Tabia ya kuvuna mawingu huenda ndiyo imesababisha mafuriko ya Dubai

Tabia ya kuvuna mawingu huenda ndiyo imesababisha mafuriko ya Dubai

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Nchi ya UAE inayounganisha na jimbo la Dubai ni miongoni mwa mataifa tajiri sana duniani.Kila kitu wamependelea kiende kiteknolojia hata pasipokuwa na umuhimu wa namna hiyo.

Maendeleo hayo ndiyo yamewafanya wasiweze kusubiri mvua zinyeshe kwa hiyari yake japo hawana shida sana ya maji wala upungufu wa chakula.

Kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1990 nchi hiyo ndipo ilipoanza tabia ya kuvuna mawingu ambayo yamekaribia kutunga mvua.

Ndege zenye madawa hurushwa angani na kwenda kuyarushia makombora yenye dawa mawingu hayo ambapo haraka huunda mvua na kunyesha eneo wanalotaka.

Mfumo huo wa kuvuna mawingu umewahi kutumika sana kwenye nchi ambazo hazimjui Mungu vyema kama vile Marekani na kwengineko.

Taarifa za wafuatiliaji wa nyenendo za ndege wamesema waliziona ndege mbili za kazi hiyo zikiruka siku za Jumatatu na Jumanne kuelekea kwenye mawingu ikiwa ni siku moja tu kabla ya mafuriko ya ghafla yaliyoikumba nchi hiyo.

Wahusika wa idara ya hali ya hewa walipofuatwa kuulizwa kuhusu zoezi hilo walikataa kuzungumza na waandishi wa habari.

Mafuriko hayo yamepelekea barabara kuu za jjji la Dubai na miji jirani kufungwa baada ya kugeuka kama mito.Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dubai kwa upande wake uligeuka kama ziwa kubwa kama maziwa ya nchi za kiafrika.

Misafara ya ndege kwenye uwanja huo imesitishwa kwa muda na kupelekea zahma ambayo haijawahi kutokea .Tayari watu kadhaa wameripotiwa kufariki katika nchi hiyo na nchi jirani ya Oman.

Gulf flooding: Dubai airport chaos as UAE and Oman reel from deadly storms

 
Sayansi ni ujuzi ambao mwanadamu amepewa na Mungu mwenyewe hivyo taifa lililo mbele kisayansi ni taifa ambalo lina baraka ya Mungu na mtu hawezi akatudanganya tuamini kinyume chake. Never.
Ndio maana mna fi..wa nyama wewe
 
Hilo ni Janga kama majanga mengine tu hakuna uspesho wowote kusema kwamba Mungu amehusika
 
Hilo ni Janga kama majanga mengine tu hakuna uspesho wowote kusema kwamba Mungu amehusika
Mambo ya kuyafuata mawingu kulazimisha mvua inyeshe naona kama ni utovu wa nidhamu kwa Mungu
 
Nchi ya UAE inayounganisha na jimbo la Dubai ni miongoni mwa mataifa tajiri sana duniani.Kila kitu wamependelea kiende kiteknolojia hata pasipokuwa na umuhimu wa namna hiyo.

Maendeleo hayo ndiyo yamewafanya wasiweze kusubiri mvua zinyeshe kwa hiyari yake japo hawana shida sana ya maji wala upungufu wa chakula.

Kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1990 nchi hiyo ndipo ilipoanza tabia ya kuvuna mawingu ambayo yamekaribia kutunga mvua.

Ndege zenye madawa hurushwa angani na kwenda kuyarushia makombora yenye dawa mawingu hayo ambapo haraka huunda mvua na kunyesha eneo wanalotaka.

Mfumo huo wa kuvuna mawingu umewahi kutumika sana kwenye nchi ambazo hazimjui Mungu vyema kama vile Marekani na kwengineko.

Taarifa za wafuatiliaji wa nyenendo za ndege wamesema waliziona ndege mbili za kazi hiyo zikiruka siku za Jumatatu na Jumanne kuelekea kwenye mawingu ikiwa ni siku moja tu kabla ya mafuriko ya ghafla yaliyoikumba nchi hiyo.

Wahusika wa idara ya hali ya hewa walipofuatwa kuulizwa kuhusu zoezi hilo walikataa kuzungumza na waandishi wa habari.

Mafuriko hayo yamepelekea barabara kuu za jjji la Dubai na miji jirani kufungwa baada ya kugeuka kama mito.Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dubai kwa upande wake uligeuka kama ziwa kubwa kama maziwa ya nchi za kiafrika.

Misafara ya ndege kwenye uwanja huo imesitishwa kwa muda na kupelekea zahma ambayo haijawahi kutokea .Tayari watu kadhaa wameripotiwa kufariki katika nchi hiyo na nchi jirani ya Oman.

Gulf flooding: Dubai airport chaos as UAE and Oman reel from deadly storms


Na kule Khazan urusi napo ni kuvuna mawingu chief.
 
