TAARIFA; Matibabu ya Edgar Mwakabela (SATIVA)

TAARIFA; Matibabu ya Edgar Mwakabela (SATIVA)

Mama Samia kasema atalipa gharama zote za matibabu kuanzia sasa za nyuma wamelipa wasamaria wema wabarikiwe za kuanzia sasa atalipa Raisi Mama Samia hivyo hakuna haja ya michango tena
 
Pamoja na yote hayo, Kwani mpaka sasa hivi POLISI WANASEMAJE??? Hawajaweka Press conference yoyote kulihusu hili swahibu la huyu jamaa???Mkiambiwa kua mnaishi kwenye bara la giza, la nchi masikini sana duniani kwamba uhai wa mtu ni kama chai ya rangi basi mue mnakubali. Sio mkishashiba matapu tapu yenu na tu bia twa Samaki samaki basi mnaanza ngenge bongo New york. Mara Kagame ni dictator, wakati nchini kwake hamna huu upuuzi. Nyanoko bhebhe.
 
Eee Mungu, inua tu watu wako watoe michango.

Hii nchi ni nini hiki
MUNGU ni mkuu Mungu ananguvu kuliko CCM na ndiyo maana leo tumuona hapo amefanya peke yake hana muda na wanaojiita viongozi wa dini wanafiki anajua nao ni wachumia tumbo tu anachora hata uwezo wa watu kumchangia apone ni nguvu zake anataka kutuonesha kwamba yupo hakuna zaidi yake na atawajibu watesi wote.
 
Kama Samia amejitokeza kugharamia matibabu ya Sativa aachwe afanye hivyo, watu wa X wapunguze ujuaji kutegemea michango ambayo hawajui itapatikana kiasi gani, na kwa muda gani, huku mgonjwa akiwa hospitali, wawe makini, watumie na akili.

- Samia kugharamia matibabu ya Sativa ni kodi zetu, ni haki yetu, lakini pia ni jukumu lake akiwa kama chief comforter wetu, aachwe afanye hivyo bila kelele.

Hii issue inahitaji organisation, sio mihemko; kuendelea kuikumbatia watu wa X pekee haitaleta majibu, zaidi itasababisha chuki izidi kukua kwenye jamii yetu.

Hapa tukubaliane au tukatae, Samia ndie kiunganishi wetu kwenye hili suala, kauli yake moja tu ya kukemea utekaji na uteswaji itamaliza kila kitu, aambiwe afanye hivyo akiwa pia anaendelea kusaidia matibabu kwa mgonjwa.

Kuendelea kumchangia Sativa huku tukiendelea kuishi kwenye jamii yenye chuki, itakuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

- Samia anatuchukia? If not, kwanini yupo kimya mpaka leo?

Tutaendelea kutekwa na kuteswa, na wakati mwingine kuuwawa, watawala wao hawatakuwa na hasara yoyote, sisi, familia zetu, na marafiki zetu ndio tutakaoumizwa, akili na busara vitumike.
Mi hata simwamini bi Samia. Ina maana hii plot ya dogo alikua haijui?
 
Back
Top Bottom