DOKEZO Taarifa za kiuchunguzi kwenda Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo juu ya Ukaribishaji wa Jangwa na Njaa

DOKEZO Taarifa za kiuchunguzi kwenda Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo juu ya Ukaribishaji wa Jangwa na Njaa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,778
Reaction score
7,145
Wana JF

Nimekusanya taarifa za kiuchunguzi katika mikoa mbali mbali hasa inayolima ndizi.

Baada ya ujio wa upandaji miti ya mbao aina ya patula pine (pinus patula) nimegundua vitu vingi vimeanza kupotea kutokana na watu wakidhani wameyakabili maisha kwa kupanda miti hii baadae wauze mbao wapate fedha zilizoshikana wafanye mambo mengine, kumbe wameingia mkenge kwa kuharibu ardhi yenye rutuba na kupoteza uoto wa asili.

pine-tree.jpg


Miti hii hupandwa mwezi wa tisa ili Ije ikutane na mvua ya mwezi wa nne. Wanafanya hivyo kuepuka miti kupinda au kudumaa. Miti hii hupandwa kavu kavu baadae hulishwa mbolea ya chumvi chumvi iamke kwa haraka.

Sababu ya kwanini nasema uharibifu wa uoto wa asili na ukaribishaji wa jangwa ni hivi:

Tamaduni za asili ya watu wanaolima ndizi na kahawa hutegemea vitu vifuatavyo, nyasi kwa ajili ya matandaza, mifugo kwa ajili ya mbolea ya mboji au mbolea asilia. Kwa sasa vitu hivi vimekuwa adimu baada ya ujio wa miti aina ya pine

Madhara yatokanayo na pine

Pine ni mmea ambao hutoa mbao nyepesi. Majani yake huchukua takribani ya miaka mitatu kuoza. Majani haya hayana utamaduni wa kuwa rafiki wa wadudu wanaoozesha majani kwa ajili ya kurutubisha ardhi. Wadudu wanaotengeneza afya ya udongo kama minyoo asili, sisimizi na vipepeo wanaodhalisha viwavi wote wamepotea hivyo ardhi husika kukuta imaharibika.

majani.jpg

Uchunguzi wa awali unaonyesha sehemu waliokaribisha miti hii kwa wingi wamepoteza mifugo mingi ambayo ilihusika kutengeneza afya ya udongo. Ng'ombe /mbuzi /kondoo ni wanyama wenye faida wanapokuwa malishoni. Kinyeshi Chao hutumika kama mbolea inayotegemewa na majani na mimea mingine midogo midogo lakini pia wadusus wanaopaa wanaozungusha kichezi wameisha. Wadudu hawa ni maalum kwa kusambaza mbolea wanapokuwa kwenye harakati ya kwenda kuhifadhi chakula ardhini. Sehemu ambayo mkulima huvuna mbao kwenye miti hii hukuchukua miaka mitano ukiweka mbolea ya asili kurutubisha ardhi uweze kulima kitu kingine.

Madhara yatokanayo na kilimo hiki

Sehemu ambayo wamebaki na ardhi ndogo kama Kagera na kilimanjaro wamepata hasara kubwa kwa kilimo mbadala kama mahindi, njugu mawe, viazi vitamu, magimbi, njugu mawe, karanga na alizeti. Ukosefu wa malisho kwa wanyama asili. Hivyo ongezeko la lishe duni linalotokana na ukosefu wa maziwa , nyama na mafuta ya wanyama na mimea kama alizeti mihogo na karanga.

Kagera ni mwathirika namba 1 kwa kuwa ardhi iliyokuwa inatumiwa na watu maskini kwa ajili ya kulima mazao mbadala kujikimu na maisha ardhi yote imatwaliwa. Ardhi hii iliachwa na mababu kwa ajiri ya malisho na watu kulima mazao ya muda mfupi. Kwa sasa hivi kagera kuna marumbano ambayo yanaweza kuleta mapigano kati ya wafugaji na wakulima.

Niwaombe wizara ya kilimo wakutane na wizara ya mifugo wafanye kampeni ya kupunguza miti hii lakini pia ardhi ya vijiji na shule ambayo imelimwa miti hii iondolewe watu wapate malisho na mazao mbadala
 
Karibu Tanzania mleta mada
Asante. Idadi ya mifugo umepunguzwa sana na miti hii watu wamekosa malisho na nyasi za kulisha ng'ombe na mbuzi wanao fugiwa nyumbani zimeisha. Wadudu waliokuwa wanaishi maporini sasa wameamia kwenye mashamba baada ya kukosa majani na virutubisho vingine kwenye sehemu iliyotumika kama malisho.
 
Hili limekuwa tatizo maeneo Mengi ambako mazao ya kudumu kama mikorosho, michikichi na miparachichi inapandwa kwenye maeneo yenye kufaa kwa kilimo cha mazao ya msimu na ufugaji
 
Hili limekuwa tatizo maeneo Mengi ambako mazao ya kudumu kama mikorosho, michikichi na miparachichi inapandwa kwenye maeneo yenye kufaa kwa kilimo cha mazao ya msimu na ufugaji
Tutegemee magonjwa yanayotokana na utapia mulo wakati serikali ipo bize kuongeza vituo vya afya bila kujua kuwa magonjwq mengi yanachagizwa na afya mbovu. Sehemu zenye chakula cha kutosha kama njombe au mbeya ina idadi ndogo ya wagonjwa. Sasa mifugo yote ikitoweka , mazao kama alizeti na mahindi yakitoweka kutokana na ukosefu wa ardhi si vifo vitaongezeka zaidi kwa lishe mbovu
 
