Taadhari kwa wapenzi na mashabiki wa Simba Sports Club.

kyata

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2015
Posts
2,535
Reaction score
2,499
Kumekuwa na majigambo mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kutoka kwa wapenzi na mashabiki wa klabu tajwa hapo juu, kwamba kesho wanaua. Napenda kuwashauri, hayo matokeo waliyokuwa nayo waanze kuyafuta vichwani mwao tangia sasa, maana matokeo ya mchezo wa kesho yanaweza kuwa kinyume na matarajio yao hivyo ikwaathiri kisaikologia na ikapelekea kufanya mambo kinyume na utaratibu kama ilivyowahi tokea siku za nyuma. Nadhani wale wapenzi wa mpira mmenielewa. Asanteni kwa kuzingatia hili angalizo.
 
Kwani nyie kandambili mnasema mtafungwa ?
 
Kwani mashabiki wa Yanga hawatambi kwenye mitandao? Waambie na wao watulize mizuka
 
Mkuu hawa mafisi maji wanajiamini sana kipindi hiki na ndo maana walirusha mawe uwanjani kule mwanza na eti yule mpiga kelele wao akawaomba radhi kwa kufungwa! Shenz taip
 
Mkuu yan naona Simba sc inatumia nguvu nyingi mno kufukua makaburi....Mimi sio fan wa Yanga ila Simba inaonekana anaogooa game ndo maana anafukua makaburi
 
Kwani mashabiki wa Yanga hawatambi kwenye mitandao? Waambie na wao watulize mizuka
Mashabiki wa Yanga Sc siyo kiviiile kama niliyowatahadharisha. Huo ndiyo ukweli. Na Yanga siyo watu wa kufanya yasiyofaa uwanjani, hawana Historia hiyo mkuu, sasa kwa mini niwaunganishe. Hata hivyo kama Kama wataona inawhusu nao ni vyema kuchukua tahadhari. Asante mkuu
 
Mpira wa mikia unachezwa na Haji. Anawaamimisha kushinda. Inapokuwa kinyume lazima wang'oe viti au wamshushie lawama mwamuzi.
Kesho wajiandae kung'oa viti tena.

Timu hizi zimekutana mara 101 Yanga ikishinda mara 36.
Yanga inamataji 27 dhidi ya 19 ya Simba.
Yanga imefunga mikia magoli 107 huku mikia wakiifunga 96.

A lot to catch up.
 
Mkuu hawa mafisi maji wanajiamini sana kipindi hiki na ndo maana walirusha mawe uwanjani kule mwanza na eti yule mpiga kelele wao akawaomba radhi kwa kufungwa! Shenz taip
Kweli jina la mtu linaendana na tabia yake
 
Labda unao wajua wewe, mimi huku nilipo mpaka hatulali kwa tambo ambazo hawana uhakika nazo. Unapo sema sio kivile umetumia kipimo au kigezo gani? Halafu acha kuchanganya mada, uzi wako umeongelea kuhusu mashabiki wa Simba SC kujigamba kupita kiasi na sio kufanya vurugu! Wale sio wapumbavu mpaka wafanye vurugu kama hawajachokozwa! Mashabiki wa Yanga toka Simba ilipofungwa na Mbao Fc mpaka leo hatulali wakijigamba kwenye mechi ya kesho! Sasa unataka mashabiki wa Simba wafanyeje?
 
Mkuu yan naona Simba sc inatumia nguvu nyingi mno kufukua makaburi....Mimi sio fan wa Yanga ila Simba inaonekana anaogooa game ndo maana anafukua makaburi
Kivipi inafukua makaburi? Huko kujigamba kuwa itashinda kesho? Kama ingekuwa inaogopa game ya kesho wasinge kubali kuingia kambini na kujiandaa
 
Tunatamba kila kona kwa kua tunajiamini na kikosi chetu.. Na kesho lazima MFE.
 
Hivi jamii forum sio mtandao ..... we mwenyewe ushatumia jf kujitamba tayari...ndo maana kuna baadhi ya vitu hatutoboi kwa sababu ya fikra kama zako....ulitakiwa ubandike bango maeneo yanayopita watu wengi tungekuelewa
 
Mimi nimetoa tahadhari tu mkuu maana kuna watu humu wanayo matokeo yao tayari vichwani, sasa ikiwa kinyume sipati picha.
Hivi jamii forum sio mtandao ..... we mwenyewe ushatumia jf kujitamba tayari...ndo maana kuna baadhi ya vitu hatutoboi kwa sababu ya fikra kama zako....ulitakiwa ubandike bango maeneo yanayopita watu wengi tungekuelewa
 
Kufanya vurugu siyo kwamba MTU anakuwa na akili timamu hapana, hiyo ndiyo kuathirika kisaiklojia mkuu, unashindwa kuhimili unachokishuhudia, matokeo yake unafanya vitu ndiyo siyo kama ilivyotokea huko nyuma mkuu, au umesahau?
 
Kivipi inafukua makaburi? Huko kujigamba kuwa itashinda kesho? Kama ingekuwa inaogopa game ya kesho wasinge kubali kuingia kambini na kujiandaa
Mna rekodi pia ya kukimbia match muda wa mapumziko,kwa mnaweza kuingiza Timu lakini halftime mkaweka mpira kwapani. Hii ni rekodi yenu,Yanga hana tabia hiyo,ni heri umfunge goal hata 5 lakini sio kuweka Mpira kwapani.
 
Na Safari hii Msemaji Hovyo wenu Manara kashasoma mchezo kaamua ajipe ugonjwa ili mkifungwa msimpigie kelele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…