Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

JokaKuu; hawa wakimbizi ambao walipewa uraia na Kikwete kwa wingi hivyo walikuwa wapi katika Tanzania? (hili ni swali la mtego kuweka rekodi sawasawa)
Mzee Mwanakijiji,

..hao wakimbizi nadhani walikuwa Tabora, Rukwa, na Kigoma.

..walikuwepo muda mrefu toka mwaka 1972.

..kuna wengine walizaliwa hapa Tanzania.

..zoezi la namna hii limewahi kufanyika mwaka 2000, 2003, na 2006.

..kuna mpaka kamati za Tanzania na Rwanda kushughulikia tatizo hili la wahamiaji haramu toka Rwanda.

..swali la ziada: is it Rwandas government policy ku-encourage wananchi wake kuwa wahamiaji haramu, particularly to Tanzania??

cc Nguruvi3, Jasusi, Kobello, Ogah, rushasha, adolay, meningitis
 
Last edited by a moderator:

The result of stupid utterences from a loose mouthed president, Kagame.
We Tanzanians dont talk much but he should be careful next time when he opens his gob.
We have bee harbouring your problems silently for years on end.
 
Waende kwao, hao ni waamiaji haramu. Hizi huruma zenu za kijinga za kuongozwa na hisia, zitatuponza na zimetuponza. Uraia sio kitu cha kutoa kama Ice cream. Kama kuwapa huo uraia mmewapa wengi sana hao sasa inatosha.
TUSIRUDIE KUTOA URAIA KWA WATU HOHEHAHE KAMA HAO, KWANI NI MZIGO KWA TAIFA LETU.
 
Wanatucheka sana na kujisifu mno eti wameendelea kuliko sisi na ubabe juu. Alafu kuna mijitu inajifanya inahuruma ya kugawa uraia. Hao ni watu wa Skeleton Kagame ahangaike nao yeye mwenyewe Au awape wakenya aliowapa dili la kutumia badari yao.
HAKUNA NCHI DUNIANI UNAWEZA KUINGIA BILA KUULIZWA, HUKU UNASWAGA NG'OMBE ISIPOKUWA TANZANIA.
Hakuna nchi katika Africa iliogawa uraia kwa wakimbizi wengi kama TANZANIA.
FAIDA TUNAYO IPATA LEO NI KUTUKANIWA RAIS WETU.
 
Hivi mkuu una uhakika gani sisi watanzania tunaoishi nje wote ni watu safi?[sio majambazi,wauza unga,].ungenipa data za crime huko rwanda labda ningekubali.Pia ujue kuna watanzania wa kuzaliwa ambao wamerudi Rwanda.Na unajua sheria yetu hapa mtu akizaliwa hapa nchini ni raia wa hapa Tanzania,sasa husije ukafikiri idadi ya watanzania waliokuwa huko ni kiasi fulani.Kwa jinsi ninavyokuangalia na kukusoma wewe unaangalia waamiaji kwenye mipaka tu wala ujajua wapo wengine kwenye mikoa yetu yote.Kwani hao wachina ,wairan na wengine wanao fanya biashara Tanzania wote wana vibali vya kufanyia kazi?na wanalipia kila mwezi vibali vyao?.Watanzania sisi mara zote tunafake kuwa sisi ni watu wazuri.naweza kusema ilikuwa zamani.Ujambazi upo na sio rahisi kujua nani ni jambazi kati yetu.Kwa nini hili zoezi la kuwaamisha watu lisifanyike siku za nyuma?naomba unijibu.Na kwa nini amesema taasisi zote za dola zitakwenda huko Bukoba na kusafisha hao waamiaji.Sikusikia kama amesema kuwa hivyo vyombo vya dola vitajipaka nchi nzima kuakikisha waamiaji wanatolewa.Yeye kasema atapeleka hivyo vyombo vya dola huko Kagera.Mimi sijafurahia maneno aliyoyatoa Kagame.Mimi nasikitika mtu aliyekuwa msuluhishi katika maziwa makuu ,sasa ameonekana kumbe sio smart.anakurupuka na alikwenda Bukoba kuongea na wananchi huko.Ningemwona smart kama ningesikia Rais Kikwete na viongozi wengine wamekutana close door sehemu fulani hata kama walichoongea nisingekifahamu ningejua kiongozi wetu ni smart.Kwa kufanya hivyo sio kwamba tunamwogopa Kagame hapana.Ni kwamba sisi hatukurupuki.Hakuna mtu hasiejua kama Tanzania ina uzoefu wa kupigana vita.Ninachosema yule Rwanda ni kama mdogo wetu.Lakini kwa kurushiana maneno bila ya kukutaka kaka na mdogo wake nani ameonekana anachekesha.Ni kaka au mdogo wake?.Watanzania hatutaki vita .tuna vita nyingi ndani ya hii nchi hatujamaliza.[tatizo la madarasa,watoto kutokuwa na madaftari,kilimo,maji safi,afya.]na mengine mengi kama rumbesa hivi hatujamaliza.Tumegundua gesi na madini mengine acha pesa zake zielekezwe kwenye vita muhimu za ndani ya nchi.kule kwa kagame tutakaa mezani tu ,sio issue kubwa kabisaa.MUNGU TUEPUSHE NA VITA NA UTUPE HEKIMA NA BUSARA YA KUAMUA AU KUTATUA MIGOGORO KWENYE MEZA NA SIO KUINGIZA NCHI VITANI.AMEN
 

