Support System...

Ndio ni vizuri kumtegemea Mungu ila kupata unachotaka/hitaji inabidi ukihangaikie pia.Huwezi kukaa ndani tu ukaomba uwe upate chakula na mavazi na vikajitokeza tu bila wewe kuhangaika. Na inapokua kwamba wewe umeshindwa/una wakati mgumu kupata mahitaji yako unatakiwa uchanganye maombi na wanadamu wengine upate kusaidika.
 
Ndicho haswa nnachomaanisha mpenzi...
Yeye kama yeye kwa wakati huo labda aliona hamna cha zaidi anachoweza kufanya kutatua matatizo yao zaidi ya kuondoa uhai aa wanawe. Ila kama angepata mawazo ya mtu mwingine pengine angegundua kwamba kuna mengi tu angeweza kufanya na kuepuka kufanya alichofanya.
 
We babu wewe...
Nwy unaona sasa kwa mfano angekua ameleta tatizo lake JF ungeshampa wazo?!Sio kila mtu anaweza kufikiria kwa mapana hivyo hata kuona option zote.

Hus hiyo ya kumpa anaejiweza ni hali ya kujionyesha na kutaka sifa. Sisi binadamu tuna roho za ajabu sana kwakweli. Hua tunaona rahisi kumuongezea alichonacho kwa sababu za kibinafsi kuliko kumpa asiyenacho bila kutegemea chochote.
Alafu marafiki na ndugu wanaokimbia wanaposikia una tatizo wapo wengi kweli...muhimu ni utafute mmoja ambae hata kama hatakua na kile unachohitaji bado atasimama na wewe na kukupa moyo.

Mr Rocky umegonga mule mule...ukosefu wa watu tunaowaamini haswa hata kuweza kushea nao matatizo yetu mazito kunasababisha sana matatizo mengine ambayo yangekwepeka kirahisi tu. Sema ndio hivyo tena binadamu hatufanani...mwingine anafurahia matatizo yako na kukasirikia maendeleo yako kwahiyo hata ukianguka hawezi kukuinua.
Ila sasa ni muhimu tusiwe tunategemea tusiyoweza kuwapa wengine. Kama wewe umekua mtu wa kupotezea/chekelea matatizo ya wengine au kuwakimbia pale wanapokua na shida usitegemee kupata kinyume cha hayo. Anza wewe kuwa mzuri kwa wengine...
 
maskini watoto............msongo wa mawazo unasababisha kufanya kitu hukutarajia.............fikiria mume wameachana, kazi umefukuzwa, msaada serikalini ndio hivyo daaah...........haya maisha wakati mwengine
 
maskini watoto............msongo wa mawazo unasababisha kufanya kitu hukutarajia.............fikiria mume wameachana, kazi umefukuzwa, msaada serikalini ndio hivyo daaah...........haya maisha wakati mwengine

Maishani mtihani mkwe...kila mtu ana mbinu zake kukabiliana nao. Nyingine nzuri na nyingine hazijitoshelezi!!
 
Maishani mtihani mkwe...kila mtu ana mbinu zake kukabiliana nao. Nyingine nzuri na nyingine hazijitoshelezi!!

mkwe hujajibu msg yangu kule

back topic.............ninafikiria kwanini hata hakuweza kuwapeleka watoto kwa baba yao hata kama atakuwa na mke mwingine ni bora kuliko alichokifinya.......au hakutaka watoto wakaishi kwa mzazi mwenzake.........ninaimagine yule bwana alipopata hii habari ameichukuliaje.............nafikiri kuna sababu kubwa ndani ya moyo wake kufikia hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…