Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Swali hili linahitaji jibu; jibu lake linaweza kuwa rahisi au gumu. Lakini ni jibu linalotegemea ujuzi wa historia. Ni jibu linalojaribu kuangalia kama uamuzi wa serikali ya Tanzania kutekeleza sheria kwa upendeleo (selective justice) ni uamuzi sahihi au ni miongoni mwa maamuzi mabovu kabisa yaliyowahi kuchukuliwa na watawala wetu. Na pia ni swali ambalo linauliza kama kutoa adhabu ya jumla (collective punishment) kwa kosa la Kagame ni jambo sahihi. Lakini pia ni lazima tujiulize baada ya muda uliotolewa kwa wahamiaji wageni kuondoka nchini wale waliobakia wakianza kutendewa vibaya na wenyeji serikali itawachukulia hatua hawa wenyeji au itawaachia kwa sababu wale ni wageni wahamiaji?

Quran na Biblia vinafundisha (na vinakubaliana kwa kiasi kikubwa) jinsi ya kuwatendea wageni wahamiaji katika nchi; na haihusishi kuwafukuza kwa nguvu! Katika Biblia kuna uhamiaji wa aina nyingi ambao wote una mafunzo kwa waamini; kuna uhamiaji wa Ibrahim (Abram) toka Uru wa Wakaldoyo kwenda nchi ya ahadi; kuna uhamiaji wa Yusuph kwenda Misra (baada ya kuuzwa na nduguze) na uhamiaji wa kundi kubwa la Waisraeli Misri; kuna uhamiaji (katika Agano Jipya) wa Yesu Masihi kwenda Misri pia baada ya kutafutwa na Herodi auawe akiwa kichanga.

Katika Uislamu bila ya shaka somo kubwa kabisa la uhamaji (hijra) ni ule wa Mtume Mohammed kutoka Mecca kwenda Madina. Ni uhamiaji mkubwa na muhimu sana katika Uislamu kiasi kwamba mwaka wa kwanza katika Kalenda ya Uislamu unaanzia katika tukio hilo (Al Hijra) la mwaka 622 (AD). Ujio wa Mohammed Medina ulitenganisha matendo aliyotendewa na njama alizotendewa na watu wa Mecca hadi kumlazimisha yeye na waamini wa mwanzo kuondoka hapo kwenda Medina katika hali ya kificho na hatari tupu!

Dini zetu kubwa hizi mbili (hata ya Kiyahudi) zinatufundisha kuwatendea wageni vizuri; haijalishi kama walihamia kihalali au la. Tuweke utaratibu mzuri wa kuwashughulikia na kuwahalalisha au hata kuwarudisha makwao katika heshima inayotokana na utu wao. Tukumbuke kuwa Katiba yetu inasema (Ibara 12 hadi 13) kuwa:

12.-(1) Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa.
(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na
kuthaminiwa utu wake.

13.-(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki,
bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya
sheria.

(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka
yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo
ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake.
(3) Haki za raia, wajibu na maslahi ya kila mtu na jumuiya ya
watu yatalindwa na kuamuliwa na Mahakama na vyombo
vinginevyo vya Mamlaka ya Nchi vilivyowekwa na sheria au kwa
mujibu wa sheria.

Utaona kuwa Ibara hizo hazisemi "kila Mtanzania" au "Kila raia wa Tanzania" na wala hazisemi "Kila aishiye TAnzania"! Zinasema kuwa "Kila mtu" anazaliwa akiwa huru na ni wote ni sawa! Yaani, Mhaya wa Kagera na Mkurya wa Tarime wote ni sawa! Kwamba inasema "Kila mtu anastahili heshima na haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake"; yaani Mndengereko na Mzaramo wana haki sawa kabisa ya kuthaminiwa utu wao kama ilivyo kwa Mnyarwanda na Mhabeshi! Yaani, hata kama wamevunja sheria ya uhamiaji - na inawezekana wengi wamefanya hivyo - hilo peke yake haliwafanyi wawe binadamu nusu au siyo watu kama wengine na hivyo hawalindwi na Katiba yetu! Katiba yetu inamlinda kila mtu aliyeko Tanzania!

Ndio maana hili swali linaendelea kusimama, Nyerere alishughulikiaje wahamiaji haramu kutoka Uganda wakati wa chokochoko? Kuna mtu anakumbuka au tuwasaidie hawa wa kizazi kipya somo la historia kidogo maana inaonekana watu wasiojua historia wanaenda kurudia makosa yake!

Tunaweza vipi kukubali serikali ichukue hatua za sheria kwa mfumo wa kibaguzi na udhalilishaji wa utu wa binadamu na bado tunajiita Watanzania?

Mungu atusaidia tusifurahie vitendo kama hivi kwa jina la 'uzalendo'!


MMM
 
Mkuu pengine wewe ulikuwa bado kinda mwaka 1972 hadi 1978 ilipoanza vita rasmi na Idi Amin.
Nyerere alifanya kosa la kimsingi kutochukua hatua ya ku- contain the fith column.
Hata hivyo by mwaka 1978/79 somo lilikuwa limeshaeleweka baada ya Amin kuingia Kagera kama nyumbani kwake.
Mwalimu aliwakusanya kina Oyite Ojok na hata kina Museveni, waganda, wakapigane kwa ajili y ao wenyewe na kwa ajili ya Tanzania.

JK kafanya kweli, ni lazima adui ajulikane toka mwanzo kwa vile ameshajitanabahisha toka mapema, pa kupiga paeleweke mapema.
Kama mtu anafikiri kutukanwa na kutishiwa maisha kwa mkuu wa nchi na bado mtu ukachekelea kama huna akili nxuri, basi hata a
yekutukana atajua kuwa wewe ni zuzu.
 
Umeshindwa kuelezea suala hili chronologically? ... au unataka kuupindisha ukweli na kuhusisha ugomvi wa Kagame na JK kama ndiyo chanzo.

Malalamiko yalianza muda mrefu kutoka kwa wenyeji. Kumyanyasa na kumwibia mali binadamu yeyote ni kosa, tunajua hilo.
 
Ningemlaumu Rais Kikwete angewashupalia wahamiaji haramu wa Rwanda kwa kuwa tu ametukanwa kwani ningemwona hana uvumilivu.Tatizo ni pale wahamiaji haramu wanapofanya matukio ya kihalifu na kutumia nguvu dhidi ya wazawa kufaidi rasilimali haswa ardhi.Kama dalili ya mvua ni mawingu nadhani ni hatua sahihi japokuwa yaweza kuwa kwa njia isiyo na taswira nzuri.
 
Maamuzi ya hekima na busara pekee hutoa majibu sahihi kwa matatizo mabalimbali.

Maamuzi ya kidikiteta, lazima na visasi hasa huishia katika utata, majanga na hata vita visivo na sababu wala lazima

Sikuwahi kusikia nyerere kawafukuza waganda kagera hata siku moja, nakama ilifanyika mwenyetaarifa sahihi aziweke hapa.

Hata pale Nyerere alipofanikiwa kuwatiamikononi wanajeshi na dege lao kutoka Libya, Nyerere aliwarejesha kwao kwa utaratibu maalum (kumbuka mateka wa kivita na waliletwa kwa lengo moja tu wale waarabu kutumaliza)

Nasikitika sana sana kwetu watanzania kushupalia kitendo hiki kiovu, kibaya na kinacholihalibia sifa nzuri taifa letu.

Hili ni tatizo:-

-kikwete anapoelekeza nguvu zake kwa kundi maalumu la watu maalu pekee.

-Kikwete anapochukuwa hatua bila maandalizi wala ushikishwaji bora wa wahusika

-Kikwete bila kuzingatia kwamba huko kwa majirani zetu, pia wapo watanzania wengi wanaioshi bila vibali kama hawa.

Nadhani Kiongozi wanchi yampasa kuruhusu hekima zaid kuchukuwa nafasi yake zaidi ya chochote.
 
Ni tafakuri pana...wahamiaji haramu,na majina yote mabaya kwa namna anayeita anaweza kutaja..na tukienda mbali zaidi ni mama zetu haramu,wajomba haramu,mashemeji haramu na baba haramu...yes..kuna entermarriage,once uharamu ueanzia kwenye kuingia ina maana kila kilichofuata ni haramu as well!..Kwanini uharamu huu umekuja wakati huu? Ni hasira ya kukashifiwa? Ni ushauri mbaya kwa bwana bosi?

Historia ya 1978 inaniacha nyuma so far nilikua peponi still ila nadhani Mwalimu alitumia busara kubwa sana kuklinganisha na Dr boss though hakuwa na reference! Adui wa Nyerere na taifa alikua ni Nduli Amin na watu wachache waliojiingiza kwa kulinda maslahi yao kwa Amin ila si Waganda wote! Nidhanivyo kwa wakati huo kuna wenzetu Kyaka na maeneo mengine ya Kagera walikua wameoana na Waganda,sina hakika kama ndoa zile zilivunjwa! Sina hakika...
 
