Taarifa ya Uamuzi wa kamati ya katiba, sheria na hadhi za wachezaji

Acheni mapovu. Point zilishayeyukia uwanja wa Kaitaba. Polisi ya dar nao wakomalie rufani yao ya kombe la FA dhidi ya Paka
 
Acha kujifanya uelewi wewe, Rufaa ya simba sio halali kwa sababu kuu mbili, haikukatwa kwa wakati unaotakiwa na pia hiyo rufaa haikulipiwa ada.
Mpaka hapo haikustahili kusikilizwa.
Kama hamjui hata masharti ya kukata rufaa inabidi tu tuwashangae tu.
Mlitaka isikilizwe bure kisha mpewe point tu za mezani au?
Ana kadi ngapi haina tena maana maana rufaa haikua halali toka mwanzo, kesi inaishia hapo tu.
Rufaa ingekua halali hapo ndipo waliopaswa kuzungumzia ana kadi mbili au tatu.
Kwa hiyo msijichoshe au kutuchosha zingatieni utaratibu tu.
 

Bwana mdogo usinilazimishe kuelewa ujinga.

Siku nyingine unapotaka mjadala na mtu fanya utafiti wa kutosha ili usilete hoja nyepesi kwenye maswali magumu.
Kwa kukusaidia tu nijibu yafuatayo;

1. Nani alikwambia Simba amekata rufaa? Unaelewa tofauti kati ya malalamiko na rufaa?
2. Kama malalamiko ya Simba yako nje ya muda na hayakidhi vigezo kwa nini yalisikilizwa na Kamati ya Saa 72?
3. Tuseme malalamiko ya Simba yako nje ya muda na hayana vigezo, unaweza kutumia siku karibu saba kuisikiliza rufaa ya
Kagera? Unaweza kuleta mashahidi hadi akina Jonisia Rukyaa ili watoe ushahidi gani kwa malalamiko ambayo nyaraka zake hazina vigezo? Unaweza kuahirisha vikao 2 vya maamuzi kwa ajili ya kuamua kama malalamiko yana stakabadhi ya malipo?
4. Malalamiko hayana vigezo, unatuambia hujajua kama kadi ilikuwa ya kumvuta mchezaji mwenzke au kumrukia?

TFF wanafaidika sana na uwepo wa kundi kubwa la watu wasio makini ambao ushabiki na unazi umefanya mshindwe kuona hata vitu rahisi. Wakati sisi tunazungumzia utawala na usimamizi wa mpira una dalili ya ukakasi na mizengwe na si afya kwa mpira wa nchi wewe na baadhi ya washabiki wenzako mnaleta unazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…