Taasisi ya Elimu ya watu wazima haijafanya malipo kwa miezi mitatu mfululizo bila taarifa yoyote

Taasisi ya Elimu ya watu wazima haijafanya malipo kwa miezi mitatu mfululizo bila taarifa yoyote

jumapondamali

Member
Joined
Nov 1, 2024
Posts
8
Reaction score
1
Mradi wa SEQUIP - AEP unafadhiliwa na Benki ya Dunia na unatekelezwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI. Mradi huu unalenga kuwarudisha watoto wa kike waliokatisha masomo kwa sababu mbalimbali kupitia elimu mbadala (Alternative Education Pathway).

Mpaka sasa umepita muda wa miezi miwili mfululizo wawezeshaji (walimu) katika mradi huu hawajalipwa stahiki zao bila taarifa yoyote. Malipo yamelipwa kwa mara ya mwisho mwezi Agosti, 2024. Malipo ya mwezi Septemba, Oktoba na Novemba hayajafanyika.

Hata hivyo, tangu kuanzishwa kwa mradi huu malipo yamekuwa yakisuasua kwa malipo ya mwezi husika (yaani malipo ya mwezi wa kwanza yamekuwa yakilpwa mwezi wa pili mwishoni au wa tatu mwanzoni) hali inayopelekea walimu kufanya kazi kwa manung'uniko.

Tunaomba mamlaka husika itoe ufafanuzi juu ya malipo kwa watumishi hao kwani mpaka sasa hakuna taarifa yoyote ile.
 
Mradi wa SEQUIP - AEP unafadhiliwa na Benki ya Dunia na unatekelezwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI. Mradi huu unalenga kuwarudisha watoto wa kike waliokatisha masomo kwa sababu mbalimbali kupitia elimu mbadala (Alternative Education Pathway).

Mpaka sasa umepita muda wa miezi miwili mfululizo wawezeshaji (walimu) katika mradi huu hawajalipwa stahiki zao bila taarifa yoyote. Malipo yamelipwa kwa mara ya mwisho mwezi Agosti, 2024. Malipo ya mwezi Septemba, Oktoba na Novemba hayajafanyika.

Hata hivyo, tangu kuanzishwa kwa mradi huu malipo yamekuwa yakisuasua kwa malipo ya mwezi husika (yaani malipo ya mwezi wa kwanza yamekuwa yakilpwa mwezi wa pili mwishoni au wa tatu mwanzoni) hali inayopelekea walimu kufanya kazi kwa manung'uniko.

Tunaomba mamlaka husika itoe ufafanuzi juu ya malipo kwa watumishi hao kwani mpaka sasa hakuna taarifa yoyote ile.​
 
Jambo n moja tu, acheni kaz ili waje kufundisha wenyew
 
Back
Top Bottom