KERO Taa za barabarani eneo la Stendi ya Morocco hadi Biafra zitengenezwe, ni hatari kwa usalama

KERO Taa za barabarani eneo la Stendi ya Morocco hadi Biafra zitengenezwe, ni hatari kwa usalama

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Taa za barabarani eneo la Stand ya Morocco hadi Biafra zinahitaji kutengenezwa, kwani ni hatarishi kwa usalama.

Ikifika usiku, Morocco inatisha kwa giza. Taa za barabarani kuanzia Stand ya Morocco hadi karibu na Biafra, Kinondoni hazifanyi kazi upande mmoja kwa muda mrefu sasa, jambo ambalo linapelekea hatari kubwa kwa watumiaji wa barabara.
5814343373627180740.jpg

Eneo la Stand lina shughuli nyingi, ambapo magari huingia na kutoka muda wote, na ni sehemu yenye shughuli za watembea kwa miguu.

Kukosekana kwa mwanga kunaweza kusababisha ajali, wizi, na matukio mengine ya uhalifu. Ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe ili kuboresha mwanga na usalama katika eneo hili.

Mamlaka husika chukueni hatua za haraka kwa usalama zaidi
5814343373627180742.jpg


5814343373627180741.jpg

Pia, Soma:
+
Tatizo la Taa za Barabarani Stendi ya Morocco hadi Biafra lamalizika, Usalama Waimarishwa

+ Arusha; Taa za kuongoza magari zina zaidi ya mwezi mmoja hazifanyia kazi
+ Taa za Barabarani eneo la Kona ya Nairobi zitengenezwe, ni hatarishi kwa usalama
+ Changamoto ya Taa za kuongoza magari Stendi ya Nata (Mwanza) kutofanya kazi, lini zitatengenezwa?
 
Back
Top Bottom