Swali..!

Swali..!

mzizimkava waboa, kutuletea hoja kavu
ni kama umekula mihogo,mikavu pale magomeni
uje ujibu kwa hoja, na si kwa longo longo
kama hujui mashairi,wapishe wanaojua

Eh! Kumbe ushairi rahisi hivi, nilikuwa sijui
 
Kama kutunga rahisi, Wangeweza wengi sana
Kama kweli mhandisi, Ungepanga vyote vina
Mbele ya kadamnasi, Watia aibu mwana

Kujuwa kwingi kusema, Vina vyako havifani
 
Kama kutunga rahisi, Wangeweza wengi sana
Kama kweli mhandisi, Ungepanga vyote vina
Mbele ya kadamnasi, Watia aibu mwana

Kujuwa kwingi kusema, Vina vyako havifani
sawa ndugu X-Paster, hongera kutukumbusha,
wengine siyo mamaster, wa vina kuvifungasha,
na wataelewa faster, vina ukiwafundisha,
rudi kwenye yetu hoja, na mfungo wa ramadhani.
 
Mmmmh!
Anyisile sikuwezi, wajua kung'ang'ania
nilishakupa uwazi, mbona walialia
nikakutungia tenzi, bado hijakuingia
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Krismasi na pasaka, wewe uzikumbukapo
ukatoa na sadaka, wao ni kama hawapo
hawahoji zako zaka, ulapo nyama za kopo
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Masuala ya imani, waachie wenye nayo
kama kuhubiri dini, si njia uiendayo
piplipili ya shambani, ikiwasha mimi sipo
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Hata nimechoka sasa, siioni yako nia
naomba kuaga sasa, mwenzako naenda oa
utabishana kwa sasa, jibu litasaidia
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!
 
Mmmmh!
Anyisile sikuwezi, wajua kung'ang'ania
nilishakupa uwazi, mbona walialia
nikakutungia tenzi, bado hijakuingia
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Krismasi na pasaka, wewe uzikumbukapo
ukatoa na sadaka, wao ni kama hawapo
hawahoji zako zaka, ulapo nyama za kopo
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Masuala ya imani, waachie wenye nayo
kama kuhubiri dini, si njia uiendayo
piplipili ya shambani, ikiwasha mimi sipo
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

Hata nimechoka sasa, siioni yako nia
naomba kuaga sasa, mwenzako naenda oa
utabishana kwa sasa, jibu litasaidia
ramadhani kwao dini, wewe yakuhusuni!

compaq nimekupata, na sitaki farakana,
majibuyo nimepata, kwa kweli nyongeza sina,
toka kwao sijapata, jama nguvu tena sina,
X-Paster mi nakuaga, mshukuru huyu compaq.
 
Haya kwaheri kijana, Kwaheri ya kuonana
Kwa usiku na mchana, Si ila kuambizana
Akipenda Rabana, takuja onana tena

Kiasi kukumbushana, Kwa amri ya Rabbana
 
Haya kwaheri kijana, Kwaheri ya kuonana
Kwa usiku na mchana, Si ila kuambizana
Akipenda Rabana, takuja onana tena

Kiasi kukumbushana, Kwa amri ya Rabbana
na elimu kupeana, wala si kutukanana,
na nakuaga kijana, siache salimiana,
ujumbe fikidhiana, tena wenye maana,
Jehova kupe busara, hekima isipunguke
 
na elimu kupeana, wala si kutukanana,
na nakuaga kijana, siache salimiana,
ujumbe fikidhiana, tena wenye maana,
Jehova kupe busara, hekima isipunguke

Watu wananufaika, kusoma mambo ya dini
wengi wanafaidika, makala zenye thamani
Ndugu wanashughulika, kutuletea yakini

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini

umuombe Subhana, Aondoshe kisirani,
Akuongoze kijana, pamoja na wana-ndani,
si usiku si mchana, dua ziwe mdomoni,

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini

Tuepuke na ghadhabu, Ghadhabu za Rahmani
tuepuke na adhabu, ya moto na kaburini
tuwawekee adabu, wazazi na majirani

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini
 
sideeq wahangaika,kutuletea porojo
kitu moja nakuomba, mwezi utakapoanza
sisahau kunambia,uniungishe magimbi
mihogo na nyanyachungu,bila sahau mbatata

takuuzia bei cheee,ili uchukue vingi
ushindilie kwa daku,usiku kucha bugia
changanya changanya vitu,kwenye ilo tumbo moja
asubuhi kuinama ili uswali vizuri

sipati picha ikoje,kwenye icho chumba chenu
cha kuswalia mtume,kwani wengi huinama
matumbo yakishajaaa, kwa daku la jana yake
utapata magensium,upunguze kuvimbiwaaaa


Kula tano
 
Haya kwaheri kijana, Kwaheri ya kuonana
Kwa usiku na mchana, Si ila kuambizana
Akipenda Rabana, takuja onana tena

Kiasi kukumbushana, Kwa amri ya Rabbana


Nakuona jinsi ulivyofurahi baada ya kuomba sana mjadala uishe, kwan mlikua mmekamatwa pabaya.
 
