Nadhani tatizo umeli create mwenyewe hapa, inaonekana una nia ya kusoma MBA thats fine, unaweza kusoma popote. Maana siku hizi ajira zinatolewa kulingana na sifa na pengine zinatolewa kindugu na hakuna mahali watakaposema tunataka MBA za UD au Mzumbe, so ni ruksa kusoma popote. Ila ukweli kwamba Chuo hicho wanakiponda una details zaidi wewe uliyesema. Kila chuo kina madhaifu yake, mengine ya kweli mengine si ya kweli, jukumu ni kwako kupima vizuri kabla hujafanya maamuzi. Ila asikudanganye mtu kwamba UD au MZUMBE ndio Best. Sisi tuliosoma UD sana sana tulijifunza personality part of our lecturers than materials walizokuwa wanatufundisha. Kuna kozi mwl aliingia siku moja tu na tukafanya final yake na tukafeli lakini hakuna aliyelalamika maana ukilalamika ndio humalizi hiyo masters, mwl lengo lake ni kutupa sup hayo tuliyakubali lakini ni changamoto za kawaida. Sisemi uende huko kwa sababu hutapata SUP ila kwa sababu utaenda kutia juhudi ili utoke na ufahamu hicho ndo cha muhimu. Asikudangaye mtu vyuo vikuu sio sekondari, wala hakuna guarantee ya kutoka mzuri peculiar kwa sababu ya kusoma UD au MZUMBE au IFM, mapoyoyo yapo mengi sana vile vile.