Swali la Ugomvi: Kwani Wenzetu Hawa Walisomea Nini? - Part 1

Swali la Ugomvi: Kwani Wenzetu Hawa Walisomea Nini? - Part 1

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! Maswali au mambo mengine wakati fulani yanakwaza na yanaweza kukufanya ufike mahali utamani kujinyofoa nywele.

Mojawapo ya maswali ambayo yameanza kunijia siku hizi za karibuni ni hili kuhusu "ndugu zetu hawa". Hawa ndugu zetu wamekuwa wakija kila baada ya miaka mitano kuomba uongozi; wanabembeleza tena wameshika kakitabu kanaitwa "Ilani ya Uchaguzi". Ukiishika hiyo Ilani imejazwa maneno na ahadi nyingi tena ziko kwenye vifungu vyenye namba ili usindishwe kunukuu. Watakuja na muziki na bendi; vikundi vya sarakasi, na ngoma za kienyeji na ngonjera! Wakati mwingine watawaalika waimba mashairi na tenzi zenye mwendo wa taarab kabambe!

Yaani, ukichukua Ilani ya Uchaguzi ya chama chao kuanzia tu na mwaka 1995 hadi sasa kuna ahadi zimetolewa humo kuhusu suala la nishati na tatizo la umeme nchini hadi unajiuliza hivi huwa wanakumbuka walichoahidi miaka mitano kabla yake? Au inawezekana kila unapokaribia uchaguzi mwingine wanaanza kuangalia na kusema "duh mbona tatizo bado lipo, hebu tuahidi tena"! Halafu wanakaa na kuja na ilani nyingine halafu tunarudia tena.

Sasa tatizo sijui ni wanasiasa au ni watendaji. Hili ndilo linanileta kwenye swali la leo. Hivi kuna uwezekano hawa ndugu zetu waliingia shuleni lakini shule haikuwaingia? Hivi watu wote waliosomea shahada za sayansi na saa katika umeme, utawala, uongozi na menejimenti; wote waliosomea mambo ya fedha n.k Hivi ni kweli kabisa hawa watu wameshindwa kabisa kutatua hili tatizo la umeme? Yaani, tunachoshuhudia hadi leo hii ni upeo wa uwezo wao!

Huwa nasema "upeo wetu, ndio ukomo wetu". Yaani, ukijumlisha elimu ya watu wote kwenye serikali - wizara, idara, na wakala mbalimbali; yaani ukijumlisha uwezo wao wote jumla yake ni "tatizo la umeme". Yaani, kwa miaka yote hii walipoenda shule, kozi, na mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi ukijumlisha vyote hivyo jumla yake ni hii: Tatizo lisiloisha la umeme. Yaani, kukatika katika kwa umeme, mgao wa mara kwa mara n.k yote haya ni jumla ya elimu ya viongozi na watendaji ndani ya serikali hadi mitaani kabisa.

Ndio maana leo najiuliza; hivi hawa wenzetu wanaosimamia sekta hii ya umeme kwa miaka yote hii walipoenda shule ambapo walisifiwa kuwa hawakupata makarai au mayai; kwamba wanasiwa kuwa wao ndio walikuwa "vipanga"; yaani maprofesa waliowafundisha na wanafunzi waliosifiwa kuwa walipata "Upper Class" kwenye shahada zao za uzamaji, uvumaji, uvumbivu na uvunjifu yaani hawa ndugu walichosomea kilikuwa kitu gani?

Yaani, mnataka kabisa tuamini kuwa kama taifa na tunapoelekea miaka 60 ya Muungano uwezo wa wasomi wetu wabobezi ndio huu kwenye sekta ya umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! aya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Tanesco wanasaidia sana sio kwamba hawafanyi kazi hapana maana ukisema toka uhuru hadi sasa umeme umesambaa eneo kubwa sana nchi hii.

mimi ninachokiona uhitaji wa nishati ya umeme ni mkubwa kuliko budget ya serikali hao tanesco wanasubili bunge na serikali iwape pesa na bahati mbaya wanapata mgao kiduchu

Tanesco hawana pesa zao mfukoni.
Hakuna mkandarasi mbobevu au mkurugenzi eti yupo teyari kukaa sehemu ili ashindwe tatizo ni pesa na bahati mbaya zaidi hii nchi ilivyo ya hovyo wanasiasa ndio watoaji pesa haohao ndio wachukuaji 10 percent ya hizo pesa na haohao ndio watumbuaji ili wao wajikoshe..
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! Maswali au mambo mengine wakati fulani yanakwaza na yanaweza kukufanya ufike mahali utamani kujinyofoa nywele.
umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Africa Elimu na utendaji ni vitu viwili tofauti. Kinachosababisha tusipige hatua sio kwamba hatuna Elimu au Elimu zetu ni duni, bali ni ubinafsi mkubwa uliotujaa.

