Taazia: Augustino Lyatonga Mrema (1944 - 2022)

Taazia: Augustino Lyatonga Mrema (1944 - 2022)

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
TAAZIA: AUGUSTINO MREMA (1944 - 2022)

Mohamed Mlamali Adam alimwandikia taazia Thabit Kombo alipofariki.

Kalamu ya Mlamali akiandika kwa lugha yeyote iwe Kiswahili au Kiingereza inastarehesha lakini pia inaumiza kwani inakata kama upanga wa Sayyidna Ali.

Naisoma taazi na kuirejea mara mbili mbili.
Nairejea kwa sababu inanitatiza.

Hii ni taazia au makala ya kawaida tu?
Najiuliza.

Taazia inapitisha kichwani mwangu maisha ya mwanasiasa mkubwa katika historia ya mapinduzi ya Zanzibar lakini sioni kitu hiki ndani ya taazia.

Haikuwa taazia kama taazia zilivyozoeleka kuandikwa.
Kwa nini?

Ninachokiona kinalingana na maneno ya Cassius katika Julius Caesar anapomweleza Brutus ukubwa wa Colossus (sanamu kubwa la mtu) na akilifananisha hilo Colossus na na kiongozi wa Roma, Julius Caesar.

Najiuliza Mlamali anataka kutupa ujumbe gani katika maisha ya Thabit Kombo?

Mimi nalijua Colossus na nayajua maneno ya Cassius.

CASSIUS: Why, man, he doth bestride the narrow world
Like a Colossus, and we petty men
Walk under his huge legs and peep about
To find ourselves dishonorable graves.

Men at some time are masters of their fates.
The fault, dear Brutus, is not in our stars,
But in ourselves, that we are underlings.

(Sawa kwani aitagaa dunia finyu hii
Kama jitu na sisi vijitu vidogo twapita
Chini ya miguu yake na kuchungulia kote
Na kujikuta katika makaburi ya fedheha.

Watu wakati mwingine hutawala sudi zao:
Lawama, mpenzi Brutus, si la nyota zetu
Kwamba tu watu wa chini, bali ni letu wenyewe).

(Kutoka tafsiri ya Julius Nyerere ya ''Julius Caesar,'' (1963).

Mwalimu Nyerere katafsiri ''Colossus,'' kama ''Jitu.''

Kuna mtu alipata kusema kuwa katika tafsiri hii Mwalimu alifanya kazi ndogo sana na tafsiri yote ilimwelemea Sheikh Abdillah Nasir aliyekuwa Mkurugenzi wa Oxford University Press (OUP), Nairobi.

OUP walihamaki sana kwa kauli hii kiasi huyu mwalimu wangu juu ya kuwa alikuwa na msaada mkubwa kwao walimtoa kwenye jopo la kuandika Kamusi ya Kiswahili.

Nilikwenda kumtembelea Sheikh Abdillah Nasir nyumbani kwake Mombasa miaka michache iliyopita na nikamuuliza kuhusu hili.

Sheikh alicheka sana.
Turejee kwa Augustino Mrema.

Siasa za Afrika ukizitafuta katika kitabu kama hicho hapo juu utazikuta humo.

Unachohitaji kufanya ni wewe ujifnze kutafsiri maneno na matukio.

Shakespeare anazungumza kuhusu ''majitu,'' na ''vijitu'' na wale wadogo na wanyonge, watu dhaifu walioko chini miguuni, watu wasio na sauti wala watu wa kuwatetea.

Sasa kinapotokea kifo cha mtu aliyekuwa mkubwa akawa na sauti watu haraka humkumbuka kwa yale yake.

Kuhusu Thabit Kombo alipokufa Mlamali aliandika maneno haya:

‘’The death of Thabit Kombo reminds one of other old grand venerable founding fathers of the ruling party in Tanzania.

The good Samatitan John Rupia whose property was later nationalised.

