Taa za umeme za LED huleta nafuu katika bili ila ni hatari kwa afya

Taa za umeme za LED huleta nafuu katika bili ila ni hatari kwa afya

Mimi nileshakuwa addict wa LED. Mwanga Murua kabisa. Hasa nyumba ikiwa umepaka rangi nyeupe.....Safiiii. Yaani inapendeza sana.
Mkuu kumbe tupo wengi mimi pia ni muhanga wa uraibu wa hizi taa yani sipati usingizi kabisa nisipoacha taa ikiwa on yani naweza kulala vizuri kwenye mazingira yenye mwanga (LED in particular) kuliko nikiwa gizani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Siasa inaua
2. Kujamiana kunaua
3. Dini inaua
4. Biashara inaua
5. Pesa inaua
6. Starehe zinaua
7. Pombe inaua
8. Kazi inaua
9. Chakula kinaua
10. Taa za LED zinaua
11. Vinywaji baridi kama coca, red bull nk vinaua
12. Sukari inaua
13. Dawa zinaua ( the best medicines are dangerous poisons)
nk
Kila kitu hapa Duniani kina hasara na faida.
Kwa hiyo tunapofanya jambo fanya kwa kiasi na kama ukifanya unapata madhara , acha kabisa.
Kama ukiacha unakufa haraka zaidi basi endea kufanya hadi utakapokufa.
PIa Serikal (TBS) iko kwa ajili ya kumlinda mlaji kwa vitu vinavyotengenezwa viwandani. Kwa hiyo kama hawajatoa tahadhari hatuna haja ya kuwa na wasi wasi
 
Kuna zile naona zimetengenezwa kama tubelight zina plastic kuzuia zile led zenyewe usizione moka kwa moja, je hii haisaidii kupunguza hizo athari?
 
light_tlo.gif
 
acha kudanganya watu wewee, taa za tubelight zina madhara makubwa sana ukilinganisha na LED, teknolojia yake inatumia mercury, sijui kama unajua kwenye bulb za tubelight ( zile mtaani tunaziita energy saver) hutakiwi kabisa kuigusa hiyo bulb, na unapo nunua kuna onyo/katazo la kutoshika hizo taa 'with bare hands'
 
Kwa sasa vifaa vya electronics ambavyo ni high quality wamekuwa wakifilter blue light.

Hasa hili nimeliona kwenye simu TV na computers...

Sent using Jamii Forums mobile app


Ni kweli kabisa maana nilipata shida ya macho nikajua moja kwa moja tatizo linasababishwa na matumizi yangu ya laptop, nilivyoenda hospitali (ccbrt) daktari alinipima akaniambia sababu tofauti kabisa na niliyokua nafikiria.

Ikabidi nimwambie kuhusu matumizi yangu yaliyokithiri ya laptop, akaniambia mwanga wa vifaa vingi vya kielectronic vya kisasa hauna madhara kama watu wengi tunavyodhani. Akanipa mfano wa computers ambazo zilikua na athari kidogo kwenye macho ni zile za kizamani ambazo mwanga wake ulikua unachezacheza.

Nakumbuka huyu daktari alikua myahudi sio mbongo!
 
Hizo ni salama ukilinganisha na LED
Kwani Transistor hizo energy saver si ndio hizo Led, ambazo zimeitwa Energy saver kwa kuwa power consuption yake ni ndogo sana ulilinganisha na zile taa za mwanzi au zile bulb za kizamani?
Halafu hizi Led ziko zile zina muwako wa warm light je nazo zina madhara kama hizi zenye muwako mweupe?
 
Na manga wa kibatali nasikia unaongeza nguvu za kiume
 
Heri ya mwaka mpya wakuu,

Taa za LED zimepata umaarufu miaka ya hivi karibuni kutokana na kuwa na mwanga mkubwa huku ulaji wake wa umeme ukiwa ni kidogo.

Licha ya faida hiyo kutokana na tafiti mbalimbali taa za LED,zimeonekana kuwa na madhara kiafya,licha ya wataalamu wanao unda taa hizi kuzidi kuziboresha,ili kuepukana na madhara hayo.

