Pia kuna hii nadharia:
*kidole Gumba = kinawakilisha wazazi wako
*Kidole kinachofuata baada ya gumba = Kinawakilisha ndugu wa tumbo moja
*Kidole cha katikati = kinakuwakilisha wewe mwenyewe (binafsi)
*Kidole cha nne = kinawakilisha mwenzi wa maisha
*Kidole kidogo cha mwisho = kinawakilisha watoto wako
Sasa jaribu kufanya hili zoezi dogo ili tuhakiki hiyo nadharia:
Kutanisha vidole vya mikono yako kama ambavyo inaonekana katika hiyo picha hapo juu.
1. Jaribu kuachanisha ncha za vidole gumba (wazazi), utagundua vinaachana - Maana yake hutaishi na wazazi wako milele
2. Jaribu zoezi hilo kwa vidole vinavyofuata (ndugu), utagundua vinaachana - Maana yake hutaishi na nduguzo milele, kaka na dada zako watakuwa na maisha yao binafsi.
3. Jaribu kuachanisha kwa vidole vidogo vya mwisho (watoto), utagundua vinaachana - Maana yake hutaishi na wanao milele maana nao watakua na kuolewa au kuoa.
4. Mwisho, jaribu kuachanisha vidole vya PETE (mwenza), hahahah hutaweza ndugu maana hivyo vilishaandaliwa kuwa pamoja daima milele, maana yake mke na mume wataishi milele na hakuna cha kuwatenganisha.
Na hii ndio sababu tunavaa pete kwenye kidole cha NNE.
"Don't hesitate to hit the like button for this clue"