The nice cheerful Mzee Sampat who toiled for measly wages and died a poor man.

The Sweet Abdul Sykes who risked his job as Market Master under colonial government in order to set up the party.

And others.

They have passed away, their dedication and love of country not quite fully requited.

Thabit, however, has all along had it good.

Neither his power and reputation nor his immense wealth were ever assailed.

How did he do it?’’
(Africa Events October 1986).

Si bure kuwa Mlamali kawataja watu watatu kutaka watu wafanye ulinganisho katika yale waliyoifanyia nchi yao bila kutaka kufaidika binafsi.

Kamtaja John Rupia, Mzee Sampat na Abdul Sykes.

Ikiwa ulipata kuwajua wazalendo hawa utaelewa Mlamali amekusudia kusema kitu gani.

Ukisoma kitabu cha Rais Ali Hassan Mwinyi, ''Mzee Rukhsa Safari ya Maisha Yangu,'' (2021) Rais Mwinyi kamweleza Augustino Mrema (uk. 269 - 273) kwa njia ambayo msomaji atajiuliza ashike lipi?

Kipi msomaji aamini kuwa hivi ndivyo alivyokuwa Mrema?

Mimi nilijiuliza.

Mrema anaingia wapi katika ile kauli ya Cassius ya, ''Jitu'' na ''Vijitu?''

Rais Mwinyi anasema katika kumbukumbu zake kuwa Augustino Mrema ilifikia wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamu Waziri Mkuu aliweza kumfunika Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania (uk. 270).

Katika utawala wa Rais Mwinyi na uhusiano wake na Augustino Mrema ni pale Mrema alipopambana na Waislam kutokana na sakata la kuvunjwa kwa mabucha yaliyokuwa yanauza nyama ya nguruwe ndiko hakika unaweza kusema hapo ndipo Rais Mwinyi alipopokonywa madaraka na nguvu zake kama Rais.

Sakata hili liliwaumiza watu wengi sana.

Mmoja katika hao alikuwa marehemu Sheikh Kassim Juma mtu aliyekuwa rafiki wa Rais aliyekamatwa akiwa njiani akielekea Nairobi kwenye matibabu.

Nyakati zilikuwa ngumu kwa Waislam.

Kwa mara ya kwanza Waislam waliandamana na kupambana na vyombo vya dola katika mitaa ya Dar es Salaam, Mrema akiwa hayuko mbali katika fikra na vinywa vyao.

Katika kitabu chake Rais Mwinyi kamsifia Mrema.

Mrema alipoamua kujitoa CCM na kuhamia upinzani gazeti la CCM Uhuru, gazeti la chama ambacho Rais Mwinyi alikuwa mwenyekiti wake lilimtangaza na kumpamba Mrema vizuri ukurasa wa mbele kwa wino mweusi uliokoza.

Mrema kwa hili akawa kasimama pazuri sana kwani alikuwa msumari wa moto juu ya kidonda cha Rais Mwinyi.

Rais Mwinyi alipata kumfananisha Mrema na kichwa cha gramophone kilichokwama kwenye santuri iliyomeguka pale alipokuwa akimshambulia yeye katika kesi iliyokuwa mashuhuri ya Chavda.

Mrema kama alivyopanda ghafla na ghafla akafifia aste aste yaani kwa taratibu akawa kama vile hakupata hata kuwepo.

Pamoja na yeye na chama chake ambacho Mrema alikuwa mwenyekiti, nacho kikawa pembeni kikimsindikiza kutoweka pazia lilipoanza kujifunga na wale waliokuwa ukumbini wakiangalia onesho wakinyanyuka vitini kutoka nje ya ukumbi.

Cassius alipata kuzungumza kuhusu "Vijitu," wakichungulia chini ya miguu mikubwa ya "Jitu."

Kipande hiki katika mchezo maarufu wa William Shakespeare, ''Julius Caesar,'' ni moja ya vipande ninavyovipenda sana.