Mwaka 2016,shirika la kimarekani la American Medical Association(AMA),lilisema tekinolojia ya taa za LED,yana athari kwa afya ya binadamu.

Taa za LED zinazalisha mwanga wake kwa kutumia mawimbi mafupi,mawimbi haya yana kiasi cha nguvu ya juu cha miale ya blue na violet yaliyo katika kiwango cha kuonwa na jicho la binadamu.

Endapo macho ya binadamu yatazama mwanga huu huweza kuathirika kwa kiasi fulani katika uwezo wake wa kulala,mara kadhaa baadhi ya watu wamekuwa wakikumbwa na tatizo la kuwashwa macho ama kichwa kuuma baada ya kuwa katika mwanga wa taa za LED kwa muda mrefu.

Endapo mtu atakua katika mazingira haya ya mwanga wa taa za LED,basi miale ya blue inayozalishwa na mwanga wa taa hizi huweza kusababisha ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataract) ,au tatizo la uoni hafifu (Macular degeneration).

Pia tafiti zinaonesha kuwa miale inayozalishwa na mwanga wa taa za LED,husababisha mabadiliko ya "retinal" katika jicho hata kwa matumizi ya muda mfupi tu ya taa hizi.

Tafiti ya mwaka 2014 ya shirika la afya ya mazingira inaonesha panya ambao waliwekwa katika mazingira ya taa za mwanga wa LED,walionekana kuathirika macho zaid dhidi ya wale waliowekwa katika vyanzo vya mwanga mwingine.

Watafiti wanashauri matumizi ya mwanga kuepuka matumizi ya mwanga mweupe hasa unaozalishwa na taa za LED,ambao una kiasi kikubwa cha miale ya blue,ambayo ni hatari kwa afya ya macho,na watumie taa za tubelight hasa sehemu za kupumzikia au sehemu ya kulala.

Wataalamu wanasisitiza kuwa macho ya binadamu yana uwezo wa kupambana na miale hii ya blue,lakini uwezo huu hutofautiana kati ya mtu na mtu kwa sababu za kimaumbile lakini pia sababu ya umri,ambapo watoto na watu wazima wapo katika hatari zaidi ya kudhurika na miale hii.

Taa hizi pia husababisha kichwa kuuma kwasababu huwaka na kuzima kwa kila hatua kwa asilimia 100,hii husababisha ubongo kufanya kazi kwa kasi zaidi wakati ukiutafsiri mwanga,kwa kifupi taa hizi hazifai kwa kusomea.wakati taa za kawaida za mwanga mweupe tubelight zenyewe huwaka na kuzima kwa asilimia 30 tu,hivyo hizi hua haziumizi kichwa.

Wataalam wanashauri kuzuiwa kwa miale ya blue katika taa hizi angalau kwa kiwango cha 415-455 nanometer kwa taa ambazo zinatumika majumbani.

Imeandaliwa na Transistor.
Mimi nina umri wa miaka 82 mpaka macho yaharibike nitakuwa sina hamu ya kuona mabinti wazuri hivyo sina cha kupoteza. Kichwa kuuma si rahisi sina kazi hivyo ninashinda nakunywa mbege, sijui kitaanzia wapi! Usingizi utapatikana tu nikisha kata mbege kutwa nzima. My mbege, my dear bottle.
 
Ni kweli kabisa maana nilipata shida ya macho nikajua moja kwa moja tatizo linasababishwa na matumizi yangu ya laptop, nilivyoenda hospitali (ccbrt) daktari alinipima akaniambia sababu tofauti kabisa na niliyokua nafikiria.

Ikabidi nimwambie kuhusu matumizi yangu yaliyokithiri ya laptop, akaniambia mwanga wa vifaa vingi vya kielectronic vya kisasa hauna madhara kama watu wengi tunavyodhani. Akanipa mfano wa computers ambazo zilikua na athari kidogo kwenye macho ni zile za kizamani ambazo mwanga wake ulikua unachezacheza.

Nakumbuka huyu daktari alikua myahudi sio mbongo!
Afadhali kuna good news
 
Back
Top Bottom