Tutegemee magonjwa yanayotokana na utapia mulo wakati serikali ipo bize kuongeza vituo vya afya bila kujua kuwa magonjwq mengi yanachagizwa na afya mbovu. Sehemu zenye chakula cha kutosha kama njombe au mbeya ina idadi ndogo ya wagonjwa. Sasa mifugo yote ikitoweka , mazao kama alizeti na mahindi yakitoweka kutokana na ukosefu wa ardhi si vifo vitaongezeka zaidi kwa lishe mbovu
Kuna haja ya kuweka makatazo ama udhibiti wa kilimo cha miti na mazao ya kudumu ili kutoingia kwenye tatzo ka njaa na utapiamulo
 
Hi ilipasawa iwe stories of changes tuipigie kura
 
utapia mulo wakati serikali ipo bize kuongeza vituo vya afya bila kujua kuwa magonjwq mengi yanachagizwa na afya mbovu
Nje ya mada lakini inashabihiina.
Ni kuwa, wakati wa COVID-19, Biashara ya kuuza madawa ya kutibu kuhara ilikufa kabisa kwa watu wengi kujali usafi wa mikono na tiba nyingine za nyungu.

Nilitaka tu hili niliweke wazi kuwa Kuna umuhimu wakutunza mimea ya asili ambayo imekuwa bega kwa bega nasi kutuvusha katika afya na good practice ya kunawa mikono.
 
Nje ya mada lakini inashabihiina.
Ni kuwa, wakati wa COVID-19, Biashara ya kuuza madawa ya kutibu kuhara ilikufa kabisa kwa watu wengi kujali usafi wa mikono na tiba nyingine za nyungu.

Nilitaka tu hili niliweke wazi kuwa Kuna umuhimu wakutunza mimea ya asili ambayo imekuwa bega kwa bega nasi kutuvusha katika afya na good practice ya kunawa mikono.
Sawa kabisa misitu mingi inatoweka wataalum wanapotea. Mimi utotoni nilifundishwa madawa mengi ya asili na wanyama. Sasa hivi uwezi kupata dawa kwa sababu misitu mingi ya asili vijijini imekatatwa. Wanyama wanakufa kwa home. Nilienda Rwanda bado wana mifugo mizuri na ng'ombe wanapendeza. Njoo Tanzania maziwa na samli vya shida sana. Wakulima wadogo mix cultivation walisaidiana sana na wafugaji. Huyu analeta maziwa na nyma huyu analeta ndizi, maharage na mahindi tunaishi. Sasa mfugaji anakufa hili si janga?
 
Hakuna kitu hapa mkuu. Bandiko lake lina loopholes nyingi sana. Jamaa kaandika kama mtoto wa Darasa la 5C.
Ni kweli mimi ni mkulima siitaji usomi wowote kwani kwa sasa haunipi chakula zaidi ya kukufugia kuku na kukulimia mahindi ili uje na usomi wako kunitoza tozo za kimangumashi ili ununue viete wakati Tarafa zima hakuna trekta . Wala watafiti wa dawa na maduka ya dawa. Lakini hili halinizuii kupiga kampain ya kupunguza miti tusiingie kwenye majanga
 
Hakuna kitu hapa mkuu. Bandiko lake lina loopholes nyingi sana. Jamaa kaandika kama mtoto wa Darasa la 5C.
Ni kweli mimi ni mkulima siitaji usomi wowote kwani kwa sasa haunipi chakula zaidi ya kukufugia kuku na kukulimia mahindi ili uje na usomi wako kunitoza tozo za kimangumashi ili ununue viete wakati Tarafa zima hakuna trekta . Wala watafiti wa dawa na maduka ya dawa. Lakini hili halinizuii kupiga kampain ya kupunguza miti tusiingie kwenye maja
 
Hayo ndo matatizo ya kuiga na kutanguliza pesa mbele bila kufanya upembuzi yakinifu, kiufupi ni kukurupuka.......huwezi kuanzisha kilimo cha miti, mkonge, kilimo cha nyonyo sijui na kilimo gani kisa umesikia kuna soko marekani huku ukijua unaenda kuharibu rutuba na ecosystem ya ardhi na kutumia ardhi inayotumika kwa ajili ya kuzalisha chakula.​
 
Umeandika jambo kubwa na nyeti sana.

Lakini nakupa pole. Sasa hivi hatuna viongozi wenye maono, pia...
Suala la "UJENZI WA TAIFA" hakuna kiongozi anayeumiza kichwa.

Nyerere pamoja na mapungufu yake, ndiye kiongozi pekee aliyekuwa anaifikiria kesho ya watu wake.

Kiufupi tujipe pole, kazi ni ngumu sana nchi hii.
 
Mm bjnafsi Nina shamba langu la miti hi pine maeneo ya iganzo mbeya uko vijini wateja wananisumbua sna saa HV wanantaka kununua mbao hzo sas nashangaa sna unanipanikisha kuwa haipazwi kivip

Zimbabwe ndio nnchi inaaongoza kwa kupanda miti hiiyo na inawalipa haswa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mm bjnafsi Nina shamba langu la miti hi pine maeneo ya iganzo mbeya uko vijini wateja wananisumbua sna saa HV wanantaka kununua mbao hzo sas nashangaa sna unanipanikisha kuwa haipazwi kivip

Zimbabwe ndio nnchi inaaongoza kwa kupanda miti hiiyo na inawalipa haswa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Huko mbeya bado wana ardhi kubwa. Mikoa ya kagera na kilimanjaro hakuna ardhi kabisa na malisho ya mifugo. Hofu ni kupata jangwa na kuharibu ecology. Sehemu ya kupanda pain mti uje kuuza elf 10 na unasubiri miaka 10 wakati mikahawa aina mpya arabika miaka 2 unaanza kuvuna
 
Back
Top Bottom