Tumuage Augustino Mrema kwa salama kwani juu ya yote kaisaidia Tanzania kujielewa na kuielewa historia yake kwani juu ya yote aliyofanya, Rais Mwinyi kiongozi mkuu wa serikali aliyoitumikia kisha akaiasi kamsifia kwa maneno haya:

''Pamoja na hila zote alizozifanya ili kujisogeza kwenye barabara ya kuendea kwenye urais, Mrema alifanya mengi mazuri katika enzi ya utawala wangu.

Sina budi kukiri deni la hisani kwangu - kama si kwa nia njema basi kwa vitendo vyake.''

Buriani Augustino Lyatonga Mrema.

1661161536226.png
1661161582160.png
1661161626301.png

1661161742718.png
 
Yaani mambo yote aliyofanya utayaweka kwenye angle ya udini tu.
Randy...
Kwangu ni historia muhimu ya Waislam wa Tanzania na serikali.

Ikiwa kuandika historia ya Waislam kwako ni udini labda hapo tunatofautiana katika maana ya udini.

Katika kipindi hicho masheikh walikuwa wanavamiwa usiku wa manane katika nyumba zao wanakamatwa bila ya heshima na kupelekwa rumande katika vituo vya polisi.

Hapo ndipo unapokuja umuhimu wao kunifanya mimi kutafiti na kuandika historia hiyo.

Kwangu huu si udini.

Udini kwetu sisi Waislam ni kutumia imani yako kunufaisha dini yako na kuwaweka wenye imani tofauti na wewe pembeni.

Kwa mfano TAMISEMI watatangaza kazi ya ualimu na pakawa na waombaji idadi karibu sawa baina ya Waislam na Wakristo.

Ikiwa Wakristo watakuwa wengi sana kupita Waislam katika kupata kazi huo unakuwa udini.

Lakini si kuwa mathalan Kanisa Katoliki liandike historia ya Peramiho jinsi kanisa lilisaidia katika elimu na afya basi mimi nilalamike kuwa wanaandika chembelecho, ''angle ya udini.''

Au niandike jinsi Waislam walivyoshiriki kwa wingi katika kupigania uhuru wa Tanganyika iwe naandika udini.

Nakushukuru sana kwa ''comment,'' yako umenipa fursa ya kujieleza.
 
Mzee Mohamed Said. Umeandika vyema Sana. Pengine. Lakini kuhusu Mrema kupaa kwake , anguko lake na kifo Hapo majuzi Ni Kama umeepuka kiitwacho main topic ya taazia.
Nashangaa! Ama LabdA mie si msomi mwenye ubongo mpana lakini mfananisho wa matukio ya taazia ya vifo Ni makubwa kuliko taazia ya Lyatonga Mrema mhusika mkuu
 
Randy...
Kwangu ni historia muhimu ya Waislam wa Tanzania na serikali.

Ikiwa kuandika historia ya Waislam kwako ni udini labda hapo tunatofautiana katika maana ya udini.

Katika kipindi hicho masheikh walikuwa wanavamiwa usiku wa manane katika nyumba zao wanakamatwa bila ya heshima na kupelekwa rumande katika vituo vya polisi.

Hapo ndipo unapokuja umuhimu wao kunifanya mimi kutafiti na kuandika historia hiyo.

Kwangu huu si udini.

Udini kwetu sisi Waislam ni kutumia imani yako kunufaisha dini yako na kuwaweka wenye imani tofauti na wewe pembeni.

Kwa mfano TAMISEMI watatangaza kazi ya ualimu na pakawa na waombaji idadi karibu sawa baina ya Waislam na Wakristo.

Ikiwa Wakristo watakuwa wengi sana kupita Waislam katika kupata kazi huo unakuwa udini.

Lakini si kuwa mathalan Kanisa Katoliki liandike historia ya Peramiho jinsi kanisa lilisaidia katika elimu na afya basi mimi nilalamike kuwa wanaandika chembelecho, ''angle ya udini.''

