Sun Tzu na masuria wa mfalme.

Sun Tzu na masuria wa mfalme.

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Sun Tzu alikuwa kamanda wa jeshi na Mwanafalsafa wa kichina enzi hizo china inatawaliwa na maemperor.

Siku moja Sun Tzu akamwambia mtawala (tumwite mfalme) kuwa, mtu yoyote anaweza kuwa mwanajeshi kinachotakiwa ni uongozi mzuri utakaosimamia nidhamu. mfalme huyu alikuwa na jeshi dogo na alikuwa kwenye hatari ya kuvamiwa na ufalme wa jirani.

Basi mfalme akamwambia inamaana hata hawa masuria wangu unaweza kuwafanya kuwa wanajeshi?(masuria kazi yao ilikuwa ni kushinda kujipamba na kujifunza jinsi ya kumridhisha mfalme kingono) Sun Tzu akajibi ndiyo. Mfalme akamwambia hebu nionyeshe. wakaitwa masuria wa mfalme na Sun Tzu akawaonyesha basic moves za mafunzo ya kijeshi. kisha akachagua masuria wawili kuwa kama maofisa watakaoongoza hayo mafunzo. Basi akawaambia ngoma ikipigwa mnaanza mafunzo. Basi ngoma ilivyopigwa wale masuria wakaangaliana na kuanza kucheka.

Sun Tzu akawaambia labda sijaeleweka. akawafundisha tena na kuwaambia ngoma ikilia anzeni mafunzo. Ngoma ilivyolia wale masuria badala ya kujifunzo wakaanza tena kucheka. Sun Tzu akachukua panga kutoka kwa wale masuria viongozi na kuwakata vichwa wale viongozi hapohapo. Kisha akachagua masuria wengine wawili na kuwaambia kuwa ngoma ikipigwa wawaongoze wenzao kwenye mazoezi ya kijeshi.

Basi ngoma ilivyopigwa wale Masuria walifanya onyesho la kijeshi kama vile ni wanajeshi wazoefu wa muda mrefu na wakaa ndani wakijipamba. Basi mfalme akamruhusu Sun Tzu aongoze jeshi lake na aliliongoza kwa mafanikio makubwa.
 
Sun Tzu alisema kuwa "kama amri au maelekezo hayaeleweki basi ni makosa ya kamanda lakini kama amri imeeleweka lakini wanajeshi hawaifuati basi ni makosa ya maofisa wa jeshi"
 
Ni kweli utayari ni kitu cha muhimu ...
 
Aliandika kitabu "Sanaa ya Vita" kinachosomwa hadi leo anamoeleza nadharia ya vita.

Mafundisho yake ni ya kwamba vita ni jambo la hatari ni afadhali kuepukana nayo ka sababu mara nyingi inaharibu taifa na dola. Vita inapaswa kufuata shabaha ya siasa inayoeleweka na kumaliza baada ya kufika shabaha.

Alisema ni bora kuvurugisha mipango ya adui kuliko kupambana naye, halau ni afadhali kuvunja ushikamano wake na wasaidizi na kwenye nafasi ya tatu tu ni kuingia vitani na kushinda.

Kitabu cha Sun Tzu inasomwa na kufundishwa hadi leo katika vyuo vya kijeshi mbalimbali. Kati ya viuongozi wa kijeshi waliotafakari ushauri wa kitabu hii ni


 
Back
Top Bottom