Mfano hapa Tz, Kila mtu ni mbinafsi kuanzia kiongozi hadi mwananchi. Kiongozi anafanya maamuzi kwa maslahi binafsi, mwananchi nae anafanya mambo kwa maslahi binafsi. Ni kawaida kumuona mtu akipigwa na polisi bila kosa lolote, alafu raia wengine wakaendelea na mishe zao bila kuhoji au kutaka kujua chochote (maana anayepigwa sio wao).

Unaweza kuona upande wa nishati haifanyi vizuri, lakini huo ni mtazamo wako wewe. Ila kwa upande wao, na malengo waliyonayo, Kila kitu kinaenda sawa. Huko unakoona ni kuboronga, wao ndivyo wanavyotaka.
 
Watakuja na muziki na bendi; vikundi vya sarakasi, na ngoma za kienyeji na ngonjera! Wakati mwingine watawaalika waimba mashairi na tenzi zenye mwendo wa taarab kabambe!
Utasikia, Piiiipoz.😂😂😂😂😂

Ila "hawa ndugu zetu" hawa, CHi Chiem nawavulia kofia kabisa, ndio nikune nywele zangu vizuri. Aisee

Ngoja wajipange tena.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna meme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Ulishapoteza Credibility baada ya kununuliwa na yule mwovu na kugeukia upande wa watesi!! Nakushangaa hii nguvu ya kutamka haya unaitoa wapi? Si ulikua upande wa aliyetaka kutawala milele?

Siku zote muda ni hakimu wa yote.... ungejikalia kimya tuu kuliko kujaribu kukirudia kichaka chako cha zamani, huaminiki zaidi sana unatia kinyaa!!
 
Yaani, mnataka kabisa tuamini kuwa kama taifa na tunapoelekea miaka 60 ya Muungano uwezo wa wasomi wetu wabobezi ndio huu kwenye sekta ya umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Wewe umechagua tatizo la "umeme"; hilo mimi ninaliona kama mfano mmoja tu wa mambo mengi (yote) tunayoshindwa kuyamudu, miaka zaidi ya 60 tokea tupate uhuru wetu. Tunaagiza njiti za kuchokonoa meno tukishashiba nyama choma huku tukijipongeza tunavyovutia wawekezaji wasiotuwezesha kutengeneza njiti hizo sisi wenyewe.

Mada yako, kama ilivyo mara nyingi ni ya msingi sana; lakini kama ujuavyo enzi hizi, hata hapa JF, kama mada haiendani na kuwa "chawa" huwezi kupata uchangiaji na uchambuzi wa kina.
 
Mkuu, uliunga mkono juhudi enzi ya JPM ukajua atakupa cheo, na yeye akafa, ukatoka patupu, heshima huna na cheo huna, miaka ile ungekuwa na comments elfu tano
Angalau magufuli alikuwa na uthubutu,tena akitumia tu common sense,hakuzingatia sana masuala ya usomi ulioshindwa, angeifikisha hii nchi pahala fulani,ila alikuwa some kind of dictator,hilo tu,MMk alipendezwa na hilo la kwanza,la pili hakuliona,he was not right but he was OK.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! Maswali au mambo mengine wakati fulani yanakwaza na yanaweza kukufanya ufike mahali utamani kujinyofoa nywele.

Mojawapo ya maswali ambayo yameanza kunijia siku hizi za karibuni ni hili kuhusu "ndugu zetu hawa". Hawa ndugu zetu wamekuwa wakija kila baada ya miaka mitano kuomba uongozi; wanabembeleza tena wameshika kakitabu kanaitwa "Ilani ya Uchaguzi". Ukiishika hiyo Ilani imejazwa maneno na ahadi nyingi tena ziko kwenye vifungu vyenye namba ili usindishwe kunukuu. Watakuja na muziki na bendi; vikundi vya sarakasi, na ngoma za kienyeji na ngonjera! Wakati mwingine watawaalika waimba mashairi na tenzi zenye mwendo wa taarab kabambe!

Yaani, ukichukua Ilani ya Uchaguzi ya chama chao kuanzia tu na mwaka 1995 hadi sasa kuna ahadi zimetolewa humo kuhusu suala la nishati na tatizo la umeme nchini hadi unajiuliza hivi huwa wanakumbuka walichoahidi miaka mitano kabla yake? Au inawezekana kila unapokaribia uchaguzi mwingine wanaanza kuangalia na kusema "duh mbona tatizo bado lipo, hebu tuahidi tena"! Halafu wanakaa na kuja na ilani nyingine halafu tunarudia tena.