Au niandike jinsi Waislam walivyoshiriki kwa wingi katika kupigania uhuru wa Tanganyika iwe naandika udini.

Nakushukuru sana kwa ''comment,'' yako umenipa fursa ya kujieleza.
Yes.

Katika huo mfano wako imeonyesha ni wazi kuwa kabla ya kila kitu unachambua jicho kwa udini kabla ya jambo lingine lolote.


We unaamini waombaji wa ajira waliopitia mchakato wa interview wanaweza kuwa 50% kwa 50% katika kazi, ni mfano ambao hauna uhalisia.

Sehemu pekee ambayo unaweza kuleta 50% ni kwenye uteuzi, ambapo kabisa mteuaji ni wazi ataangalia dini lakini sio katika mchakato wa kuomba ajira .

Unaleta hesabu ambazo hazipo kabisa Duniani.


Kingine, Dini sio ukristo na uislamu pekee, vipi wapagani na wenyewe wakiomba wawe considered ?
 
Mzee Mohamed Said. Umeandika vyema Sana. Pengine. Lakini kuhusu Mrema kupaa kwake , anguko lake na kifo Hapo majuzi Ni Kama umeepuka kiitwacho main topic ya taazia.
Nashangaa! Ama LabdA mie si msomi mwenye ubongo mpana lakini mfananisho wa matukio ya taazia ya vifo Ni makubwa kuliko taazia ya Lyatonga Mrema mhusika mkuu
Nilianz kumhoji hapo
 
Mzee Mohamed Said. Umeandika vyema Sana. Pengine. Lakini kuhusu Mrema kupaa kwake , anguko lake na kifo Hapo majuzi Ni Kama umeepuka kiitwacho main topic ya taazia.
Nashangaa! Ama LabdA mie si msomi mwenye ubongo mpana lakini mfananisho wa matukio ya taazia ya vifo Ni makubwa kuliko taazia ya Lyatonga Mrema mhusika mkuu
Sela...
Ulitegemea niseme nini katika taazia ya Mrema ambacho sikukisema?
 
Umeongelea mengine kibao ukaamuacha Lyatonga
Sela...
Hiyo ndiyo staili ya uandishi wangu.

Vifo viwili nieleta cha Thabit Kombo na Augustino Mrema.
Ikiwa unaijua historia ya Thabit Kombo kuna kitu utakipata hapo.

Nikakuletea mwandishi mkubwa ulimwenguni na William Shakespeare - ''Julius Caesar''

Nikamleta Mohamed Mlamali Adam bingwa wa lugha ya Kiingereza anamzungumza Thabit Kombo.

Mimi nkamzungumza Mrema kwa kuakisi hao niliowataja na mikasa iliyomo kwao waliyotueleza.

Nikahitimisha na Rais Mwinyi.
Wako wengi walionielewa.

Hangaisha akili yako.
Soma na usichoke kujifunza.
 
Yes.

Katika huo mfano wako imeonyesha ni wazi kuwa kabla ya kila kitu unachambua jicho kwa udini kabla ya jambo lingine lolote.


We unaamini waombaji wa ajira waliopitia mchakato wa interview wanaweza kuwa 50% kwa 50% katika kazi, ni mfano ambao hauna uhalisia.

Sehemu pekee ambayo unaweza kuleta 50% ni kwenye uteuzi, ambapo kabisa mteuaji ni wazi ataangalia dini lakini sio katika mchakato wa kuomba ajira .

Unaleta hesabu ambazo hazipo kabisa Duniani.


Kingine, Dini sio ukristo na uislamu pekee, vipi wapagani na wenyewe wakiomba wawe considered ?
Randy...
Fanya utafiti wako kuhusu TAMISEMI na teuzi zake utapata jibu.
Kuhusu Wapagani.

