Tabia ya Simba kukomalia mechi na Yanga ndiyo mana haiendelei

Tabia ya Simba kukomalia mechi na Yanga ndiyo mana haiendelei

Nimefurahishwa sana na maelezo yako mkuu!
Kama kweli wewe ni mwanasimba, tukipata viongozi kama wewe ktk vilabu vitano tu... (Ligi kuu) tutafika mbali, mfano mimi ni Yanga ila kwa mtazamo wako huu nikweli unafikra endelevu kwa simba na soka la tz kwa ujumla

mkuu ahsante. Nawaza ligi inaenda ukingoni na hakuna kitu kizuri kama kufanya biashara asubuh alaf jioni we unahesabu noti huku meno yote 32 yakiwa nje. Hii tabia yakuombeana mabaya flani afungwe au atoe droo ili nichukue ubingwe ni sawa na kumaliza biashara jioni na kushindwa kupiga mahesabu mapema.
 
As long as it works na mashabiki ndicho wanachopenda let them continue (kishabiki zaidi)...... kiujumla soka letu linahitaji kuzaliwa upya kuna uswahili mwingi
 
...si huwa mnasema bado mnajenga timu
 
Haieleweki hapa ni bandarini au mwalo wa kuvulia kambale?
 

Attachments

  • 1427049011251.jpg
    1427049011251.jpg
    56.2 KB · Views: 95
  • 1427049490830.jpg
    1427049490830.jpg
    21.6 KB · Views: 89
Ingekuwa kwenye ligi kuu unachagua timu ya kucheza nayo mimi ningekuwa naichagua yanga kila mechi. Saa hii tayari ningekuwa nimeshatangaza ubingwa, hizi timu nyingine zinanuka vikwapa mpaka wachezaji wangu wanashindwa kucheza kandanda lao.
 
Pole kaka,hamia huku Dar Young Africa hakuna uswahili oooh uwanja mbaya sijui nn ni magoli tu!..

Ni kweli huko hakuna uswahili kuna uhindi wa kutembeza noti ili makipa wa timu pinzani watoe zawadi na timu zinazokaza mechi nyingine zilegeze dakika 10 za mwisho...
 
Ni miaka zaidi ya mitatu timu yetu ya simba haijashiriki mashindano yeyote ya kimataifa. inaona kuifunga yanga pekee ndiyo imemaliza ligi kuu na kuchukua ubingwa. Matokeo ya leo kati ya yanga na mgambo yamedhihirisha kuwa hata mwaka huu simba haitacheza ligi ya mabingwa au ligi ya shirikisho. Simba tujitapange sana hii tabia ya kujiona na kusema bora tufungwe na timu yeyote lakini tusifungwe na yanga itatupelekea tusicheze ligi za kimataifa na kila mwaka tutaendelea kuishia ligi ya ndani tu.

Imeniuma sana
Mleta uzi waambie na yeboyebo waache kuachia achia kila wakikutana na Simba, wabane kama wanavyobana mbele ya Azam.
Mpaka imekuwa Simba anafikiri timu zote ni mbovu kama yeboyebo yanga bhana. Allaaaaaa
 
Mikia mnashida sana na ninyi tembezeni hizo pesa kama rahisi,mnajua kulala makaburini tu!

Ni kweli huko hakuna uswahili kuna uhindi wa kutembeza noti ili makipa wa timu pinzani watoe zawadi na timu zinazokaza mechi nyingine zilegeze dakika 10 za mwisho...
 
Ingekuwa kwenye ligi kuu unachagua timu ya kucheza nayo mimi ningekuwa naichagua yanga kila mechi. Saa hii tayari ningekuwa nimeshatangaza ubingwa, hizi timu nyingine zinanuka vikwapa mpaka wachezaji wangu wanashindwa kucheza kandanda lao.

umeona ee,halafu wakipata ushindi wa kubahatisha wanamaneno mengi kama waimba taarabu.
 
Back
Top Bottom