Sasa tatizo sijui ni wanasiasa au ni watendaji. Hili ndilo linanileta kwenye swali la leo. Hivi kuna uwezekano hawa ndugu zetu waliingia shuleni lakini shule haikuwaingia? Hivi watu wote waliosomea shahada za sayansi na saa katika umeme, utawala, uongozi na menejimenti; wote waliosomea mambo ya fedha n.k Hivi ni kweli kabisa hawa watu wameshindwa kabisa kutatua hili tatizo la umeme? Yaani, tunachoshuhudia hadi leo hii ni upeo wa uwezo wao!

Huwa nasema "upeo wetu, ndio ukomo wetu". Yaani, ukijumlisha elimu ya watu wote kwenye serikali - wizara, idara, na wakala mbalimbali; yaani ukijumlisha uwezo wao wote jumla yake ni "tatizo la umeme". Yaani, kwa miaka yote hii walipoenda shule, kozi, na mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi ukijumlisha vyote hivyo jumla yake ni hii: Tatizo lisiloisha la umeme. Yaani, kukatika katika kwa umeme, mgao wa mara kwa mara n.k yote haya ni jumla ya elimu ya viongozi na watendaji ndani ya serikali hadi mitaani kabisa.

Ndio maana leo najiuliza; hivi hawa wenzetu wanaosimamia sekta hii ya umeme kwa miaka yote hii walipoenda shule ambapo walisifiwa kuwa hawakupata makarai au mayai; kwamba wanasiwa kuwa wao ndio walikuwa "vipanga"; yaani maprofesa waliowafundisha na wanafunzi waliosifiwa kuwa walipata "Upper Class" kwenye shahada zao za uzamaji, uvumaji, uvumbivu na uvunjifu yaani hawa ndugu walichosomea kilikuwa kitu gani?

Yaani, mnataka kabisa tuamini kuwa kama taifa na tunapoelekea miaka 60 ya Muungano uwezo wa wasomi wetu wabobezi ndio huu kwenye sekta ya umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Ni mpaka uwe kama wao ndio utawaelewa.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! Maswali au mambo mengine wakati fulani yanakwaza na yanaweza kukufanya ufike mahali utamani kujinyofoa nywele.

Mojawapo ya maswali ambayo yameanza kunijia siku hizi za karibuni ni hili kuhusu "ndugu zetu hawa". Hawa ndugu zetu wamekuwa wakija kila baada ya miaka mitano kuomba uongozi; wanabembeleza tena wameshika kakitabu kanaitwa "Ilani ya Uchaguzi". Ukiishika hiyo Ilani imejazwa maneno na ahadi nyingi tena ziko kwenye vifungu vyenye namba ili usindishwe kunukuu. Watakuja na muziki na bendi; vikundi vya sarakasi, na ngoma za kienyeji na ngonjera! Wakati mwingine watawaalika waimba mashairi na tenzi zenye mwendo wa taarab kabambe!

Yaani, ukichukua Ilani ya Uchaguzi ya chama chao kuanzia tu na mwaka 1995 hadi sasa kuna ahadi zimetolewa humo kuhusu suala la nishati na tatizo la umeme nchini hadi unajiuliza hivi huwa wanakumbuka walichoahidi miaka mitano kabla yake? Au inawezekana kila unapokaribia uchaguzi mwingine wanaanza kuangalia na kusema "duh mbona tatizo bado lipo, hebu tuahidi tena"! Halafu wanakaa na kuja na ilani nyingine halafu tunarudia tena.

Sasa tatizo sijui ni wanasiasa au ni watendaji. Hili ndilo linanileta kwenye swali la leo. Hivi kuna uwezekano hawa ndugu zetu waliingia shuleni lakini shule haikuwaingia? Hivi watu wote waliosomea shahada za sayansi na saa katika umeme, utawala, uongozi na menejimenti; wote waliosomea mambo ya fedha n.k Hivi ni kweli kabisa hawa watu wameshindwa kabisa kutatua hili tatizo la umeme? Yaani, tunachoshuhudia hadi leo hii ni upeo wa uwezo wao!

Huwa nasema "upeo wetu, ndio ukomo wetu". Yaani, ukijumlisha elimu ya watu wote kwenye serikali - wizara, idara, na wakala mbalimbali; yaani ukijumlisha uwezo wao wote jumla yake ni "tatizo la umeme". Yaani, kwa miaka yote hii walipoenda shule, kozi, na mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi ukijumlisha vyote hivyo jumla yake ni hii: Tatizo lisiloisha la umeme. Yaani, kukatika katika kwa umeme, mgao wa mara kwa mara n.k yote haya ni jumla ya elimu ya viongozi na watendaji ndani ya serikali hadi mitaani kabisa.

Ndio maana leo najiuliza; hivi hawa wenzetu wanaosimamia sekta hii ya umeme kwa miaka yote hii walipoenda shule ambapo walisifiwa kuwa hawakupata makarai au mayai; kwamba wanasiwa kuwa wao ndio walikuwa "vipanga"; yaani maprofesa waliowafundisha na wanafunzi waliosifiwa kuwa walipata "Upper Class" kwenye shahada zao za uzamaji, uvugumaji, uvumbivu na uvunjifu yaani hawa ndugu walichosomea kilikuwa kitu gani?

