domo bwakubwaku
Member
- Mar 2, 2011
- 86
- 29
Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu wanatakiwa kuwa makini na taarifa zao kwa umma.
1.Kuepuka makosa ya kisarufu na uandishi katika Kiswahili
rejea aya ya tatu sentensi ya pili wameanza na kiunganishi "Na" jamani katika Kiswahili hakuna tungo huru wala tegemezi inayoweza kuanza na kiunganishi hicho.
Ngoja niwarudishe shule.
Matumizi ya NA
i.Kuunganisha neno na neno.
mfano -Mkapa na Kikwete.
ii.Kuunganisha tungo na tungo iwe huru au la.
Mfano Rais Kikwete anaongoza nchi yetu na Mkapa aliongoza nchi yetu.
Muhimu - Kiunganishi NA hakianzi mwanzoni mwa tungo.
2.Kuepuka matumizi ya lugha kavu.
Mfano neno Upuuzi katika aya ya pili sentensi ya kwanza na neno la mwisho.
Tafsiri yake ni kwamba-Ni jambo la kijinga, la kishenzi au lisilo na maana.
Sentensi sahihi ilikuwa ni Kauli hii ya Bwana Lema si ya kweli(ondoa neno Upuuzi).
Muhimu. lugha ya Kiswahili ina desturi zake, kubwa matumzi ya tafsida.
3.Kwa uandishi wa taarifa kwa umma mwandishi anapashwa kuepuka ushabiki (unatakiwa kuwa kati katika mizani) na taarifa inapaswa kuwa fupi ya maneno machache.
4.Kuepuka makosa ya kimantiki
Mfano. Ikulu haipaswi kuisemea Mahakama au kumsemea Jaji Gabriel Rwakibalira lakini mnalo jukumu la kuisemea Ikulu.
5.Kukwepa matumizi ya ubunge kama mtu, ubunge ni jamii- anapigiwa kura na watu wanampa ridhaa ya kuwa mbunge kwa hiyo panapotokea lolote lile iwe kifo, maamuzi ya mahakama, kuachia ngazi aú lingine hatusemi ni la mbunge au Lema au Sumari au Makwega, bali jambo hilo ni la wananchi wote.
Sentensi sahihi tunasema, Wananchi wa jimbo la Arusha Mjini hawana mwakilishi kwa sababu ya... (Msiba, maamuzi ya mahakama, ugonjwa n.k)
6.Kukwepa matumizi ya lugha za dini
Aya ya sita sentensi ya kwanza imemaliziwa ...hakuna mtu mwingine wa kumbebesha msalaba.
Hapo msalaba si kwa lema kukosa ubunge bali wananchi wa jimbo la Arusha Mjini kukosa mwakilishi wao Bungeni. Hilo linaweza kusababisha watu wengine kumbebea huo msalaba.
Muhimu.
Taarifa kama hii inawapa nafasi umma kuhuzunika pamoja na yule anayetajwa katika jambo hilo wakati dhumuni lake lilikuwa na kuondoa utata.
Tuwe makini.
1.Kuepuka makosa ya kisarufu na uandishi katika Kiswahili
rejea aya ya tatu sentensi ya pili wameanza na kiunganishi "Na" jamani katika Kiswahili hakuna tungo huru wala tegemezi inayoweza kuanza na kiunganishi hicho.
Ngoja niwarudishe shule.
Matumizi ya NA
i.Kuunganisha neno na neno.
mfano -Mkapa na Kikwete.
ii.Kuunganisha tungo na tungo iwe huru au la.
Mfano Rais Kikwete anaongoza nchi yetu na Mkapa aliongoza nchi yetu.
Muhimu - Kiunganishi NA hakianzi mwanzoni mwa tungo.
2.Kuepuka matumizi ya lugha kavu.
Mfano neno Upuuzi katika aya ya pili sentensi ya kwanza na neno la mwisho.
Tafsiri yake ni kwamba-Ni jambo la kijinga, la kishenzi au lisilo na maana.
Sentensi sahihi ilikuwa ni Kauli hii ya Bwana Lema si ya kweli(ondoa neno Upuuzi).
Muhimu. lugha ya Kiswahili ina desturi zake, kubwa matumzi ya tafsida.
3.Kwa uandishi wa taarifa kwa umma mwandishi anapashwa kuepuka ushabiki (unatakiwa kuwa kati katika mizani) na taarifa inapaswa kuwa fupi ya maneno machache.
4.Kuepuka makosa ya kimantiki
Mfano. Ikulu haipaswi kuisemea Mahakama au kumsemea Jaji Gabriel Rwakibalira lakini mnalo jukumu la kuisemea Ikulu.
5.Kukwepa matumizi ya ubunge kama mtu, ubunge ni jamii- anapigiwa kura na watu wanampa ridhaa ya kuwa mbunge kwa hiyo panapotokea lolote lile iwe kifo, maamuzi ya mahakama, kuachia ngazi aú lingine hatusemi ni la mbunge au Lema au Sumari au Makwega, bali jambo hilo ni la wananchi wote.
Sentensi sahihi tunasema, Wananchi wa jimbo la Arusha Mjini hawana mwakilishi kwa sababu ya... (Msiba, maamuzi ya mahakama, ugonjwa n.k)
6.Kukwepa matumizi ya lugha za dini
Aya ya sita sentensi ya kwanza imemaliziwa ...hakuna mtu mwingine wa kumbebesha msalaba.
Hapo msalaba si kwa lema kukosa ubunge bali wananchi wa jimbo la Arusha Mjini kukosa mwakilishi wao Bungeni. Hilo linaweza kusababisha watu wengine kumbebea huo msalaba.
Muhimu.
Taarifa kama hii inawapa nafasi umma kuhuzunika pamoja na yule anayetajwa katika jambo hilo wakati dhumuni lake lilikuwa na kuondoa utata.
Tuwe makini.