Give a dog a bad name and then kill it. In the first place serikali zinakuwa wapi hadi panakuwa na wahamiaji haramu? Naweza kuelewa ukizungumzia wakimbizi. Why would one enter a foreign country illegally awe ni Mtanzania au Mnyarwanda? This is wrong. Kwanini watendaji wa serikali maeneo ya mpakani wanakubali rushwa na kuruhusu watu kuingia bila utaratibu. Bila kujali Nyerere aliwashughulikiaje these must go. Kama wanataka kurudi waje kwa utaratibu unaoeleweka. Huu ujinga ndiyo unafanya nchi inabaki uchi kwani wamejipenyeza hadi kwenye majeshi. Wasakwe hata kama tumechelewa warudishwe kwao. Nyerere hakuwa Mungu. Yeye naye kama binadamu alifanya makosa.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Najiuliza kunani nyuma ya pazia?
Juzi juzi tu tulikuwa na tension juu ya mpaka wetu na malawi lakini sikusikia 'wanaharamu' wa kusini warudishwe makwao ndani ya siku 14.
Naendelea kujiuliza ni upi ugomvi unaotishia usalama wa Taifa hili?ni ule wa mpaka au ule wa wakuu wawili walioamua kujibizana nje ya oval-table?

Au agizo limetwanga kotekote yaani wanaharamu wa kinyarwanda na kinyasa wachape lapa?
 
Kuwafukuza wageni has never been utamaduni wa Mtanzania, we are too smart to be barbaric. Serikali ijirekebishe.
 
Tatizo la Mwanakijiji ni kutokuijua Tanzania vizuri.

Yaani macho yake yameishia kuona kwamba wahamiaji haramu ni swala linalohusu chokochoko za kagame. Hujui kabisa kuwa Tanzania kuna sehemu huwezi kusafiri bila escort ya polisi kwa sababu ya wahamiaji haramu.

Hivi hao waganda unaowazungumzia walikuwa wanazuia watanzania kufanya movements zao nchini kwao?

Kumchukia kwako Kikwete kunakufanya kila analosema au kulifanya utafute jinsi ya kulipinga!

By the way, unapomlinganisha Nyerere na Kikwete unataka kujustify nini???

Chuki itakupeleka kubaya Mwanakijiji.
 
Hivi mkuu wewe ni Mzee Mwanakijiji wa siku zote ambaye alikua anachambua mada vizuri na kwa busara kubwa au mtu anatumia jina lako?. Siku za karibuni umebadiluka sana! Kwenye hizo quote zako zote za bible,quran na katiba ya Tanzania kumeainishwa na kumefundisha watu wafuate taratibu na sheria zilizowekwa na mamlaka husika. Mbona hauja quote vipengele hivyo? Ulipenda watu waishi nchi si yao wakiwa si raia na wanyamaziwe?.Ulipenda watanzania walalamike kuhusu uhalifu wanaofanyiwa kila siku kwenye nchi yao. Ulipenda hali ya kusindikizwa na mapolisi kila watu wanapotaka kusafiri toka wilaya moja kwenda wilaya nyingine ndani ya nchi yao?. By the way wanaoondolewa kule si wanyarwanda peke yao ni raia wote wa kigeni ambao wanaishi isivyo halali.Mifano na quotes na refferences ulizotoa hazihusiani kabisa na linaloendelea kule. Pia hakuna nchi yeyote inayoruhusu mhamiaji kuishi akiwa hana passport,working permit au documents za kuhalalisha ukaaji wake. Kuhusu kuoana wala hakukatazwi ila asiye raia aombe uraia ili aishi ki halali.Ndio maana nikasema wewe ni yuleyule au tutegemee mwingine!?
 
umeandika kishabiki sana hata ukweli umekushinda kuweka bayana nadhani kunakitu unakitafuta au unachezea akili za watu.

Huyu jamaa tangu mgomo wake wa simu ulivyofeli amekuwa akiweweseka kujaribu kupata njia nyingine ya kuchochea chuki baina ya watanzania.

Kikwete na Nyerere wote ni wana CCM. Hawana tofauti kiitikadi. Sasa huyu Mwanakijiji anapotaka kuwalinganisha sijui lengo lake kujustify nini!!!
 
Tatizo la Mwanakijiji ni kutokuijua Tanzania vizuri.

Yaani macho yake yameishia kuona kwamba wahamiaji haramu ni swala linalohusu chokochoko za kagame. Hujui kabisa kuwa Tanzania kuna sehemu huwezi kusafiri bila escort ya polisi kwa sababu ya wahamiaji haramu.

Hivi hao waganda unaowazungumzia walikuwa wanazuia watanzania kufanya movements zao nchini kwao?

