Tabia hizi za wageni zinakera

Tabia hizi za wageni zinakera

Na ni wasaa muafaka wa kujua tabia za jamii ingine.Mimi sikuwahi kufikiri kwamba kuazima charger ni kosa la kumuudhi mwenyeji wangu mpaka nilipouona uzi huu.
Simu ya mwenyeji wako ikizima shauri ya chaja uliyoazima ili tu utoe pevu jf unapoteza deal za mwenyeji wako , ambaye ana kupatia mahitaji yako kwake, haihitaji degree ya chuo kikuu ili utambue hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine tukipiga masanga tunaporudi nyumbani lazima tyimbe nyimbo za kikwetu kwa sauti na shati begani,kifua wazi.Sasa,kwa hii namna ya mleta uzi lazima atanikoyonga makofi.Ndipo vita ya tatu ya dunia itazuka.Nyumba za wageni zidumu!
Hahahhahahaaha!!!

***Mbire mwene Nyamwonyo***
 
hahahaha.
Hakuna mtu ambaye hajawahi kuwa mgeni na kama bado lazima siku moja utakuwa ugenini, kuna vijitabia ambavyo vinaweza kuwa kero kwa wenyeji wako bila ya wewe kujua.

Binafsi sipendi mgeni anayenitembelea ana simu lakini hana chaja, hivyo ratiba ya kuchaji simu yake inaingiliana na mimi mwenyeji huku akitoa visababu visivyoeleweka vya kwanini hana chaja.

Hebu turushie vitabia vya wageni vinavyokera ili tujirekebishe tukiwa ugenini.

Uzi huo leta sindano tuwashone

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukitaka kusafiri fanya yafuatayo
1. panga aina ya usafiri utakaotumia (usafiri binafsi, wa pamoja)
2. hakikisha una vitu muhimu kwa safari na sehemu unakofikia mfano taulo, shuka, power bank, charger na simu ndogo kwa ajili ya dharura, dawa ya meno na mswaki.
3. panga sehemu ya kufikia. kama unafikia kwa mtu hakikisha una mahali pa kufikia bila kusababisha usumbufu. kama ni geto la kuunga bora ujue mapema msije kuonana wabaya. kama ni guest hakikisha
4. panga bajeti ya safari inayohusisha nauli, bili ya guest, nauli za mizunguko na gharama za vyakula na pesa ya dharula. kwenye makadirio ya gharama weka makadirio ya juu kwa mfano nauli ni 35,000/= tenga 40,000/=. kama guest ni 15,000/= tenga 20,000/=
5. kama unaenda kufikia kwa ndugu hakikisha unabeba na vitu kama mchele, matunda au chochote kupunguza ukali wa maisha huko unakoenda.
ukizingatia haya huwezi kukutwa na anachokisema mtoa mada
 
ukitaka kusafiri fanya yafuatayo
1. panga aina ya usafiri utakaotumia (usafiri binafsi, wa pamoja)
2. hakikisha una vitu muhimu kwa safari na sehemu unakofikia mfano taulo, shuka, power bank, charger na simu ndogo kwa ajili ya dharura, dawa ya meno na mswaki.
3. panga sehemu ya kufikia. kama unafikia kwa mtu hakikisha una mahali pa kufikia bila kusababisha usumbufu. kama ni geto la kuunga bora ujue mapema msije kuonana wabaya. kama ni guest hakikisha
4. panga bajeti ya safari inayohusisha nauli, bili ya guest, nauli za mizunguko na gharama za vyakula na pesa ya dharula. kwenye makadirio ya gharama weka makadirio ya juu kwa mfano nauli ni 35,000/= tenga 40,000/=. kama guest ni 15,000/= tenga 20,000/=
5. kama unaenda kufikia kwa ndugu hakikisha unabeba na vitu kama mchele, matunda au chochote kupunguza ukali wa maisha huko unakoenda.
ukizingatia haya huwezi kukutwa na anachokisema mtoa mada
Hayo yote ntazingatia lakini kwa watu jamii ya mleta uzi asahau kupata mgeni sampuli yangu.Hata hivyo nilichokimaizi kwa hawa wakuu,wachoyo wa chaja pini bapa,ni hali ya uchumi tu inawafanya wanakuwa na hasirahasira kwa vitu vidogovidogo tu.Mungu awapunguzie adhabu ya kaburi.Amina!
 
