Pre GE2025 Taarifa ya kutekwa kwa Abdul Nondo kutoka ACT Wazalendo

Pre GE2025 Taarifa ya kutekwa kwa Abdul Nondo kutoka ACT Wazalendo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

KUTEKWA KWA MWENYEKITI WA NGOME YA VIJANA NDUGU ADBUL NONDO

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ya ACT Wazalendo Ndugu Abdul Omar Nondoametekwa asubuhi hii na watu wasiojulikana akitokea mkoani Kigoma alikokuwa sehemu ya viongozi wa kitaifa walioongoza kampeni kwenye mikoa ya magharibi mwa Tanzania. Nondo aliwasili stendi ya Magufuli iliyopo eneo la Mbezi kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za usajili T 221 DKB

Mashuhuda wa tukio wanasema kuwa kulikuwa na purukushani katika utekaji wa Nondo iliyosababisha begi lake dogo la nguo na pingu iliyobebwa na mmoja wa watekaji kudondoka.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Katibu Mwenezi Mkoa wa Dar es salaam Ndugu Monalisa Ndala na Afisa wa Harakati na Matukio Taifa Ndugu Wiston Mogha waliofika mapema kituoni hapo walitambua haraka kuwa aliyetekwa ni Abdul Nondo kwa sababu walizitambua nguo zake kwenye begi lililodondoka na notebook yake.

Chama kinaendelea kufuatilia taarifa zaidi kuhusu tukio hili na kitatoa taarifa zaidi kwa umma.

Katika hatua ya sasa tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Cammillus Wambura kufuatilia haraka tukio hili na kuhakikisha Ndugu Abdul Nondo anaachiwa huru mara moja.

Imetolewa na:
Mbarala Maharagande,
Naibu Katibu wa Haki za Binadamu na Vyombo vya Uwakilishi wa Wananchi,
ACT Wazalendo.
01 Desemba, 2024.


nondo.jpg

 
Kwa kuwa Abdul Nondo katekwa, anayefuatani Abdul OG mtoto wa mama Abdul..
 
I'm sure soon mudi watabadili heading iwe amechukuliwa na sio ametekwa na watu wasio julikana
 
Mpaka mtu anatekwa mnamuangalia tu, hv hapo magu stand hakuna hata mawe ya kuwapopoa hao jamaa?

Udhaifu huu kwa wanaume wa dar
 
Wakuu,

KUTEKWA KWA MWENYEKITI WA NGOME YA VIJANA NDUGU ADBUL NONDO

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ya ACT Wazalendo Ndugu Abdul Omar Nondoametekwa asubuhi hii na watu wasiojulikana akitokea mkoani Kigoma alikokuwa sehemu ya viongozi wa kitaifa walioongoza kampeni kwenye mikoa ya magharibi mwa Tanzania. Nondo aliwasili stendi ya Magufuli iliyopo eneo la Mbezi kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za usajili T 221 DKB

Mashuhuda wa tukio wanasema kuwa kulikuwa na purukushani katika utekaji wa Nondo iliyosababisha begi lake dogo la nguo na pingu iliyobebwa na mmoja wa watekaji kudondoka.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Katibu Mwenezi Mkoa wa Dar es salaam Ndugu Monalisa Ndala na Afisa wa Harakati na Matukio Taifa Ndugu Wiston Mogha waliofika mapema kituoni hapo walitambua haraka kuwa aliyetekwa ni Abdul Nondo kwa sababu walizitambua nguo zake kwenye begi lililodondoka na notebook yake.

Chama kinaendelea kufuatilia taarifa zaidi kuhusu tukio hili na kitatoa taarifa zaidi kwa umma.

Katika hatua ya sasa tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Cammillus Wambura kufuatilia haraka tukio hili na kuhakikisha Ndugu Abdul Nondo anaachiwa huru mara moja.

Imetolewa na:
Mbarala Maharagande,
Naibu Katibu wa Haki za Binadamu na Vyombo vya Uwakilishi wa Wananchi,
ACT Wazalendo.
01 Desemba, 2024.


Kama sijakosea Abdul Nondo sio mara ya kwanza kutekwa. Ni mzoefu kwa hiyo wa kutekwa. Mara ya kwaza kulikua na dalili kama alijiteka. Itakua vizuri kama safari hii ataonyesha uadilifu kwa kutekwa kweli ili watu wapambane kiukweli kutafuta haki.
 
Kama sijakosea Abdul Nondo sio mara ya kwanza kutekwa. Ni mzoefu kwa hiyo wa kutekwa. Mara ya kwaza kulikua na dalili kama alijiteka. Itakua vizuri kama safari hii ataonyesha uadilifu kwa kutekwa kweli ili watu wapambane kiukweli kutafuta haki.
...'Uadilifu kwa kutekwa'... 🤣🤣😁
 
Viongozi wa ACT Wazalwndo itakuwa ni bussra mkatoa picha ya Abdul Nondo akiwa hospitalni au baada ya kupatikana coco beach au Makao Makuu ys Chama chenu.

Mpaka sasa naona mmechelewa sana kutoa picha zake walau watu wajiridhishe na kuondoa mashaka waliyonayo baadhi ya watu.

Actions speak louder than words.
 
Back
Top Bottom