Kumchukia kwako Kikwete kunakufanya kila analosema au kulifanya utafute jinsi ya kulipinga!

By the way, unapomlinganisha Nyerere na Kikwete unataka kujustify nini???

Chuki itakupeleka kubaya Mwanakijiji.
Mwanakijiji yeye Tanzania anayoijua ni dar tu Huko kwingine hakujui. Pia hata taarifa za habari hasikilizi.
 
Hivi mkuu wewe ni Mzee Mwanakijiji wa siku zote ambaye alikua anachambua mada vizuri na kwa busara kubwa au mtu anatumia jina lako?. Siku za karibuni umebadiluka sana! Kwenye hizo quote zako zote za bible,quran na katiba ya Tanzania kumeainishwa na kumefundisha watu wafuate taratibu na sheria zilizowekwa na mamlaka husika. Mbona hauja quote vipengele hivyo? Ulipenda watu waishi nchi si yao wakiwa si raia na wanyamaziwe?.Ulipenda watanzania walalamike kuhusu uhalifu wanaofanyiwa kila siku kwenye nchi yao. Ulipenda hali ya kusindikizwa na mapolisi kila watu wanapotaka kusafiri toka wilaya moja kwenda wilaya nyingine ndani ya nchi yao?. By the way wanaoondolewa kule si wanyarwanda peke yao ni raia wote wa kigeni ambao wanaishi isivyo halali.Mifano na quotes na refferences ulizotoa hazihusiani kabisa na linaloendelea kule. Pia hakuna nchi yeyote inayoruhusu mhamiaji kuishi akiwa hana passport,working permit au documents za kuhalalisha ukaaji wake. Kuhusu kuoana wala hakukatazwi ila asiye raia aombe uraia ili aishi ki halali.Ndio maana nikasema wewe ni yuleyule au tutegemee mwingine!?

Mwanakijii anaendeshwa na chuki aliyo nayo juu ya Rais wetu.

Hakuna kingine.

Hata Kikwete angesema "tuwavumilia wahamiaji toka nchi jirani mpaka serikali zao zitakapokuwa tayari kuwahcukua" pia angeandika article ya kupinga.

Watu kama hawa kwenye jamii hawakosekani, ila tatizo ni kwamba kwa Tanzania ya sasa watu kama hawa ni hatari sana.

Kwa mfano anapomlinganisha Nyerere na Kikwete lengo lake ni kujustify nini? Hivi tukifikia conclusion kwamba Nyerere alifanya maamuzi bora zaidi ya Kikwete, then what?

Chuki inampeleka kubaya sana Mwanakijiji.
 
Tatizo la Mwanakijiji ni kutokuijua Tanzania vizuri.

Yaani macho yake yameishia kuona kwamba wahamiaji haramu ni swala linalohusu chokochoko za kagame. Hujui kabisa kuwa Tanzania kuna sehemu huwezi kusafiri bila escort ya polisi kwa sababu ya wahamiaji haramu.
.
kwa hiyo serikali ndio imekumbuka kwamba wahamiaji haramu wanatakiwa kuhama baada ya kitisho cha kagame-(I will hit you).
Walishambuliwa wanajeshi wetu na boti zao kuzamishwa hapo mwambao wa ziwa Tanganyika lakini sikusikia kauli ya 'Bwana kubwa'
Naweza sema thanks to Kagame kwa kukumbushia majukumu ya serikali yetu.
 
Mwanakijiji yeye Tanzania anayoijua ni dar tu Huko kwingine hakujui. Pia hata taarifa za habari hasikilizi.

Hata Dar haijui vizuri. Angekuwa anaijua Dizim asengethubutu kujihusisha na mgomo wa kuwaambia watu wazime simu zao.

Huyu jamaa amejaa chuki tu. Anachokifanya ni kuipandikiza chuki hiyo kwa watu wengine, kwa sababu anajua hata moto ukiwaka yeye hayupo.
 
Ange wafukuza vipi wakati aliwatumia kwenye Vita? Ndii kwanza aliwakaribisha waje wajiunge na Museven pia Kagame akiwemo alikuja kujiunga kwenye vita zidi ya IDD Amin.

Narudia tena naogopa kusema , Tena Naogopa kusema wewe ni Mtetezi wa pili nakuona humu baada ya ile inayodaiwa Kauli ya Dr. Slaa.

Jamani sitaki kuamini kama mmekuwa watetezi wa Kagame/WaTUSI mara hii kwa sababu ya ......

Naogopa kusema Hadharani.
 
Back
Top Bottom