SWALI LA KIZUSHI: Kwa nini aliyepata Divisheni Ziro azuiwe kujiunga Chuo?

SWALI LA KIZUSHI: Kwa nini aliyepata Divisheni Ziro azuiwe kujiunga Chuo?

Yule ziro mbona alimaliza miaka kumi kulikua na shida gani ? na kama zero in janga kwa nini na yenyewe iitwe division hoja ipo hapa hakuna mwenye division zero anaetembea uchi huyu nae asome chuo.
Hapo tatizo liko wapi? Fursa sawa iwe kwa wote. Kupata ziro siyo mwisho wa dunia. Ni siyo?
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Wana uwezo mkubwa wa kujiongeza,halaf pia Wana maneno ya shombo.

Asante kwa kutambua hayo yanayotuongezea haki ya kujiunga na chuo.
 
Ni wewe huyu [emoji28]
Screenshot_20190714-093303.jpeg
 
Unapofeli kwenye eneo moja, ni fursa nyingine ya kuongeza juhudi kwenye eneo hilohilo au kujaribu eneo jingine. Kama umefeli shule basi jaribu kazi za nguvu kama kilimo, uvuvi, biashara, kucheza dance n.k
Lengo la kukupatia elimu wewe si tu ikufae wewe, bali hata jamii inayokuzunguka inufaike. Sasa kila taaluma ina sifa zake kulingana na uzito wa taaluma yenyewe, sasa sifa za kuingilia kusoma hizo kozi huna, maana yake hufai. Kulazimisha kukuchukua ni kutaka kujaza nafasi ambazo zinawastahili wenye sifa zao ambazo huna.

Ikiwa nitashindwa kwenye ushindani dhidi ya wenzangu waliopata maksi nyingi kunizidi, hapo hakuna neno. Hata wenye divisheni wani kali hukosa nafasi kwa kuzidiwa na wenye divisheni wani kali zaidi. Lakini nipewe fursa ya kujiunga, nishindwe mwenyewe.
 
Inakuaje unataga form six??yaani umeacha kutagia form four wew umekuja kutaga form six
 
Yule ziro mbona alimaliza miaka kumi kulikua na shida gani ? na kama zero in janga kwa nini na yenyewe iitwe division hoja ipo hapa hakuna mwenye division zero anaetembea uchi huyu nae asome chuo.

Wanavyonyanyasa divisheni ziro utadhani divisheni ziro ni sawa na kuiba mitihani. Yaani mpaka unaweza kudhani kwamba lengo lao ni watu wachache wapate elimu ya juu tusije tukawa wengi kukawa hakuna ujaiko wa kuwa na digirii.
 
Mwenye kisu kikali ndiye anaruhusiwa kula nyama wewe kisu chako ni butu huna budi kula kwa macho.

Mpaka hapo nimeeleweka nini namaanisha.
 
Mwenye kisu kikali ndiye anaruhusiwa kula nyama wewe kisu chako ni butu huna budi kula kwa macho.

Mpaka hapo nimeeleweka nini namaanisha.

Kisu kikali = siyo divisheni ziro
Kisu butu = divisheni ziro
Nyama = Kusoma chuo

Asante sana kwa kuunga mkono hoja. Mimi mwenye kisu butu (ziro) nishindanishwe kukata nyama na mwenye kisu kikali (siyo ziro) halafu tuone nani ataondoka na nyama. Siyo ukiangalie kisu changu butu na kuniambia hata kujaribu kukata nyama usijaribu maana hutafanikiwa. Umenifahamu?
 
Ikiwa nitashindwa kwenye ushindani dhidi ya wenzangu waliopata maksi nyingi kunizidi, hapo hakuna neno. Hata wenye divisheni wani kali hukosa nafasi kwa kuzidiwa na wenye divisheni wani kali zaidi. Lakini nipewe fursa ya kujiunga, nishindwe mwenyewe.
Zamani kulikuwa na Marticulation Exam ambao ulitumika kuwachuja wanaostahili kujiunga na chuo. Utaratibu huo ulikuja kufutwa, na kuacha kipimo kiwe ni mtihani wa taifa wa form six na diploma kwa wale wa equivalent.
Kwahiyo unatakiwa ujue kuwa ukifeli form six umefeli kipimo cha kuingia chuo chochote kwa ngazi ya digrii. Chukua cheti chako cha form four kaanze certificate.
 
Zamani kulikuwa na Marticulation Exam ambao ulitumika kuwachuja wanaostahili kujiunga na chuo. Utaratibu huo ulikuja kufutwa, na kuacha kipimo kiwe ni mtihani wa taifa wa form six na diploma kwa wale wa equivalent.
Kwahiyo unatakiwa ujue kuwa ukifeli form six umefeli kipimo cha kuingia chuo chochote kwa ngazi ya digrii. Chukua cheti chako cha form four kaanze certificate.

Asante iamokay , umeelezea hali ilivyo. Sasa tueleze kwa nini isibadilishwe ili chuo wadahili kila mtu, wabakie kushindana tu ukubwa wa maksi. Kwa sasa wanaona ni vema nafasi ziende tupu kuliko kuruhusu wenye ziro.
 
Chuo nasikia mkifika mnaanza sufuri. Mwalimu anawafundisha mwenyewe, anatunga mtihani mwenyewe, anasahihisha mwenyewe, maksi anatoa yeye. Unafelije kwa mfano? Ukifeli unapewa supu, unarudia mtihani. Ukiifeli mtihani wa supu unarudia tena somo mwaka mwingine. Nani atashindwa shule ya hivyo?
Lol,
kweli wana haki ya kufungia division zero zisipate hata cheti.
 
Sasa kama unaamini kila kitu ni chako na hasara zoote za kwako...

Kwa nin usijilipie ada mwenyewe ukasomea chumbani kwako.. Ukifeli ujione mwenyewe tu mkuu?
 
Back
Top Bottom