Swali Fyatu la Wiki: Yote Sawa? Mapenzi ya Kinafiki au Heshima ya Woga?

Swali Fyatu la Wiki: Yote Sawa? Mapenzi ya Kinafiki au Heshima ya Woga?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Na. M. M. Mwanakijiji
images.jpeg

Sijui lipi ni bora katika siasa au yote ni sawa tu? Yaani, unamheshimu mtu si kwa sababu anastahili heshima hiyo bali kwa vile unamuogopa. Unaogopa huyo mtu atakufanya nini. Unajitahidi kumfurahisha kwa sababu hutaki achukie au akushukie. Akinuna unaweweseka. Unajua humpendi lakini ufanye nini wakati yeye kashika mpini.

Au, unamuonesha mtu mapenzi kwa sababu hutaki akufanye lolote na yeye hakufanyi lolote kwa sababu anaamini unamuo. nesha mapenzi. Unamsifia na kumuonesha heshima kwa sababu atakuzawadia mapenzi yake. Unataka na wewe akuone unampenda. Akikasirika anaweza kukunyima vitu na hilo wazo linakutisha.

Kumbe ukiangalia utaona kuwa heshima ya woga na penzi la kinafiki ni pande mbili za sarafu moja. Vyote viwili msingi wake ni khofu. Lakini, Kuna watu wanaamini kimojawapo ni nafuu.

Yaani, mmoja anaweza kukupa sumu kwa sababu hakupendi ila mwingine anaweza kukupa sumu ukiamini anakupenda.

Go figure.
MMM
 
Utii unaosababishwa na hofu ni hatari..
Mapenzi yakinafiki nayo ni hatari...

Utii wa hofu dhidi ya Ghadafi pale Libya ndio umeleta maafa mpaka leo, maana watu walimtii wakiwa na vinyongo, lilikuwa suala la muda tu..

Utii wa hofu kwa Saadam Hussein pale Iraq ulizaa unafiki uliomsubiri Saadam afe au atoke madarakani, matokeo yake ni chuki mpaka leo, uasi umeibuka kila mahala..

Nina wasiwasi na nchi moja jirani yetu kuna Giant siku akianguka tu nako yatatokea maafa maana kuna kabila linamtii kwa sababu ya uoga, siku akianguka lazima lilipe kisasi na kudai haki zao wanazonyimwa miaka yoote..

Utii wa kweli na upendo wa kweli ndio vitu tulivyohubiliwa kwenye vitabu vitakatifu au hata kwenye mila na desturi....Unafiki na Utii kwa sababu ya woga havina tofauti na jamii ya kichawi inayosubiri kubwa la wachawi afe waanze kumla nyama....

Tupendana, tuipende Tanzania, siasa hizi ni uchafu ambao mwisho wake ni hatari....
 
Hoja murua kabisa, hakuna mapenzi ya dhati isipokuwa ni unafiki umetawala kutokana na hofu.
Screenshot_20220404-200005.jpg
 
Kumbe ukiangalia utaona kuwa heshima ya woga na penzi la kinafiki ni pande mbili za sarafu moja. Vyote viwili msingi wake ni khofu. Lakini, Kuna watu wanaamini kimojawapo ni nafuu.
Hakuna chenye unafuu hapo, Sana Sana ni kujitesa tu.

Ila unafiki na kujipendekeza ni sehemu muhimu ya siasa za hii nchi, hivyo tuendelee tu na maisha waliyoyachagua wenye kushika mpini.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sijui lipi ni bora katika siasa au yote ni sawa tu? Yaani, unamheshimu mtu si kwa sababu anastahili heshima hiyo bali kwa vile unamuogopa. Unaogopa huyo mtu atakufanya nini. Unajitahidi kumfurahisha kwa sababu hutaki achukie au akushukie. Akinuna unaweweseka. Unajua humpendi lakini ufanye nini wakati yeye kashika mpini.

Au, unamuonesha mtu mapenzi kwa sababu hutaki akufanye lolote na yeye hakufanyi lolote kwa sababu anaamini unamuo. nesha mapenzi. Unamsifia na kumuonesha heshima kwa sababu atakuzawadia mapenzi yake. Unataka na wewe akuone unampenda. Akikasirika anaweza kukunyima vitu na hilo wazo linakutisha.

Kumbe ukiangalia utaona kuwa heshima ya woga na penzi la kinafiki ni pande mbili za sarafu moja. Vyote viwili msingi wake ni khofu. Lakini, Kuna watu wanaamini kimojawapo ni nafuu.

Yaani, mmoja anaweza kukupa sumu kwa sababu hakupendi ila mwingine anaweza kukupa sumu ukiamini anakupenda.

Go figure.
MMM
MMM katika ubora wako
 
Kama Taifa natamani tutoke kwenye hivyo vifungo, vyote viwili ni mateso kwa Taifa, aliyeanzisha hii tabia anastahili kulaaniwa.
 
Siasa za kiafrika zimejaa unafiki tu
 
Kweli Dunia inakimbia yaani mwanakijiji anaanzishai siredi' inachangiwa na watu 15 Kwa masaa 48!
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sijui lipi ni bora katika siasa au yote ni sawa tu? Yaani, unamheshimu mtu si kwa sababu anastahili heshima hiyo bali kwa vile unamuogopa. Unaogopa huyo mtu atakufanya nini. Unajitahidi kumfurahisha kwa sababu hutaki achukie au akushukie. Akinuna unaweweseka. Unajua humpendi lakini ufanye nini wakati yeye kashika mpini.

Au, unamuonesha mtu mapenzi kwa sababu hutaki akufanye lolote na yeye hakufanyi lolote kwa sababu anaamini unamuo. nesha mapenzi. Unamsifia na kumuonesha heshima kwa sababu atakuzawadia mapenzi yake. Unataka na wewe akuone unampenda. Akikasirika anaweza kukunyima vitu na hilo wazo linakutisha.

Kumbe ukiangalia utaona kuwa heshima ya woga na penzi la kinafiki ni pande mbili za sarafu moja. Vyote viwili msingi wake ni khofu. Lakini, Kuna watu wanaamini kimojawapo ni nafuu.

Yaani, mmoja anaweza kukupa sumu kwa sababu hakupendi ila mwingine anaweza kukupa sumu ukiamini anakupenda.

Go figure.
MMM
Cc.
Dr slaa aione kwenye sahani ya mihogo
 
Mwanakijiji mtetezi wa udikteta..
Enzi za mwendazake ulikuwa wa ovyo kabisa we mzee.
 
Back
Top Bottom