Swali kwa Waziri wa Mazingira, Dkt Suleiman Jaffo: Watumishi wa umma 333 wamefuata nini kwenye mkutano wa COP28 huko Dubai?

Mtoto wa Samia, Abdul - Halim Hafidh Ameir ameandikwa ni National delegate.

Swali la kujiuliza huyu mtu ni National delegate kutoka taasisi ipi?

Hii ni serious state capture.
Hapo president office hujaona mkuu....acheni watumishi nao wale mema ya nchi ingawaje sijaona hapo wizara ya elimu ikimaanisha kwamba walimu wamewekwa kando kwenye huu ulaji.​
 
Kama walitenga bajeti au kama uhusiano wao mzuri na Dubai umewasaidia kupeleka watu wengi COP28 hilo ni jambo la kupongeza!
Climate Change is a serious threat to humanity. And global conferences the right spot to negotiate and deliberate on the matter.
Mama Amon ungetuletea pia event schedules ili tujue je kwa idadi ya watu walioenda COP28 EXPO CITY wanaweza kuhudhuria kila major event na side events??
Hata hivyo tujenge interest ya kuhudhuria matukio ya kimataifa yenye relevance kubwa kwetu!
 
Mwisho wa mwaka huu, ni muda wa watu kutoana out baada ya kazi ngumu ya kutafuta pesa na visirani vya kukwaruzana na mabosi.
Swali ni je, hao wote wamelipiwa na serikali? Bila shaka jibu ni hapana.
 
Wachache sana hao, ilitakiwa kila watu 1000 angalau wawakilishwe na mtu mmoja.
 
Per diem za kutosha[emoji4]
Hebu tupige hesabu kidogo:
Kwa maafisa wa serikali (na hasa wale wanaokwenda kwenye COP huwa ni Principal Officers and above) = USD (420+incidental 84) = 504/day x 14 days = 7,056, hapo bado ticket na kwa wale wakurugenzi, makatibu wakuu na mawaziri ongeza na enterterinment allowance (?). Tickets kwa PS na wajuu ni kuanzia Business class.

Hesabu yangu ya darasa la saba imekomea hapo.
 
Hapo president office hujaona mkuu....acheni watumishi nao wale mema ya nchi ingawaje sijaona hapo wizara ya elimu ikimaanisha kwamba walimu wamewekwa kando kwenye huu ulaji.​
Watu wamebeba hadi vimada wao!

Marehemu Bob Marley alisema ni rahisi kudanganya watu wote , ila sio rahisi kudanganya watu wote kwa wakati wote .
 
Hao ni watu wa "State Capture." Ikumbukwe kuwa Climate Change is a falsified agenda ya NWO,kwa hiyo agents wa NWO lazima wahudhurie kwa wingi ili ionekane kwamba inaungwa mkono.
 
Wanafanya hayo huku barabara Jiji la Dar tu ni mahandaki kila kona.

Nenda hospital yaani facilities ni chakavu mpaka inatia huruma.

Ipo haja wahusika wajiuzulu nafasi zao.

Haya ni matumizi mabaya ya fedha za umma.
Ccm ni ile ile oh ni ile ile
 
Hivi tuna uhakika kuwa hawa viongozi ni binadamu wenzetu kweli?
Idije ikawa tunawaona binadamu kwa macho ya kawaida kumbe sio binadamu wa kweli!
 
Hao ni watu wa "State Capture." Ikumbukwe kuwa Climate Change is a falsified agenda ya NWO,kwa hiyo agents wa NWO lazima wahudhurie kwa wingi ili ionekane kwamba inaungwa mkono.
Yaa naona hizi ishu za climate change, pandemic (covid), cyberattack wale jamaa wa agenda 2030 wanazichukulia kama agenda zao za kutaka kuleta mabadiliko mbalimbali kwenye mifumo ikiwemo kutoa utambulisho kwa kila mwanadamu (unique ID), wanasema 'you will own nothing and be happy' na kwamba watu watakuwa wanakula wadudu.......hatari sana hawa watu.​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…