Wapagani wana historia yoyote katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?
Unakijua chama chao au mchango wao katika kupigani uhuru?

Unaifahamu hata idadi yao na wapi tunaweza kuwapata hao Wapagani?
Umepata kusoma kitabu hiki?:
The Life and Times of Abdulwahid Sykes
(1924-1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
1661290417182.jpeg
 
Mrema aliwagaraza CCM ubunge wa Temeke, CCM walituma timu nzima Temeke na viongozi wao wa kitaifa wote kuanzia Raisi mpaka katibu mkuu wa CCM kupiga kampeni Temeke lakini haikusaidia, mwamba aliwapiga chini kisawasawa, nafikiri baada ya hapo CCM wakagundua bila wizi ni watupu na watapoteza nchi sio miaka mingi ndio maana sasa ni wezi wa kura kuliko vyama vyote vya kisiasa duniani
 
Randy...
Kwangu ni historia muhimu ya Waislam wa Tanzania na serikali.

Ikiwa kuandika historia ya Waislam kwako ni udini labda hapo tunatofautiana katika maana ya udini.

Katika kipindi hicho masheikh walikuwa wanavamiwa usiku wa manane katika nyumba zao wanakamatwa bila ya heshima na kupelekwa rumande katika vituo vya polisi.

Hapo ndipo unapokuja umuhimu wao kunifanya mimi kutafiti na kuandika historia hiyo.

Kwangu huu si udini.

Udini kwetu sisi Waislam ni kutumia imani yako kunufaisha dini yako na kuwaweka wenye imani tofauti na wewe pembeni.

Kwa mfano TAMISEMI watatangaza kazi ya ualimu na pakawa na waombaji idadi karibu sawa baina ya Waislam na Wakristo.

Ikiwa Wakristo watakuwa wengi sana kupita Waislam katika kupata kazi huo unakuwa udini.

Lakini si kuwa mathalan Kanisa Katoliki liandike historia ya Peramiho jinsi kanisa lilisaidia katika elimu na afya basi mimi nilalamike kuwa wanaandika chembelecho, ''angle ya udini.''

Au niandike jinsi Waislam walivyoshiriki kwa wingi katika kupigania uhuru wa Tanganyika iwe naandika udini.

Nakushukuru sana kwa ''comment,'' yako umenipa fursa ya kujieleza.
Nimejifunza jambo moja kwenye andishi

Kila mtu huwa na mtazamo wake kwenye kila jambo ama tukio.

Sidhanj kama ni sahihi kukushambulia. Tukupinge kwa hoja
 
Msanii,
Hakika.
Staili yangu inafahamika na wengi na nashukuru kuwa inapendwa.
Jf wajitahidi warudishe jukwaa la dini mzee wangu huku kwingine naona unapwaya unakosa pa kupumulia udini udini
 
Mageuzi ya sasa ni ya KATIBA mpya hakuna kingine... mwanasiasa yeyote anayeitakia mapenzi mema Tanzania ijayo atapigania KATIBA MPYA.

RIP Mrema, RIP Seif Sharif HAMAD, RIP Mtikila... Ingawa dakika za mwisho Mh. Mrema ukitembea mwendo wa mateka ukajisalimisha kundini....anyway sisi Tunasonga mbele hadi KATIBA MPYA itakapopatikana.
 
Amesema yeye ndo mtindo wake wa uandishi. Lakini huku Ni kufeli kabisa kwa mzee huyu katika swala la fani na maudhui. Sijamwelewa.
Sela...
Watu lazima tutofautiane.

Pengine katika yote na wote niliowataja katika makala hujui historia zao.

Pengine humjui Cassius wala Mohamed Mlamali Adam hata Mzee Sampati.

Pengine hujapata hata siku moja kusikia historia ya Colossus of Rhodes.

Ikiwa hivyo vipi utanielewa?
Ingia Google.
 
Back
Top Bottom