Na kule Khazan urusi napo ni kuvuna mawingu chief.
Rufiji na Urusi hata utabiri wa hali ya hewa na mazingira ni kuwa mvua ingenyesha na ndio maana imejaza mito na mabwawa.
UAE kaenda kuchokoza mawingu ili mvua inyeshe kwa lazima.Tatizo liko hapo na ukitumia akili utaona.
 
Kumbuka barabara za Dubai hazina mitaro inayotiritisha maji baharini ukitembea Dubai hauwezi kuona mitaro
 
Rufiji na Urusi hata utabiri wa hali ya hewa na mazingira ni kuwa mvua ingenyesha na ndio maana imejaza mito na mabwawa.
UAE kaenda kuchokoza mawingu ili mvua inyeshe kwa lazima.Tatizo liko hapo na ukitumia akili utaona.
Una uhakika na unachosema kuhusu urusi au umevimbiwa njegere hapo tandale. Kwa taarifa yako Thailand hasa mji wa Bangkok hizo Mambo wanafanya sasa hiv ni miaka karibu 15. Nachojua hii ni climet changes. Dunia joto limekuwa jingi so barafu iliyopo northpole inayeyuka maji yanajaa so hali ya hewa haitabiriki. Ukienda maeneo ya Indonesia hasa huko Sumatra kila siku mvua maporomoko vimbunga na matetemeko.
 
Sayansi ni ujuzi ambao mwanadamu amepewa na Mungu mwenyewe hivyo taifa lililo mbele kisayansi ni taifa ambalo lina baraka ya Mungu na mtu hawezi akatudanganya tuamini kinyume chake. Never.
Taifa teule au sio
 
Sio kwamba Hayati Mwamba JPM aliwazuia kufanya feasibility study kabla ya mradi??!!
 
Una uhakika na unachosema kuhusu urusi au umevimbiwa njegere hapo tandale. Kwa taarifa yako Thailand hasa mji wa Bangkok hizo Mambo wanafanya sasa hiv ni miaka karibu 15. Nachojua hii ni climet changes. Dunia joto limekuwa jingi so barafu iliyopo northpole inayeyuka maji yanajaa so hali ya hewa haitabiriki. Ukienda maeneo ya Indonesia hasa huko Sumatra kila siku mvua maporomoko vimbunga na matetemeko.
Ninachosema hata wananchi wa Dubai nao wamekuwa wakisema.
Vyombo vya habari kwa kujua hilo haraka wakawafuata watu wa hali ya hewa na wao wakagoma kujibu kuonesha shaka hizo za watu wanazijua.
Kubwa zaidi kuna mambo yanafanywa na watu wasiomjua Mungu na yakawa na athari tofauti yanapofanywa na wale wanaomjua.
 
Ninachosema hata wananchi wa Dubai nao wamekuwa wakisema.
Vyombo vya habari kwa kujua hilo haraka wakawafuata watu wa hali ya hewa na wao wakagoma kujibu kuonesha shaka hizo za watu wanazijua.
Kubwa zaidi kuna mambo yanafanywa na watu wasiomjua Mungu na yakawa na athari tofauti yanapofanywa na wale wanaomjua.
Mbona unapenda kuongelea heresy mzee hunaga evidence support maelezo yako. Mwanach anajulia wapi mambo ya nchi hasa za kifalme zinazodhibiti kila kitu.
 
Mbona unapenda kuongelea heresy mzee hunaga evidence support maelezo yako. Mwanach anajulia wapi mambo ya nchi hasa za kifalme zinazodhibiti kila kitu.
Soma link niliyoweka utakuta ambacho nakisema,kwamba hiyo shaka ipo kwa watu wa huko kwamba ndege zinaruka kwenda kuyagonga mawingu na kwa hivyo mvua hiyo ni janga la kutengenezwa na watu.
Hearsay iko wapi hapo.
 
Soma link niliyoweka utakuta ambacho nakisema,kwamba hiyo shaka ipo kwa watu wa huko kwamba ndege zinaruka kwenda kuyagonga mawingu.
Hearsay iko wapi hapo.
Watu wanasema. Unakuwa kama wale watz kipind cha Kikwete walikuwa kila ukiona jengo zuri ni la Rizwan. Maneno hata mlevi anayo nilitaka official mzee
 
Watu wanasema. Unakuwa kama wale watz kipind cha Kikwete walikuwa kila ukiona jengo zuri ni la Rizwan. Maneno hata mlevi anayo nilitaka official mzee
Hatuzungumzii kwamba yanayosemwa ni kweli au uongo.
Muhimu nimekujibu kwamba hayo maneno sijayatunga mimi yako huko huko Dubai.Yanaweza yakawa kweli au Uongo.
Na hata Rizwan walivyosema watu si kwamba ilikuwa ni uongo wote.Kuna sehemu walipatia.
 
Back
Top Bottom