SWALI FIKIRISHI: Je, Magufuli ameondoka na Corona? Hatusikii tena kelele zake

Toka Magufuli afariki, wapinzani nao wamenyamaza kupiga kelele za uwepo wa corona - Tanzania.
Najiuliza je Magufuli ameondoka na corona yake?
Ulikuwa jela? Kila siku watu wanapiga makelele humu kwamba mama alete chanjo ,kila siku watu wanapiga makelele kwanini Mama havai Barakoa! Korona inaenda na wave, wave la pili limemuondoa JIWE na mapadri 33+ ,tusubiri wave ya tatu.
 
Hatujabisha hilo, tunachojoji ni kupotea kwa kelele za Corona baada ya kifo cha Rais. Huwa unaelewa kabla ya kujibu?

Mama kasema anaunda tume ya wataalamu wabobezi kuhusiana na Corona.

Kelele zipi tena kabla ya mrejesho?

Tulipo tunasubiria kufahamu tume imeshaundwa na imefika wapi.

Kelele za nini hapo?
 
asante
 
FRANCIS DA DON huko sawa kabisa. Kila jambo lina sababu. Wahenga walisema "UKIONA KIFARANGA KIKO JUU YA CHUNGU UJUE MAMA YAKE YUKO CHINI".
JPM alitujenga kisaikolojia kuhusu vita za wababe wa ulimwengu. Kazi iliyobaki ni sisi wananchi mmoja mmoja kuijua falsafa hii ya JPM na kuitetea ili sisi na vizazi vyetu tuwe salama.
 
Kwahiyo tume ndio imepiga marufuku zile Tanzia mlizokuwa mnaleta kila siku?

Kelele ulizokuwa unazisikia zilikuwa ni miito kwa serikali ya awamu ya 5 kuchukua hatua.

Serikali iliyopo imekubali kuchukua hatua.

Tunasubiria sasa mrejesho. Kipi huelewi hapo?
 
Kelele ulizokuwa unazisikia zilikuwa ni miito kwa serikali ya awamu ya 5 kuchukua hatua.

Serikali iliyopo imekubali kuchukua hatua.

Tunasubiria sasa mrejesho. Kipi huelewi hapo?
Watu si bado wanaendelea kufa? Au hawafi kwa Corona tena?Kwani Tanzia lengo ni nini? Kupanikishana au kupeana taarifa? Endeleeni kutupa taarifa kama mwanzo; otherwise mlikuwa na agenda ovu juu ya Hayati JPM
 
Watu si bado wanaendelea kufa? Au hawafi kwa Corona tena?Kwani Tanzia lengo ni nini? Kupanikishana au kupeana taarifa? Endeleeni kutupa taarifa kama mwanzo; otherwise mlikuwa na agenda ovu juu ya Hayati JPM

Angefanya JPM aliyofanya Samia, kusingekuwa na kelele.

Samia kachukua njia iliyo sahihi kuwaacha wataalamu washauri kitalaamu na kwa uhuru wao wote.

Angefanya hivyo JPM mbona tungemwuunga mkono kama tunavyomwuunga mkono mama?

Hapendwi mtu. Matendo!
 
Kuna hatari ya covid 19 lakini mahali nilipo sijawahi kushuhudia kesi ya covid hata kwa jirani.
 
Corona inakuja kama waves na kupotea.
Kweeliiii???
Hili wimbi linapotea Tanzania tuu.
Vipi majirani zetu Kenya ambao wamejifungia toka MWAKA Jana,
Tena wakajarobu kufungua shule MWAKA huu, lakini yamewashinda,
Bado wamefunga shule, ikiambatana na hatua nyingine Kama lockdown, nk
 
Kwani huamini alichosema mama .....

Kuzaliwa muafrika n barakoa tosha...👣
 
Watu si bado wanaendelea kufa? Au hawafi kwa Corona tena?Kwani Tanzia lengo ni nini? Kupanikishana au kupeana taarifa? Endeleeni kutupa taarifa kama mwanzo; otherwise mlikuwa na agenda ovu juu ya Hayati JPM
Maneno hayooo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…