Swali kuhusu ule Mkongo wa Taifa (Fibre Optic)

Soki

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
1,303
Reaction score
279
Naomba kufahamu mambo kadhaa kuhusu mkongo wa Taifa:

1. Je umekamilika?

2. Je tumeshaanza kuutumia? Kama jibu ni ndiyo, mbona basi speed ya internet iko vilevile kama zamani na mbona bei hazijashuka kama ilivyotarajiwa?

3. Kama haujakamilika, je ukikamilika kutakuwa na unafuu wowote au ni PROPAGANDA TU?

Najua hapa JF kuna watu wanaojua. Naomba mtujuze tafadhali.

Ahsanteni!
 

Au pengine hii topic inatakiwa PIA ijibiwe na wanasiasa? Naona swala la lini labda ningelipeleka kwenye jukwaa la siasa. Lakini kuna mengi ya kisayansi na kiufundi pia katika mada hii. Pia BAADHI ya wanasiasa hutembelea jukwaa hili la sayansi pia hivyo wataweza kutusaidia.
 
Umeshaanza kutumika kipindi na nafuu ya speed ipo na bei imepungua kwa kiwango kikubwa sana. Kutokuwepo kwa speed naona inategemea na ISP na kiwango cha band-with kilichonunuliwa
 
Umeshaanza kutumika kipindi na nafuu ya speed ipo na bei imepungua kwa kiwango kikubwa sana. Kutokuwepo kwa speed naona inategemea na ISP na kiwango cha band-with kilichonunuliwa

Kumbe tatizo langu ni kwamba nilikuwa nina matarajio makubwa zaidi!! Nilitarajia kuweza kudownload movies faster zaidi na ku-watch live progrmmes na kuweza kupiga nje ya nchi kwa nafuu zaidi. Au pengine bado wataboresha zaidi??
 
Haujakamilika in the sense kuwa zile link za kusambaza nchi nzima bado hazijakamilika.

Bei zimepungua sana angalia package ya Unlimited Voda au bei za broadband ya TTCL sasa hivi ukifananisha na kabla ya fiber.

Nadhani kushuka zaidi mpaka ije cable itakayoleta ushindani maana investment ya kujenga fiber ya baharini ni kubwa sana, so bei haziwezi kuwa low.
 
Kama nakumbuka vizuri mwaka jana wakati haya mambo yanaiva kulikuwa na optic fiber cable companies/consortiums tatu. Hivyo kam zote zimeanza kufanya kazi ushindani unapaswa kuwepo.
 
Umeshaanza kutumika kipindi na nafuu ya speed ipo na bei imepungua kwa kiwango kikubwa sana. Kutokuwepo kwa speed naona inategemea na ISP na kiwango cha band-with kilichonunuliwa

na sehemu ulipo
 
na sehemu ulipo

Nilidhani makampuni ya simu kama voda, airtel, tigo, n.k, ndo wanajinga na sisi tunaipata through wao sehemu popote ulipo! sasa kumbe kuna swala la sehemu ulipo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…