Ubungoubungo said:
sideeq wahangaika,kutuletea porojo
kitu moja nakuomba, mwezi utakapoanza
sisahau kunambia,uniungishe magimbi
mihogo na nyanyachungu,bila sahau mbatata

takuuzia bei cheee,ili uchukue vingi
Sikupi wangu muhogo, sikia mwanahizaya
Hupati hata kidogo ,malu`uni usiye haya
wachezewaje kichogo? ondosha wako udhiya!
Ni maajabu ya duniya jamani yatizameni

Hata naye mpigajeki, yuko kwenye disapora
Maneno haambiliki, kazidi wake ukora
Uzayoni naye shabiki, mradi tumbole kufura
Ni maajabu ya duniya jamani yatizameni

Kaja yeye kwetu mjini, kwao tabu zilizidi
Akajiita ni Salimini, kuficha zake hasadi
Ameishia kutukhini, yu ajikomba kwa yahudi
Ni maajabu ya duniya jamani yatizameni

Na Mbona Joni mwenzako, amekuwa ni Athumani
Mashakanini hayuko, humwoni vijaridani
Umebaki u peke yako,kusifiwa maglobuni
Ni maajabu ya duniya jamani yatizameni
 
Watu wananufaika, kusoma mambo ya dini
wengi wanafaidika, makala zenye thamani
Ndugu wanashughulika, kutuletea yakini

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini

umuombe Subhana, Aondoshe kisirani,
Akuongoze kijana, pamoja na wana-ndani,
si usiku si mchana, dua ziwe mdomoni,

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini

Tuepuke na ghadhabu, Ghadhabu za Rahmani
tuepuke na adhabu, ya moto na kaburini
tuwawekee adabu, wazazi na majirani

Akuepushe na mashaka, huwe na matumaini
Tena ni yeye daima, hakuna wa kulingana,
Hata bila ya hekima, hapana wa kufanana,
Hakika ni mtoa mema, hata kama twabishana,
Yeye ni mwenye upole, yatupasa kumwabudu.

Basi Mola wako mcheni, Maana ni mwenye kuumba
Akili keshakupeni, tofauti na za Komba,
Neema kakujarieni, pasipo hata kuomba,
Yeye ni mwenye upole, yatupasa kumwabudu.
 
Unampa mtu tano hata ushairi hajui!


Duuu!!!! blaza unadhani wale wachambuzi wa mpira kwenye tv na radio huwa wanaweza kucheza kama wanavyoshabikiaga au kukosoa?

Isitoshe sio lazima nijue, kwani kila mtu na fani yake.
 
Duuu!!!! blaza unadhani wale wachambuzi wa mpira kwenye tv na radio huwa wanaweza kucheza kama wanavyoshabikiaga au kukosoa?

Isitoshe sio lazima nijue, kwani kila mtu na fani yake.
Kwa hiyo wewe fani yako ushairi au sio!? lol!
 
X-Paster hodi nakuja, Jinius sichukie,
Tumaini kwako naja, Sadeeq unisikie,
Hafif andaa hoja, MziziMkavu nisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.


Hili swali ni noma, tena laumiza ubongo,
nimesachi kila kona, mbagala, Ilala, Ubungo,
Wakujibu sijaona, wakimbia na hoja fyongo

Limeulizwa swali, anyisile ataka juzwa,
Kufunga hii Ramadhani, ni nini? la mkwaza,
Ratiba i-change kwa nini?, ndo swali lilo ulizwa.

Ratiba yabadilika, mchana kwenda usiku,
Milo mitatu kadhalika, futuri, saa sita na daku,
Swali li wazi hakika, ajibiwe apate fahamu.

Mjukuu wa kimokole
 
Hili swali ni noma, tena laumiza ubongo,
nimesachi kila kona, mbagala, Ilala, Ubungo,
Wakujibu sijaona, wakimbia na hoja fyongo

Limeulizwa swali, anyisile ataka juzwa,
Kufunga hii Ramadhani, ni nini? la mkwaza,
Ratiba i-change kwa nini?, ndo swali lilo ulizwa.

Ratiba yabadilika, mchana kwenda usiku,
Milo mitatu kadhalika, futuri, saa sita na daku,
Swali li wazi hakika, ajibiwe apate fahamu.

Mjukuu wa kimokole

Nilidhani limeisha, swali hili la obheli
tukazane na maisha, mjukuu na obheli
usiku nijapokesha, kwa sababu ya kusali
mchana wote nilale, wewe lakuhusu vipi!????????????
 
Kati ya nguzo zetu, Twakumbuka Ramadhani
Sisi na vizazi vyetu, Tunahimizwa ayani
Na hata Mtume wetu, Katuhimiza jamani

Viumbe tunashindana, Pepo kuipigania

Saumu bila makuu, Sababuze taweleza
Mwili wapata nafuu, Mlitambule la kwanza
Yatuonyesha matuu, Masikini wasoweza

Hujuwi kama mwakani, Upo katika dunia,

Nao waso Isilamu, Kuijuwa wanataka
Maana hiyo saumu, Isilamu waloshika
Walipoona kaumu, Wote wameimarika

Kwa Mungu tukisharudi, Hakuna nyingine njia

Awali walielezwa, Mola katuamrisha
Ni shuruti kufuatwa, Katu hatuto kanusha
Na adhabuye n'kubwa, Wasiyo imairisha

Maiti anatamani, Arudi kuhudhuria


Wakazidi uchunguzi, Kwa wingi na tahayuri
Wakajitweka makazi, Yaso yao makafiri
Wakaona ni vizazi, Wafungao kwa hiari

Mwezi huo ni adhimu, Mungu Ametujalia

Mwezi huu mashetani, Wana pingu mikononi,
minyororo ya shingoni, Wametiwa huwaoni,
Ona vipi Rahmani, Mwezi Anauthamini

Mwezi huu tarawihi ni Swalah za Ramadhani


Mwezi huu wa kufunga, kila kitu mdomoni,
Sio mwezi wa kuringa, kujivuna mitaani,
Ni mwezi wa kujikinga, na maasi duniani,

Na ibada shughulika, Asubuhi na jioni
 
Back
Top Bottom