndo huo. Ngoja soko liamue. Na sisi walaji tufaidike.
 
Asante Uber! Tax drivers wa bongo walijisahau mno! Toka Mwenge kwenda posta unaambiwa 20,000! Ukisikia utandawazi ndo huo. Ngoja soko liamue. Na sisi walaji tufaidike.
Walijisahau Ila kunatakiwa kuwe na usimamizi mzuri WA hizi huduma maana hawa jamaa wanaweza wakaua vyombo na kuwafanya madereva wakashindwa peleka hesabu Huku vyombo vikiharibika
 
Hakuna SUMATRA sasa hivi. Labda kama unawaambia LATRA
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna App za wazawa kama TANTAXI ambazo ziko vizuri sana na zingeleta mabadiliko ila watu wamekariri uber na Bolt. Uwekezaji pia lazima utazame wawekezaji wa ndani ambao gharama zao za uendeshaji sio kubwa kivile kiasi haitowalazimu kuweka kamisheni kubwa kama ilivyo kwa Bolt na Uber: TanTaxi Passenger - Apps on Google Play. Hii TanTaxi haikati kamisheni kwa sasa na wamedhamiria kutovuka asilimia 10%. Abiria anafaidika na dereva anafaidika na kupata moyo wa kutoka huduma nzuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…