Kama wewe ni ke wewe uu mchoyo wa kila kitu si ajabu hata umeme wa kuchagia unaumwa roha.. na ukiolewa wewe hakuna upande wa kiumeni atakuja kwako................

Kama wewe ni me ni shida zaidi wanaume hawana huu uchoyo wa SG
 
Huyo huyo mgeni anaisunda kwenye mizigo yake hio chaji na kuondoka nayo akiwa njian utaona sms oooh samahani nimejisahau nikaondoka na chaji hapo ni mkazi wa mikoa mitatu toka ulipo
Uko sahihi kabisa mkuu, ni kwa vile makekengeza ya wengi wanaamini ugeni ni hadi mtu aende nyumba ya mtu mwingine, mwenyeji wako "host" mnaweza kukutana hata njiani tu, maelezo yako yakakufanya mgeni na mwengine akawa mwenyeji, mfano mimi binafsi siku moja nilikuwa nimepaki gari karibu na kituo cha polisi, wakaja vijana wawili wana pikipiki tairi la nyuma limejam halizunguki wanakokota pikipiki yao kwa kuinua tairi la nyuma yaelekea ufunguo ulipote kituoni ama shida nyingine ya kiufundi , sijui. wakaomba pamoja na watu wengine waliokuwa pale mwenye plaiz awasaidie, kwakuwa nilikuwa nayo sikuona sababu ya kuwanyima, niliwapa cha ajabu walipomaliza kazi yao na ile plaiz waliondoka nayo, pale si kwamba wote wawili walijisau, ndivyo baadhi yetu tulivyo, ni njiani pale ila mimi nilikuwa mwenyeji wao na wao walikuwa wageni wangu na mwisho wa siku walinitenda tuliangalie hii issue kwa mapana hayo tutaelewana taratibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mm km mgeni kinaniwazisha kuamka asubuhi na mapema ikiwa sijazoea


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hakuna mtu ambaye hajawahi kuwa mgeni na kama bado lazima siku moja utakuwa ugenini, kuna vijitabia ambavyo vinaweza kuwa kero kwa wenyeji wako bila ya wewe kujua.

Binafsi sipendi mgeni anayenitembelea ana simu lakini hana chaja, hivyo ratiba ya kuchaji simu yake inaingiliana na mimi mwenyeji huku akitoa visababu visivyoeleweka vya kwanini hana chaja.

Hebu turushie vitabia vya wageni vinavyokera ili tujirekebishe tukiwa ugenini.

Uzi huo leta sindano tuwashone

Sent using Jamii Forums mobile app
Roho mbaya inakusumbua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa wasiojua na wenye roho ngumu mkae mkijua mgeni asipofika kwako itabidi ujiulize sana kwa sisi wasukuma mpaka unajiuliza kwanini sipati wageni maana mgeni ni baraka kwako anapofika kwako ni baraka tosha kabisa tubadilike

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha kama mimi chaliangu,naudhikaga kinyama alaf hana shuka anachukua yakwako daah!!
Hahahah!!! Huwa nawaombea kambi kwingine, nasogeza manzi fasta ili nipate kisingizio

***Mbire mwene Nyamwonyo***
 
Sipendi wageni vidume kulala ghetto kwangu, maana sina vitanda viwili. Kulala ndume mbili kwa bed moja ni tizi sana. Labda awe ndugu yangu wa damu na alale ukutani huko.
***Mbire mwene Nyamwonyo***
Hahaha kama mimi chaliangu,naudhikaga kinyama alaf hana shuka anachukua yakwako daah!!
 
Huyo huyo mgeni anaisunda kwenye mizigo yake hio chaji na kuondoka nayo akiwa njian utaona sms oooh samahani nimejisahau nikaondoka na chaji hapo ni mkazi wa mikoa mitatu toka ulipo
Halafu ukienda nunua nyingine ukianza kucharge masaa 6 ndiyo simu inajaa [emoji23] [emoji23] [emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom