unahangaika nini ndugu yangu......... muache tu akikua ataacha............
unachanganya mambo mawili hapo.............. kukua kimwili na kukua kiakili............... huo umri wa miaka minane ni umri wa mwili na kutokana na maelezo yako inaonekana umri wa akili yake uko nyuma kidogo ya miaka minane............... hapo ndipo wazazi wengi hukosa hekima........... sio lazima akili na mwili vikue pamoja........ kuna watoto amabo akili iko mbele ya umri a wengine umri uko mbele ya akili. huyu wako naona mwili ndio uko mbele ya akili kwa makuzi............... jaribu kutathmini na matendo mengine ayafanyayo kama michezo, uhusiano na watoto wengine, nyimbo aazoimba, tabia ake wakati wa chakula nk...... utagundua kuwa ana tabia ambaz watoto wengine wa miaka 8 walisha ziacha.......... ushauri wangu:
1. endelea kumsoma. inaonekana hata wewe hujamjua vizuri na kama utaendelea kumhukumu kabla hujamjua sawasawa utamuathiri kisaikolojia
2. wakati unapoendelea kumsoma usimchukulie hatua ambazo ni harsh kama hizo ulizoshauriwa za kutumia pilipili, au viboko kama ulivyosema umewahi kumchapa............ ulifanya makosa, acha. unaweza hata kumfanya akuogope, kukuchukia, au hata akajiona hapendeki... ni hatari kwa saikolojia yake
3. jitahidi kusisitiza shule na uhakikishe anapata elimu bora
4. jitahidi kuzumgumza naye mara kwa mara na hasa mambo mbalimbali ya maisha kwa mfano hadithi za kidini kuhusu watu maarufu katika dini yako kutoka katika biblia kama hutojali
5. nk.
kwa kifupi, mwanao ni mzima hana tatizp lolote ila ukiendelea kumshughulikia bila busara wewe ndiye utakayemletea matatizo hasa ya kisaikolojia........................