Swali halijibu swali!

Swali halijibu swali!

Mashairi ni matamu,
Je yatashika tamu?
Katika enzi za hujumu,
Tumeipoteza elimu.
 
Kiranga.. you and I agree that when a question is posed so as to help in answering another question then the second question is part of an answer. Mtu akiuliza swali ambalo halisaidii kujibu swali aliloulizwa basi anakwepa au anakebehi mchakato mzima wa mazungumzo. Hivyo, kwangu mimi swali haliwezi kuwa lenyewe ni mwisho wa swali jingine. Lakini, wakati wowote linapotumika kujibu swali basi naamini swali hilo ni sehemu ya jibu.
 
Kweli Mwanakijiji,
Maana kweli haiji,
Swali likizidi lahoji,
Jibu pia lisihoji.

Ya kale kutupa njia,
Na hekima kutujia,
Swali linapotujia,
Na jibu lipate njia.

Mpanda ngazi hushuka,
Mkwezi hutelemka,
Mimi siyo mahoka,
Ukajifanya kucheka.

Mwanamke kuwepo,
Na mwanaume kawepo,
Kama vile usiku upo,
Na mchana pia upo.

Nami nakuunga mkono
Wala sitalala pono,
Kujenga lugha nono,
Ifaayo kwa maono.
 
Swali halijibu swali
hapo naunga mkono
kamwe haijalishi hali
swali lahitaji jibu!

Ati unaenda wapi
ama jina lako nani
Dada yako yuko wapi
swali lahitaji jibu!

Kwanini wataka jua
ama "kwani lakuhusu nini?"
nia gani wamtakia
swali halijibu swali!

Mzee Mwanakijiji
nina hoja ya nyongeza
enzi si za kijiji
swali halijibu swali!

Wandugu hawana utu
si wema kwa kila kitu
wakikuuliza kitu
wana mioyo ya kutu.

Dadangu wamtakiani
ama mliaganani
labda wamfatilia
maisha kumharibia.

Niendapo kwakuhusuni
Kama wewe si muhuni
sihitaji sindikizwa
labda wataka niuza.

Jamii meharibika
siku hizi hakuna kaka
huyu kauliza hivi
hujui yake moyoni!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom