Taasisi za dini zianzishe utarabu wa kuwaunganisha vijana/ndoa

Taasisi za dini zianzishe utarabu wa kuwaunganisha vijana/ndoa

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Kutokana na mabadiliko makubwa ya Sayansi na Teknologia, Kumekuwa na changamoto kubwa sana kwa vijana wa kike na kiume kupata wenza sahihi wa kuoa/kuolewa na kwa wakati sahihi; Hii ni kutokana na mfumo mzima wa Elimu nk
Nashauri Makanisa na Misikini ianzishe utaratibu rafiki (wa faragha) ambao utaweza kuwakutanisha Vijana ( wa kike na kiume) ambapo Kijana atafika kwa wazee wa kanisa/Msikiti (kwa wakati wake) huku ameandika sifa za Msichana/Mume anayetamani kuwa naye;
Mfano kijana wa Kiume ataandika;
  • Majina yake kamili
  • Anakaa wapi - akiambatanisha na copy ya kitambulisho chake cha taifa
  • Ameoa au alishawahi kuoa? (kwa waislam kutakuwa na nyongeza, mke wa ngapi?
  • Makazi (ananyumba, amepanga, anaishi kwa ndugu, anaishi kwa wazazi nk)
  • Majina na mawasiliano ya ndugu yake angalau mmoja (yaweza kuwa mzazi) nk
  • Anajishughulisha na nini na wastani wa kipato chake kwa mwezi
  • Sifa za anayemtaka (sifa ataandika mwenyewe)
  • Huu ni mfano tu ila Vigezo vinaweza kupangwa vizuri
Hapo wazee watapata nafasi ya kumuuliza maswali kadhaa kujiridhisha kama yupo tayari kuoa.
Vile vile wasichana wapate nafasi kama hiyo
Baada ya hapo wazee wa Kanisa/Msikiti watakaa na kupitia maombi ya pande mbili na kuanza kuona yanayo endana na kuwa kutanisha (faragha) kuona kama wataendana/watakubaliana.
Tunaweza kuta tunapata Ndoa bora na Imara kuliko nyingi za sasa hivi!!!
Hii haibadilishi utaratibu ulioko sasa hivi; Kijana atachagua mwenyewe njia anayo ona ni njema kwake !
 
Sikupingi sema hapa changamoto ni tabia unaweza pata sifa zote unazo taka lakini tabia ukaja kuifahamu baada ya kuwa karibu na mwenza wako ..... mfano mwanamke akawa na sifa zote kwa mwonekano lakini hashiki mimba au mwanaume hana uwezo wa kuzalisha mbegu hazina nguvu za kutunngisha mimba changamoto kama hizi kwa sisi tumesha ziona sana
 
Sikupingi sema hapa changamoto ni tabia unaweza pata sifa zote unazo taka lakini tabia ukaja kuifahamu baada ya kuwa karibu na mwenza wako ..... mfano mwanamke akawa na sifa zote kwa mwonekano lakini hashiki mimba au mwanaume hana uwezo wa kuzalisha mbegu hazina nguvu za kutunngisha mimba changamoto kama hizi kwa sisi tumesha ziona sana
Mimi nimeongelea Mahusiano yaliyo halalishwa kanisani/Misikitini ambapo Mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Naona mawazo yako yamelenga Ndoa kwa mfumo wa mtaani ambapo mnapeana kwanza mimba ndio muoane kitu ambacho sio maelekezo ya Mungu. Ila pia Unaweza kuoa/olewa na mwenye mtoto kwani wapo pia mtaani
 
Umakini mkubwa unahitajika vinginevyo RISASI 7
 
Nishawahi sikia Msikitini Shekhe akitangaza kuna mwanamke mwenye wasifu huu na huu anahitaji mume hivyo aliyeko tayari anajitokeza.

Halafu nadhani sio mpaka waweje utaratibu ila mimi nina imani kama ninahitaji mume kupitia utaratibu huo namfuata kiongozi wangu wa dini namweleza hitaji langu nadhani nitasaidika mana anaweza tangaza au anaweza akawa anajua watu ambao nao wanauhitaji huo.

Nadhani kwa upande wa dini nyingine wanafanya sema haujawekwa rasmi kama utaratibu ila watu wanaoana sana tu hasa huku kwenye Makanisa yasiyo na majina huku mtaani.

Kama utakuwa na faida wauweke tu ilimradi tu unafuata taratibu za kiimani na hazitaleta mkanganyiko.

Kuna page naifuatilia Instagram kwa naona watu wanaconnectiwa na kuoana ila ni mtu binafsi kaianzisha nadhani ila kwa waislamu tu na kuna kiwango unalipia kama sikosei tangazo linabandikwa pamoja na sifa zako mtu akikuridhia huko sasa ndio sijui wanafuata taratibu gani mpaka ndoa.
 
Nishawahi sikia Msikitini Shekhe Kuna mwanamke mwenye wasifu huu na huu anahitaji mume hivyo aliyeko tayari anajitokeza.
Halafu nadhani sio mpaka waweje utaratibu ila mimi nina imani kama ninahitaji mume kupitia utaratibu huo namfuata kiongozi wangu wa dini namweleza hitaji langu nadhani nitasaidika mana anaweza tangaza au anaweza akawa anajua watu ambao nao wanauhitaji huo.
Nadhani kwa upande wa dini nyingine wanafanya sema haujawekwa rasmi kama utaratibu ila watu wanaoana sana tu hasa huku kwenye Makanisa yasiyo na majina huku mtaani.
Kama utakuwa na faida wauweke tu ilimradi tu unafuata taratibu za kiimani na hazitaleta mkanganyiko.
Kuna page naifuatilia Instagram kwa naona watu wanaconnectiwa na kuoana ila ni mtu binafsi kaianzisha nadhani ila kwa waislamu tu na kuna kiwangu unalipia kama sikosei tangazo linabandikwa pamoja na sifa zako mtu akikuridhia huko sasa ndio sijui wanafuata taratibu gani mpaka ndoa.
Nipe hiyo page
 
Back
Top Bottom