While at it ningependa kuuliza swali jingine: Ni Wanyarwanda wangapi na Warundi waliopewa uraia wakati wa Mwalimu Nyerere? Naona jinsi watu wanavyosifia hapa kutimuliwa kwa Wanyarwanda I am really ashamed to be a Tanzanian.
 

umesema vema mwanamazingira
 
Mkuu kuna watu akili zimewazidi.
Lakini akili hizo haziwafikishi mwisho wa safari zao.

Hawaelewi kuwa for a long time Kagame had it coming, alijidai kucheza hard ball katika hii interlacustrine region ambayo na sisi Tanzania ni sphere yetu ya influence.
Kwamba Tanzania haija itumia hiyo clout yake sehemu hizo, kuna viongozi wajinga waliichukulia kuwa ni sign of weakness, kiasi cha kudiriki kumtukana kiongozi wetu JK

Mbaya zaidi ni kiongozi huyo ambaye siri zake za mauaji zinafahamika vile vilr kifiriki kusems atsmdhuru kiongozi wetu kimwili.

Naona ni mtu mjinga tu asiyeweza kuona kuwa Kagame alikuea anacheza mchexo unao hitaji majibu anayoweza kuelewa kinagaubaga.
Pamoja na vitisho vya wakimbizi ambao huko DRC wamejigeuza kuwa M23, somo hili nashangaa watu wanapungukiwa na akili ya kulielewa.

Namsapoti Jk 100% kwa kulichukulia tatizo la Kagame bila papara na kwa uvumilivu.
 
Last edited by a moderator:
While at it ningependa kuuliza swali jingine: Ni Wanyarwanda wangapi na Warundi waliopewa uraia wakati wa Mwalimu Nyerere? Naona jinsi watu wanavyosifia hapa kutimuliwa kwa Wanyarwanda I am really ashamed to be a Tanzanian.
Mkuu Jasusi kwanza nikuulize, kwani ubaya wa zoezi hili ni upi? Yaani tatizo lake ni nini hadi ujisikie ashamed
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Jasusi kwanza nikuulize, kwani ubaya wa zoezi hili ni upi? Yaani tatizo lake ni nini hadi ujisikie ashamed
Ndugu yangu, I feel ashamed kuona Waafrika wenzetu, majirani, wakibeba virago vyao kurudi kwao wakati Wasomali, Wahindi, Wapakistani wazungu na Wachina wakila sahani moja na viongozi wa CCM na hawa tunawaona eti ni watu wanaotuletea neema. Nenda Rufiji leo uone ni Wasomali wangapi wamenunua ardhi kule. Mwalimu angekuwa hai hivi leo naye angeona aibu eti tunawatimua Wanyarwanda just because Kikwete ana beef na Kagame. It is a shame. Kweli Tanzania ya Julius Nyerere imefika hapo?
 