Yaani, mnataka kabisa tuamini kuwa kama taifa na tunapoelekea miaka 60 ya Muungano uwezo wa wasomi wetu wabobezi ndio huu kwenye sekta ya umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Tangu Nyerere aondoke madarakani hatujawahi kuwa na rais mwenye na nchi yetu na watu wake. Marais wote waliofuata kazi yao ilikuwa kujitajirisha wao na familia zao tu. Wanashindana kuiba pesa za umma sababu katiba inawaruhusu kuiba watakavyo na ndio maana hawataki ibadilishwe
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Sikuwahi kuelewa kwanini wakati mwingine mtu anapokuwa na mawazo au ametatizika kimawazo anaanza kujikuna nywele. Au mtu anakuuliza jambo halafu hauna jibu unaanza kujishika kidevu au unakuna nywele hata kama haziwashi! Maswali au mambo mengine wakati fulani yanakwaza na yanaweza kukufanya ufike mahali utamani kujinyofoa nywele.

Mojawapo ya maswali ambayo yameanza kunijia siku hizi za karibuni ni hili kuhusu "ndugu zetu hawa". Hawa ndugu zetu wamekuwa wakija kila baada ya miaka mitano kuomba uongozi; wanabembeleza tena wameshika kakitabu kanaitwa "Ilani ya Uchaguzi". Ukiishika hiyo Ilani imejazwa maneno na ahadi nyingi tena ziko kwenye vifungu vyenye namba ili usindishwe kunukuu. Watakuja na muziki na bendi; vikundi vya sarakasi, na ngoma za kienyeji na ngonjera! Wakati mwingine watawaalika waimba mashairi na tenzi zenye mwendo wa taarab kabambe!

Yaani, ukichukua Ilani ya Uchaguzi ya chama chao kuanzia tu na mwaka 1995 hadi sasa kuna ahadi zimetolewa humo kuhusu suala la nishati na tatizo la umeme nchini hadi unajiuliza hivi huwa wanakumbuka walichoahidi miaka mitano kabla yake? Au inawezekana kila unapokaribia uchaguzi mwingine wanaanza kuangalia na kusema "duh mbona tatizo bado lipo, hebu tuahidi tena"! Halafu wanakaa na kuja na ilani nyingine halafu tunarudia tena.

Sasa tatizo sijui ni wanasiasa au ni watendaji. Hili ndilo linanileta kwenye swali la leo. Hivi kuna uwezekano hawa ndugu zetu waliingia shuleni lakini shule haikuwaingia? Hivi watu wote waliosomea shahada za sayansi na saa katika umeme, utawala, uongozi na menejimenti; wote waliosomea mambo ya fedha n.k Hivi ni kweli kabisa hawa watu wameshindwa kabisa kutatua hili tatizo la umeme? Yaani, tunachoshuhudia hadi leo hii ni upeo wa uwezo wao!

Huwa nasema "upeo wetu, ndio ukomo wetu". Yaani, ukijumlisha elimu ya watu wote kwenye serikali - wizara, idara, na wakala mbalimbali; yaani ukijumlisha uwezo wao wote jumla yake ni "tatizo la umeme". Yaani, kwa miaka yote hii walipoenda shule, kozi, na mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi ukijumlisha vyote hivyo jumla yake ni hii: Tatizo lisiloisha la umeme. Yaani, kukatika katika kwa umeme, mgao wa mara kwa mara n.k yote haya ni jumla ya elimu ya viongozi na watendaji ndani ya serikali hadi mitaani kabisa.

Ndio maana leo najiuliza; hivi hawa wenzetu wanaosimamia sekta hii ya umeme kwa miaka yote hii walipoenda shule ambapo walisifiwa kuwa hawakupata makarai au mayai; kwamba wanasiwa kuwa wao ndio walikuwa "vipanga"; yaani maprofesa waliowafundisha na wanafunzi waliosifiwa kuwa walipata "Upper Class" kwenye shahada zao za uzamaji, uvumaji, uvumbivu na uvunjifu yaani hawa ndugu walichosomea kilikuwa kitu gani?

Yaani, mnataka kabisa tuamini kuwa kama taifa na tunapoelekea miaka 60 ya Muungano uwezo wa wasomi wetu wabobezi ndio huu kwenye sekta ya umeme? Yaani, haya ndiyo matunda ya kujivunjia ya muungano? Au kuna kitu kingine walikisomea wenzetu hawa?
Sasa hv wameshaanza kuwaandalia ftari wapiga kura na mijitu ilivyo mijinga itapiga kura kwa sababu ya ftari
 
Back
Top Bottom