Tabia ya Magari ya Mwendokasi hasa Kimara Mwisho hadi Kibaha kutotaja majina ya vituo njiani ni kero kubwa

Tabia ya Magari ya Mwendokasi hasa Kimara Mwisho hadi Kibaha kutotaja majina ya vituo njiani ni kero kubwa

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Nina malalamiko kuhusu magari ya Mwendokasi, nina mambo mawili, la kwanza ni kuhusu kutotajwa kwa majina ya vituo, tabia hii ilianza mdogomdogo na hatimaye imekuwa kawaida.

Ni kama vile wanaamini kila anayepanda Mwendokasi basi anajua vituo na anaijua Dar vizuri.

Katika vituo vya hatikati ya Mji japo hawataji lakini mtu unaweza kuchungulia kituo ambacho gari inaelekea ukasoma na ukatambua umefika wapi.

Changamoto ni kutoka Kimara Mwisho kwenda Mbezi, Mloganzila na Kibaha, hapo kati hakuna anayetaja kituo, inabidi ujiongeze mwenyewe kwa kuuliza watu au kama unapajua basi uchungulie nje.

Kama makonda kwenye daladala za kawaida wanataja majina ya vituo kila siku, inakuwaje Mwendokasi inashindikana? AU ndio ile kuchukuliana poa kwa kuwa wanajua lazima watu watapanda tu huo usafiri? Nimeshuhudia watu kibao wakipitiliza vituo na kulazimima ufanya mchakato wa kurudi walipotakiwa kushuka.

Jambo la pili
Juzi nilimepata changamoto wakati nataka kusafiri, nilikata tiketi ya online kutokea Kituo cha Kimara Stop Over kuelekea Kibaha.

Nikashushwa kwenye gari na madreva wawili kwa madai kuwa hawaamini kama tiketi imekuwa scanned lakini pia kuna mmoja akasema kabisa kwamba hakuna scanner katika vitu vya katikati na hawawezi kunipakia kwa sababu nitasafiri bure.

Yaani nimebaki nimeshangaa, kwanza magari ni machache ya kwedna Kibaha ila hao madereva ndio walinichosha kabisa ikabidi nibadilishe usafiri ili niwahi kibaruni.

Kama vituo vingine vinasumbua ni bora wakasema kabisa kwamba tusilipie online.
 
Huu mradi utakufa siku yoyote , unaendeshwa kienyeji mno !
 
Mnaongeaga pointi ila mnakosea kulenga shabaha. Hii ni nchi yenye mipaka yake kimataifa. Ungesema iwe koloni hapo ungeeleweka. Kuwa jimbo ina maana isiwe nchi huru, mind kuwa haiko jirani na marekani kama canada na mexico ambazo ni rahisi kuvunja mipaka
 
Hivi zile tv zinazoonesha kituo kinachofuata ni kwamba zimekufa kwa sasa mwendokasi hizo ukishapanda mida ya usiku kama ni mgenj unaweza kupitiliza kituo au kushuka nyuma ya kituo
 
Mabasi ya mwendokasi tumeshindwa kuyasimamia wenyewe halafu tunajimwambafy kuweza kuendesha bandari... hatuko serious.
 
watu wana sensor puani, kila atakaefika kituo chake cha kushuka anastuka hata kama alikuwa anasinzia.., hizo sensor zinauzwa
 
Nina malalamiko kuhusu magari ya Mwendokasi, nina mambo mawili, la kwanza ni kuhusu kutotajwa kwa majina ya vituo, tabia hii ilianza mdogomdogo na hatimaye imekuwa kawaida.

Ni kama vile wanaamini kila anayepanda Mwendokasi basi anajua vituo na anaijua Dar vizuri.

Katika vituo vya hatikati ya Mji japo hawataji lakini mtu unaweza kuchungulia kituo ambacho gari inaelekea ukasoma na ukatambua umefika wapi.

Changamoto ni kutoka Kimara Mwisho kwenda Mbezi, Mloganzila na Kibaha, hapo kati hakuna anayetaja kituo, inabidi ujiongeze mwenyewe kwa kuuliza watu au kama unapajua basi uchungulie nje.

Kama makonda kwenye daladala za kawaida wanataja majina ya vituo kila siku, inakuwaje Mwendokasi inashindikana? AU ndio ile kuchukuliana poa kwa kuwa wanajua lazima watu watapanda tu huo usafiri? Nimeshuhudia watu kibao wakipitiliza vituo na kulazimima ufanya mchakato wa kurudi walipotakiwa kushuka.

Jambo la pili
Juzi nilimepata changamoto wakati nataka kusafiri, nilikata tiketi ya online kutokea Kituo cha Kimara Stop Over kuelekea Kibaha.

Nikashushwa kwenye gari na madreva wawili kwa madai kuwa hawaamini kama tiketi imekuwa scanned lakini pia kuna mmoja akasema kabisa kwamba hakuna scanner katika vitu vya katikati na hawawezi kunipakia kwa sababu nitasafiri bure.

Yaani nimebaki nimeshangaa, kwanza magari ni machache ya kwedna Kibaha ila hao madereva ndio walinichosha kabisa ikabidi nibadilishe usafiri ili niwahi kibaruni.

Kama vituo vingine vinasumbua ni bora wakasema kabisa kwamba tusilipie online.
Uliza jirani yako kituo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Huu mradi ulianza vizr tu, labda magari yalikuwa mapya screen ndani ya basi zinasoma na kutangaza vituo. Wanajaribu kupanua huduma kwa kuongeza ruti bila kuzingatia namna ya kuboresha huduma yenyewe
 
Hivi zile tv zinazoonesha kituo kinachofuata ni kwamba zimekufa kwa sasa mwendokasi hizo ukishapanda mida ya usiku kama ni mgenj unaweza kupitiliza kituo au kushuka nyuma ya kituo
Mfumo ushakufa

Kengele zishakufa

Ac ndiyo [emoji1]

Huu usafiri ni kwa ajili ya wajng malof

Tu akina sisi [emoji1]

Ova
 
Mabasi ya mwendokasi tumeshindwa kuyasimamia wenyewe halafu tunajimwambafy kuweza kuendesha bandari... hatuko serious.
Mtanzania sahv anachoweza ni udaku,kukatika na kucheza singeli amapiano tu,starehe kwishney

Ova
 
Back
Top Bottom