Swali fukunyuzi: Kabudi katuasa vizuri sisi Wakenya, ila mbona huko kwao Tanzania hawazingatii haya haya anayoturai?

Swali fukunyuzi: Kabudi katuasa vizuri sisi Wakenya, ila mbona huko kwao Tanzania hawazingatii haya haya anayoturai?

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Nimeisikiliza hotuba ya Profesa Kabudi wa kutokea Tanzania, kwa kweli ametiririka maneno yenye hekima na kutuasa Wakenya tuwe kimoja, pia akamsifia sana Rais wetu Uhuru kwa kukubali kujishusha na kuweka uzalendo mbele na kukaa meza moja na wapinzani kwa minajili ya vipaumbele vya taifa.

Nikawa najiuliza mengi, maana taarifa tunazozisoma kuhusu Tanzania zinakinzana na huu ushauri wa Professa kwa asilimia 100%, kule watu wamegawanyika kwa misingi ya vyama, yaani juzi tu chama kinachotawala kimeibuka na ushindi wa asilimia 99% baada ya upinzani kutunishiwa misuli hadi wakajiondoa.

Tumekuwa tukiona matamko na mikwara ya waliopo kwenye dola wakiweka wazi bila kuremba kwamba maeneo ya upinzani yanakosa maendeleo kama adhabu ya maamuzi yao mabaya.

Mifano ni mingi tu ambayo tunaisoma inayodhihrisha demokrasia ilivyofukiwa kwa Wabongo, sasa professa, hivi alikua anatuma ujumbe kwao nyumbani kinyemela au alikua na maana gani.

Pia juzi tuliona Spika wa Tanzania alitutembelea hapa Kenya na kusifia sana mfumo wetu wa kurusha shughuli za bunge mubashara, licha ya yeye kule kwao kubana hayo hayo aliyokuwa anasifia, sielewi mbona wakija huku wanasifia mambo ambayo wenyewe kwao wanayakandamiza na kuyadidimiza.
 
Whataboutism?

Sasa ulitaka Kabudi afanye nini? Kwani Kabudi ni Raisi wa JMTZ? Yeye ni Waziri tu isitoshe katoa maoni yake binafsi kama alivyoombwa na waliomualika, labda tujiulize kwa nini aalikwe yeye mbona sikuona Mganda, Rwanda, Sudani, Somalia au hata Kongo pia wakiongea?
 
Huyu ni yule yule Kabuti alikuwa analia Ati ndege ya ATCL imekamatwa na mkulima kule Canada??? Duuuh.... vituko haviishi kweli
 
Wewe siku hizi umekua ni mkorofi mtukutu, badala ya kuyafanyia kazi maneno kuntu ya Prof Kabudi tayari umeshaanza kuleta ubishi wako hapa janvini, kwa mwendo huu na tabia hizi mtaendelea kulialia sana na ukabila.

Nimeisikiliza hotuba ya Profesa Kabudi wa kutokea Tanzania, kwa kweli ametiririka maneno yenye hekima na kutuasa Wakenya tuwe kimoja, pia akamsifia sana Rais wetu Uhuru kwa kukubali kujishusha na kuweka uzalendo mbele na kukaa meza moja na wapinzani kwa minajili ya vipaumbele vya taifa.
 
Fuata maeneo yake usifuate matendo yake
 
Katutia aibu
IMG-20191127-WA0072.jpeg
 
Whataboutism?

Sasa ulitaka Kabudi afanye nini? Kwani Kabudi ni Raisi wa JMTZ? Yeye ni Waziri tu isitoshe katoa maoni yake binafsi kama alivyoombwa na waliomualika, labda tujiulize kwa nini aalikwe yeye mbona sikuona Mganda, Rwanda, Sudani, Somalia au hata Kongo pia wakiongea?

So uhuni unaofanyika huku Tanzania rais ndio kinara! Huyo Kabudi ilibidi azomewe kwa kutaka kupeleka unafiki Kenya. Halafu anataka kupeleka huu upuuzi wa huku Tanzania wa kumsifia rais wa Kenya, akidhani huko rais anasujudiwa kinafiki kama huku.
 
Sisi hatuna ukabila ulioota mizizi kama kwenu Kenya!

Huku kuna upuuzi anaupandikiza wa vyama, sasa hivi maendeleo anapeleka kwa mtazamo wa vyama, na ajira chache anazotoa kigezo ni kadi ya ccm.
 
Huku kuna upuuzi jiwe anaupandikiza wa vyama, sasa hivi maendeleo anapeleka kwa mtazamo wa vyama, na ajira chache anazotoa kigezo ni kadi ya ccm.
Unazidi kuchanganyikiwa, which is good
 
Back
Top Bottom