Taarifa gani umewahi kusikia kuhusu Saratani ikakupa shaka?

Taarifa gani umewahi kusikia kuhusu Saratani ikakupa shaka?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766

Kila mwaka Februari 04 huwa ni siku ya kuadhimisha saratani duniani kwa lengo la kutoa elimu, takwimu na uelewa kuhusu Saratani. Na kwa takwimu za mwaka 2024 zimeonesha kuwa bara la Asia ndo linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya waangaa wa Saratani ya shingo ya kizazi

SARATANI NI NINI​

Miili yetu ina chembechembe hai nyingi ambazo huzaliana, hukua, na kufa kwa mpangalio maalum. Chembechembe hizi zinapobadilika na kuanza kuzaliana na kukua katika utaratibu ambao sio wa kawaida ndio zinasababisha saratani. Chembe chembe za Saratani hufuata mfumo huo usio wa kawaida – zinazaliana haraka zaidi bila mpangilio na kukua kwa haraka zaidi na wakati mwingine kuwa na umbile kubwa zaidi. Chembechembe hizi za saratani zisipodhibitiwa/zisipotibiwa mapema zina uwezo wa kusambaa na kuota sehemu nyingine ya mwili wa mhusika

AINA ZA SARATANI
Saratani ni uvimbe unaojitiokeza mahala popote katika mwili wa binadamu, uvimbe huu hauna maumivu yoyote mwanzoni. Saratani zipo za aina nyingi sana na majina yake hutegemea kiungo kilichougua na aina ya chembechembe hai zilizoshambuliwa
Kiungo chochote chaweza shambuliwa mfano
  • Shingo ya mfuko wa kizazi
  • Matiti
  • Ngozi
  • Koo na njia ya chakula Tumbo, utumbo, kongosho, ini
  • Kibofu cha mkojo na tezi dume
  • Mapafu ,ubongo,macho, mifupa,misuli
  • Matezi hasa kwa watoto
  • Damu nk

    NINI HUSABABISHA SARATANI?

    1. Matumizi ya Kemikali
    2. Ulaji mbovu
    3. Kutofanya mazoezi
    4. Kutumia pombe kupita kiasi
    5. Uvutaji wa Sigara

  • DALILI ZA AWALI
    • Kila Saratani huwa na dalili zake kutokana na ilipoanzia
    • Mara nyingi saratani haina maumivu mwanzoni na ni ngumu kugundua hasa kamma iko kwa ndani
    • Uvumbe sehemu yoyote ya mwili
    • Mafindofindo
    • Mabadiliko ya haja kubwa au ndogo
    • Kidonda ambacho hakiponi
    • Damu kutoka bila mpangilio au uchafu usio wa kawaida kutoka sehemu za siri(uke)
    • Shida kumeza au kupumua
 

Kila mwaka Februari 04 huwa ni siku ya kuadhimisha saratani duniani kwa lengo la kutoa elimu, takwimu na uelewa kuhusu Saratani. Na kwa takwimu za mwaka 2024 zimeonesha kuwa bara la Asia ndo linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya waangaa wa Saratani ya shingo ya kizazi

SARATANI NI NINI​

Miili yetu ina chembechembe hai nyingi ambazo huzaliana, hukua, na kufa kwa mpangalio maalum. Chembechembe hizi zinapobadilika na kuanza kuzaliana na kukua katika utaratibu ambao sio wa kawaida ndio zinasababisha saratani. Chembe chembe za Saratani hufuata mfumo huo usio wa kawaida – zinazaliana haraka zaidi bila mpangilio na kukua kwa haraka zaidi na wakati mwingine kuwa na umbile kubwa zaidi. Chembechembe hizi za saratani zisipodhibitiwa/zisipotibiwa mapema zina uwezo wa kusambaa na kuota sehemu nyingine ya mwili wa mhusika

AINA ZA SARATANI
Saratani ni uvimbe unaojitiokeza mahala popote katika mwili wa binadamu, uvimbe huu hauna maumivu yoyote mwanzoni. Saratani zipo za aina nyingi sana na majina yake hutegemea kiungo kilichougua na aina ya chembechembe hai zilizoshambuliwa
Kiungo chochote chaweza shambuliwa mfano
  • Shingo ya mfuko wa kizazi
  • Matiti
  • Ngozi
  • Koo na njia ya chakula Tumbo, utumbo, kongosho, ini
  • Kibofu cha mkojo na tezi dume
  • Mapafu ,ubongo,macho, mifupa,misuli
  • Matezi hasa kwa watoto
  • Damu nk

    NINI HUSABABISHA SARATANI?

    1. Matumizi ya Kemikali
    2. Ulaji mbovu
    3. Kutofanya mazoezi
    4. Kutumia pombe kupita kiasi
    5. Uvutaji wa Sigara

  • DALILI ZA AWALI
    • Kila Saratani huwa na dalili zake kutokana na ilipoanzia
    • Mara nyingi saratani haina maumivu mwanzoni na ni ngumu kugundua hasa kamma iko kwa ndani
    • Uvumbe sehemu yoyote ya mwili
    • Mafindofindo
    • Mabadiliko ya haja kubwa au ndogo
    • Kidonda ambacho hakiponi
    • Damu kutoka bila mpangilio au uchafu usio wa kawaida kutoka sehemu za siri(uke)
    • Shida kumeza au kupumua
Eti kuna watanzania wanatibu saratani. Aha haha
 
Saratani ni matokeo ya sumu au asidi kuzidi mwilini kwa muda mrefu

Mazoezi ya viungo na kula mboga za majani nyingi hasa ambazo hazipikwi ni kinga dhidi ya saratani

Ni ugonjwa wa kawaida ila kisiasa umefanywa uonekane ni ugonjwa wa ajabu ili watu wapige hela
 
Saratani ni matokeo ya sumu au asidi kuzidi mwilini kwa muda mrefu

Mazoezi ya viungo na kula mboga za majani nyingi hasa ambazo hazipikwi ni kinga dhidi ya saratani

Ni ugonjwa wa kawaida ila kisiasa umefanywa uonekane ni ugonjwa wa ajabu ili watu wapige hela
saratani sio ugonjwa wa kawaida Jomba, AChana na huo ugonjwa ni balaa
 
Hizo sababu au visababishi ni nadharia tuu au tuseme vinachochea..ila saratani ni mwili tuu unakosa namna nzuri ya kujiendesha wenyewe..ndo maana kuna nyingine wanakwambia ni za kurithi...
Kuna ndugu yangu alikufa na saratani ya maziwa..hakuwa na tabia hata moja na alikua na mazoezi kwa sbb kazi yake ilikua ni ya movement...

Nyingine zinatokea kwa sbb ya maradhi fulani ya muda mrefu kila mara mahali fulani..mfano saratani ya koo...unakuta mtu anaumwa fangas mara kwa mara za mdomo au kinywa hazitibiwi ipasavyo au zinajirudia rudia...inapelekea hyo sehemu au kiungo hicho kuzaliwa kwa chembe chembe za saratani..
 
Aisee mama wa msanii mkubwa kwa sasa nilisikia yupo Nairobee aliniambia hivi "Mwanangu naoza huku nikiwa hai" hiyo kauli haijawahi kunitoka 💔 R.I.P mama Manka. Note Huyo msanii alikuwa mkubwa zamani 🤣
 
Balaa sana daaah,ukiushinda huo Kuna Ini,Figo,motor,pressure, Yukari,asthma na yote hayo hayaeleweki kabisa
 
Back
Top Bottom