Swali fukunyuzi: Kabudi katuasa vizuri sisi Wakenya, ila mbona huko kwao Tanzania hawazingatii haya haya anayoturai?


alimwapisha jaji mmoja mchaga, akamsifia anavyopinga ufisadi mpaka watu walisema "huyu mchaga gani hataki rushwa?..."

jana pia amehutubia Igunga kwa kilugha, nikajiuliza, Igunga huko anaongea lugha gani, ghafla mzee akaona hapati muitikio, akawauliza, Kisukuma si mnakisikia? Sasa kama huna hakika Igunga wanasikia Kisukuma, kwa nini usiongee Kiswahili?

Alikuwa akijitetea ucheleweshaji wa mradi wa maji ya Victoria, akawaliwaza kwa Kisukuma kwamba hata shamba la mpunga linaanza kwa kuandaa shamba kabla ya kupanda na kuvuna... akielezea failures za serikali yake anatumia karata ya ukabila kutafuta sympathy kuwakumbusha ni mtu ni wao, anawaona ni wakulima ma primitive ambao akiongea nao lugha za kienyeji ata connect...
 
Kuna Tanzania mbili tofaut ndugu yangu kuna Tanzania ya mitandaon na Tanzania kama nchii yamitandaoni sio tunayoyaishi uraiani uku mitandaoni unaweza sema Tanzania kesho hawaamki salama ila ukakuta watu wanadunda tuu kama kawaida
 
Kuna Tanzania mbili tofaut ndugu yangu kuna Tanzania ya mitandaon na Tanzania kama nchii yamitandaoni sio tunayoyaishi uraiani uku mitandaoni unaweza sema Tanzania kesho hawaamki salama ila ukakuta watu wanadunda tuu kama kawaida
Kaandika eti watanzania wamegawanyika 😂😂😂 angejua huku mitaani watanzania walivyo busy na maisha yao wala asingeandika huu upumbavu wake hapa,
Au anafikiri Tanzania ni kama kenya namna wanavyo kokotwa na wanasiasa wao.
 
Kuna Tanzania mbili tofaut ndugu yangu kuna Tanzania ya mitandaon na Tanzania kama nchii yamitandaoni sio tunayoyaishi uraiani uku mitandaoni unaweza sema Tanzania kesho hawaamki salama ila ukakuta watu wanadunda tuu kama kawaida

Ya mtaani lazima kila mtu aonyeshe furaha bila kulalamika maana mpo kwenye mwendo wa mapambio, bila kuimba mapambio mambo yako hayaendi, ila mkija huku kwenye mitandao mnatoa yote ya moyoni.
 
Hata Bashiru Ali maneno anayoongea sasa huwezi amini kama ni yule yule aliyekua UDSM akitoa lecturer mbalimbali katika somo la Development Studies au akiwa mwanafunzi pale maana mimi minesoma nae
 
November 28, 2019
Nairobi , Kenya

Tundu Lissu atema cheche ktk mahojiano maalum jijini Nairobi Kenya

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Singida Mashariki nchini Tanzania kupitia chama cha CHADEMA, Mh. Tundu Lissu akielezea kinaga ubaga hali halisi ya kisiasa nchini Tanzania ambapo siasa za vyama vingi, mikutano ya wazi na ndani vyote vimepigwa marufuku na serikali ya awamu ya 5 ya CCM
Source: KTN News Kenya
 
November 28, 2019
Unguja, Zanzibar

Kufuatia mbinyo wa kidiplomasia toka mataifa ya nje, Katibu Mkuu wa CCM atoa onyo kali

Katibu Mkuu wa chama cha CCM kinachoongoza serikali nchini Tanzania Bw. Bashiru Ally akemea nchi rafiki na mashirika ya kimataifa kujiingiza ktk mambo ya ndani hususan siasa baada nchi kadhaa kukosoa dosari kubwa gandamizi zilizojitokeza ktk uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijiji ambapo vyama vya upinzani vilifanyiwa rafu na kusababisha wagombea asilimia 94 kuondolewa haki yao ya kugombea nafasi hizo.
Source : ITV Tanzania

Akiongea kwa jazba Katibu Mkuu wa CCM alisema onyo hilo pia linawahusu Waziri ktk Afisi ya Rais (TAMISEMI) anayesimamia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Suleiman Jaffo ambaye ofisi yake ilushiriki moja kwa moja kuratibu chaguzi za mitaa na vijiji pia onyo hilo alipewa Msajili wa Vyama Vingi vya Siasa Mh. Judge Francis Mutungi kuwa wasitoe nafasi kwa balozi hizo za nje kuwa na mazungumzo nao kuhusu uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijiji ama sivyo vigogo hao wa serikali watapoteza ajira zao.

Uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijiji ulingia dosari na kusababisha vyama vikuu vya siasa nchini Tanzania kujitoa na kukiachia CCM kupitisha wagombea wake bila washindani hivyo kupelekea chama hicho kikongwe cha siasa Afrika kupata 'ushindi' wa asilimia 99.9.
 
Kabudi ni mzushi na tapeli.
 
sijaelewa maana ya neno anayoturai! nafikiri mhusika alitaka kutafsiri neno coax in swahili in short from a word "rai".

suppossed to read "anayoturaia"! yaani noun to verb or use neno "himiza"

(Kar)


ra.i1* kt [ele] 1 coax. 2 feed sb (as a sign of affection). (tde) raia, (tden) raiana, (tdew) raiwa; (tdk) raika; (tds) raisha. (Kar)


rai2* nm [i-/zi-] view, opinion. (Kar)


rai3* nm [i-/zi-] health: Sina ~ I am not in good health. (Kar)

 
Jaji Mkuu Afungukia Sakata la Tundu Lissu, Akataa Kujifananisha na Majaji wa Kenya

Published on 21 Sep 2017


JAJI MKUU wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, leo amesema shambulio la kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, ni kitendo cha uhalifu mkubwa hivyo kitu cha kwanza kinachotakiwa kufanywa ni kukusanya ushahidi ili upelekwe mahakamani.
Jaji Mkuu huyo alifafanua hilo baada ya kutupiwa swali na mwandishi wa habari kuhusu waraka wa Chama cha Wanasheria cha Bar Human Rights Comitee cha Uingereza ambacho kimezungumzia tukio la kushambuliwa kwa kiongozi huyo kwenye barua yao waliyoiandika na kumpelekea Rais Dk. John Magufuli.

Profesa Juma alisema tukio la Lissu linahitaji kukusanywa kwa ushahidi. “Ushahidi huo utakusanywa hapa nchini, asikudanye mtu kuwa kuna mtu atatoka nje aje kukusanya ushahidi hapa nchini, ushahidi utakusanywa hapahapa Tanzania, sasa sisi mahakamani kanuni zetu haturuhusiwi kuongelea jambo ambalo tunaona litaletwa mahakamani.

“Ndiyo maana mnatuona kimya, kwenye mitandao watu wanajaribu kutuvuta lakini hatutaweza kusema chochote,” alisema.

Jaji Mkuu akaongeza :”Tutakapoona waliopewa jukumu la kukusanya ushahidi wameshindwa kufanya hivyo ndiyo tupige kelele kwani hata waraka unahimiza uchunguzi ufanywe na wahusika wapelekwe mahakamani.”

Source: Global TV online
 
Wahusika wa kukusanya Ushahidi kuhusu shambulio la risasi dhidi ya Tundu Lissu, habari hii ni kaa la moto mpaka sasa, hivyo hakuna anayetaka kuji commit sijui kwanini wameingia gazi na hawataki kabisa kulizungumzia.
 
November 25, 2019
Dar - Es - Salaam, Tanzania

CCM ni chama dola kinaendeshwa kwa vitisho, kimekosa ushawishi na hivyo kimekosa sifa ya kuitwa chama cha siasa.

Mwalimu Lwaitama asema ni hatari sana jinsi CCM walivyobinya demokrasia ktk uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijijini uliofanyika November 24, 2019 nchini kote Tanzania.


Mwalimu Lwaitama akaenda mbali zaidi na kuonesha hofu kuwa inawezekana CCM wakafanya uchafuzi wa uchaguzi hata ktk ngazi ya chaguzi za wabunge na Rais mwaka 2020.

Watanzania wengi wanahoji ikiwa CCM kimeogopa uchaguzi wa ngazi za mitaa na serikali za vijiji, hivi kweli hofu yao CCM haitakuwa maradufu na kufanya uchafuzi wa ajabu ktk Uchaguzi Mkuu wa kupata wabunge na Rais ambapo chama kitachopata wabunge wengi huunda serikali. Uchaguzi huo mkuu unatarajiwa kufanyika October 2020.
Source: ABC habari
 

Duh! yuko Kenya, ameanza kusogea....naona anawabip hao jamaa wasiojulikana ila asipokua makini wanaweza wakampigia simu hata akiwa Nairobi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…