Swali la kizushi - Je Pesa za TFF zinazodaiwa kupigwa na Malinzi ni Mali ya Umma ?

Swali la kizushi - Je Pesa za TFF zinazodaiwa kupigwa na Malinzi ni Mali ya Umma ?

Soka inagusa maslahi ya umma. Kwa maana hiyo ni za umma.

TFF ina taratibu na kanuni zake. Ukiukwaji wowote unaweza kuhatarisha maslahi ya sehemu au umma wote. Serikali haiwezi kufumba macho

Ndiyo maana serikali hutoa ulinzi wa Polisi kwenye mechi kwa maslahi ya umma.

Hata hela za vicoba ni za umma kwa maana hizo hizo. Mtu akifuja au kutumia kinyume cha kanuni za wanakiboba anashughulikiwa kuepuka uvunjaji wa amani
 
Kuna watu waajabu sana hivi unajitokeza kutetea mtu kama Malinzi!. Kila nikimfikiria yule Nahodha wa Serengeti Boys aliyetelekezwa napata hasira sana na hao watu!
Mkuu kuna watu wapuuzi sana, mimi nilifika kwa yule nahodha anaishi mazingira magumu sana, anasema walipewa nauli na fedha ya kula njia hawajalipwa posho wote. Ina maana fedha zote zilizotolewa na Serengeti jamaa katia ndani ili kujiandaa na uchaguzi.
 
mnamuona malinzi tu je maney loundering ya simba ni za uma? mwizi ni mwizi na wakiachwa serikali itaonekana ya ovyo takukuru kamata wote Hans Pop alishaonjeshwa bado MO na yeye. ajiandae
Hata za Simba ni za umma wa wana Simba
 
Rushwa ni matumizi mabaya ya ofisi ya uma kwa manufaa binafsi (civics form 2) ..so simba na tff ni za Mali za uma..

Hata kashfa ya blater Wa FIFA iliendeswa na FBI
 
Mkuu kuna watu wapuuzi sana, mimi nilifika kwa yule nahodha anaishi mazingira magumu sana, anasema walipewa nauli na fedha ya kula njia hawajalipwa posho wote. Ina maana fedha zote zilizotolewa na Serengeti jamaa katia ndani ili kujiandaa na uchaguzi.
Huyu jamaa hastahili kuongoza soka. Pia nami nilijitahidi kumuona.
Kijana wa watu utamkuta amejikunyata kwenye uwanja wa Dundie akitizama wenzake wanavyofurahia vipaji vyao. Maskini, hajui aafanyaje na wala hakuna wa kumsaidia kinachosikitisha ni kwamba ameumia wakati akiliwakilisha taifa!
 
kuna watu waligeuza michezi kuwa kichaka cha wizi takukuru imepewa meno pia kumbuka Zanzibar hawajapata uwanachama wa FIFA sababu sio nchi hivyo ni lazima kuwepi nchi ndipo kipatikane chama cha soka
 
Nadhani unapaswa kwanza kujua nini maana ya "uma"

Serikali kutoingilia masuala ya soka... je wizi ni suala la soka?

Uhalifu ni uhalifu tu. Au kwamfano Malinzi angefanya mauaji angeachwa kwakuwa FIFA imekataza serikali kutoingilia masuala ya soka?

Kama hajakuelewa hapa basi hatokuja kuelewa tena. Safi sana Mkuu nimelipenda jibu lako ulilompa kwani ni ' Kuntu '.
 
Nimeuliza makusudi ili nipate ufafanuzi .

Kuna fungu lolote kutoka serikalini linatengwa na kuingizwa kwenye akaunti ya TFF ? Nakumbuka wakati wa FAT ya Muhidin Ndolanga , FIFA ilipiga Marufuku kwa serikali kuingilia masuala ya soka , sasa siku hizi FIFA wamebadili msimamo wao ?

Je hela zile ni za Umma ama ni mchango wa FIFA kwa TFF ?
Hata mchango wa FIFA kwa TFF ni fedha za umma.

Kwa sababu zinatolewa kuendeleza soka la umma wa Watanzania, hazijatolewa achukue mtu mmoja.
 
Kazi yetu vidonge ni kutuliza maumivu au kutibu. Nimetimiza wajibu wetu.

Safi sana Mkuu na nimeipenda hiyo. Sisi humu JF tukikuona ' unakengeuka / unapotoka / unakosea ' basi Kazi yetu huwa ni rahisi mno ya kukupa ' dozi ' mujarab kabisa ili ikuingie na ikuponye vizuri na haraka hasa ' Kifikra / Kiakili '. Tupo pamoja mwana ' dawa ' mwenzangu.
 
Kuna watu waajabu sana hivi unajitokeza kutetea mtu kama Malinzi!. Kila nikimfikiria yule Nahodha wa Serengeti Boys aliyetelekezwa napata hasira sana na hao watu!
Pamezuka mtindo wa mawakili huru JF kutetea uovu alimradi pawe na pande mbili jinai zinawekwa wazi kisha pana watu wanajitoa ufahamu na kutetea ndipo tulipofika hapa ndugu.
 
Mkuu kuna watu wapuuzi sana, mimi nilifika kwa yule nahodha anaishi mazingira magumu sana, anasema walipewa nauli na fedha ya kula njia hawajalipwa posho wote. Ina maana fedha zote zilizotolewa na Serengeti jamaa katia ndani ili kujiandaa na uchaguzi.
Huyo nahodha anaishi maeneo gani? Nahitaji kwenda kumuona..
 
Mkuu kuna watu wapuuzi sana, mimi nilifika kwa yule nahodha anaishi mazingira magumu sana, anasema walipewa nauli na fedha ya kula njia hawajalipwa posho wote. Ina maana fedha zote zilizotolewa na Serengeti jamaa katia ndani ili kujiandaa na uchaguzi.
Mwesigwa alimtembelea huyo dogo majuzi kati ila kijana huyo pia alionekana na mtoto wa 2 yrs!!!
 
  • Thanks
Reactions: R.B
Mwesigwa alimtembelea huyo dogo majuzi kati ila kijana huyo pia alionekana na mtoto wa 2 yrs!!!
Aache uongo. Tena anapata dhambi sana na ndio maana yanamkuta mabaya. Hayo analiyoyasema hayana ukweli. Sidhani kama alishawahi fika Hazina kwa Mzee Makamba. Wanatafuta sababu ya kumtompa matibabu.
 
Back
Top Bottom