Wakimbizi walikuwepo hata kabla ya kupishana kwa kauli za viongozi wetu (suala la kutekwa magari nimelisikia tangu miaka ya 85's nilipokuwa nasafiri kwenda pande za biharamulo) na tuwe wawazi hapa hatetewi mtu na hakuna mtu aliye kamili chini ya jua (labda uwe muumini wa kauli ya kuwa kiongozi hakosei ila anaangushwa na wasaidizi wake), unaweza ukatoa ushauri kwa nia njema lakini ukajikuta umecross the line kwa yule unaye mpa ushauri (kwa mtazamo wake). Jk anahaki ya kuhami mipaka ya taifa letu lakini wakimbizi hawa hawajafika hivihivi tu bila ya msaada wa watendaji walio kwenye serikali anayoiongoza, je amewachukulia hatua gani maana ushahidi uko wazi na si kuonyeshana kuwa nimeshika mpini nawe umeshika makali.
 
Kuwafukuza wageni has never been utamaduni wa Mtanzania, we are too smart to be barbaric. Serikali ijirekebishe.

Kuwafukuza wahamiaji haramu ni historia ya Tz tangia baada ya uhuru. Ukiacha collective nationalization ya Nyerere kwa wanyarwanda wengine wote wamekuwa wakiishi kwa taabu Tz. Kabla ya kuundwa kwa makambi ya Tabora na Katavi, kulikuwa na killings na kurudishwa hata katika nchi za vita na serikali ya Nyerere. Kisha serikali ya Mwinyi imerudisha wote warundi, wanyarwanda na wakongomani toka mikoa hii hii tunayoisema ukiacha Geita ambayo haukuwa mkoa lakini baadhi kutoka maeneo ya Chato waliathirika (Lyatonga ni shahidi hata miaka ya 1987 anajua alipewa nini Bujumbura na akarudi akaswaga hata waha kwa kusema lazima warudi kwao) walipofika mipakani wakakuta wengine si tu waha bali ni wachaga wanaoonekana kama watu fulani wa Burundi na hivyo wakarudi Kgm na kukimbilia Himo kwao. Miaka ya 90 walisindikizwa kwa helkopta kuhakikisha hawaendi sehemu nyingine ila Rwanda (na hawa walikuwa ni sehemu ya hao Kagame anaosema ni Interahamwe waliokuwa wamefika maeneo ya Benako kusalimisha maisha baada ya mauaji ya kimbari (nasita kusema nani alifanya mauaji ya kimbari kwa kuwa historia siku zote inashughulika na mshindi) lakini tunajua historia inashughulika na mshindi na si vinginevyo. Miaka hiyo hiyo ya 90 wakati wa Mkapa wakongomani wa mwambaoni mwa ziwa Tanganyika nao walikumbwa na dhahama hiyo hiyo. Labda suali lisiwe kuwa kuna waliolengwa katika tamko la JK maana alisema wahamiaji haramu wote wala hajasema wanyarwanda, ila walioamua kutekeleza agizo la raisi ni wanyarwanda. Sasa mwisho
 
1959 wakati wimbi la kwanza linaanza kuingia Tanganyika wewe ulikuwaq na umri gani?
 
Una maana ujangiri unaotendeka nchini unatendwa na wahamiaji haramu? You could do better.
 
I have read som ---- but yours takes prise.
 

Una ushahidi gani kuwa waliokuteka (kama kweli ulitekwa) walikuwa ni wahamiaji haramu? Ulimboka alitekwa na wahamiaji haramu? Mabasi ya kutoka mikoani hayaruhusiwi kuondoka morogoro kuelekea Dar baada ya saa sita usiku - je nayo yanazuiwa kwa sababu ya majangiri wahamiaji haramu?
 
Jasusi,

..hili zoezi liliwahi kuendeshwa mwaka 2000, 2003, na 2006.

..kuna mpaka research papers zimeandikwa kuhusu tatizo la wahamiaji haramu wa Rwanda nchini kwetu.

..kwanini watu hawa wanaendelea kurudi huku Tanzania? ina maana hawana taarifa kwamba haturuhusu wahamiaji haramu? je, serikali ya Rwanda ina-encourage raia wake wasiheshimu mipaka na sheria za uhamiaji za Tanzania??

cc murutongore, enviromental, Mzee Mwanakijiji, Ogah, adolay,
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Jasusi kwa muda nafatilia mkasa na sitofahamu inayoendelea kwamba Shekhe ponda kapigwa risasi.

Nitarejea baada ya muda, kwasasa nipo kwenye uzi kumhusu ponda.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…