Tabia ya Watanzania kupenda michango

Tabia ya Watanzania kupenda michango

Setting ikoje hiyo nami nifanye? Yani juzi kuna mtu nimempa namba kesho yake tayariii nipo group sijui jumuiya ya mtakatifu gani tayari anaomba michango nikabaki...,[emoji15]
Yaan sasa hivi namba za simu ni fursa...mtoto wa ukoo wa mbali utashangaa kakuunga kwenye group kume mwezi ujao anaoa[emoji848]
 
Hii ni legacy ya Nyerere na sera zake za ujamaa

If we could go back in time ningetamani Kambona afanikiwe kupindua serikali ya Nyerere na kuintroduce capitalism from the 60s. Hii mentality ya kuombaonba hovyo kila ukiwa na shida isingekwepo.

Kila mtu aishi kwa uwezo wake, kila mbuzi ashibe kwa urefu wa kamba yake.

Wewe ni mpumbavu
 
Kiukweli hii michango ya sherehe inakera si kidogo, sasa unakaa unajiuliza huyu/hawa wameshtukizwa kufanya sijui send off sijui harusi? Maana kama umepanga kuoa/kuolewa hakuna haja ya kusumbua watu, angalia watu wako wa karibu + ndugu zako.....tena wamekuja na kautaratibu ka kuanzia 70 single laki double, jamani.....Yaani tupambane kuweka akiba bado tupambane na kusherehesha watu.

Halafu michango inakuwa kama deni vile, unawindwa hupumui.

Si lazima ujaze liukumbi, angalia idadi ya watu unaoweza kuafford chakula na vinywaji ....Wao wakija watakuja na zawadi...Ila budget iwe jukumu lako.
Watu 20 - 25 mbona sherehe inanoga tu.

Ugonjwa na misiba sawa.
 
Tunatakiwa tuanze kukataa kwa kutochanga. Yaani hata ukumbuni huwa sioni cha maana zaidi ya makelele ya maspika na mbwembwe za ma MC,yaani kwa kweli huwa sioni cha maana kinachofanyika
Kimasihala masihala milioni 30 zimetumika.
 
hivi na hii michango ya kuvhangia sijui majengo ya mashule, hospitals e.t.c ni kwa sheria ya wapi???
 
Hii ni legacy ya Nyerere na sera zake za ujamaa

If we could go back in time ningetamani Kambona afanikiwe kupindua serikali ya Nyerere na kuintroduce capitalism from the 60s. Hii mentality ya kuombaonba hovyo kila ukiwa na shida isingekwepo.

Kila mtu aishi kwa uwezo wake, kila mbuzi ashibe kwa urefu wa kamba yake.
Umezaliwa lini? Mbona wakati wa nyerere hakukuwa na michango mingi? Kwanza kipindi hicho vitu kama harusi vilikuwa simple sana na hakukuwa na vikao vingi. Mambo ya michango yameanza kushika kasi tangu watu wajue kitu kinachoitwa ''whatsup''. Whatsup imerahisisha kuweka watu kwenye ma-group na kuombana michango kwa vitu hata vya kijinga. Njia moja kubwa ni kujitoa kwenye hayo ma-group na kubakiwa na yale unayoona yana umuhimu.
 
Kama una mgonjwa anayehitaji fedha nyingi kwa ajili ya matibabu ntachangia,kama umekwama ada ntakuchangia,kama umepata msiba wa karibu ntakueezesha kidogo,ila kama ni harusi,kipaimara,graduation,birthday party,au sherehe nyingine yoyote ya anasa sitakuchangia!! Sitoi hata mia!
Hii ndiyo dawa. Na siku hizi wanawake wa uswazi wanajifanya kuwa wazungu kuliko hata wazungu wenyewe. Wengi hawajaenda shule hivyo wanakuwa rahisi sana kuingia kwenye mkumbo. Kitu kama birthday uswahilini imekuwa kama ni lazima. Kuna mama mmoja darasa la saba ukimsikia anavyozitamka sasa. Utasikia ''nilikuwa kwenye basi-dei ya jirani yangu''. Wamejua mpaka baby shower wewe unafikiria mchezo. Kweli ukitaka kujua gharama za ujinga nenda uswahilini huko uone kina mama wanavyoshindana na sherehe.
 
Tunatakiwa tuanze kukataa kwa kutochanga. Yaani hata ukumbuni huwa sioni cha maana zaidi ya makelele ya maspika na mbwembwe za ma MC,yaani kwa kweli huwa sioni cha maana kinachofanyika
Ni utopolo mtupu na kupotezeana muda na pesa.
 
Habari wadau,

Leo nimepata muda kujiuliza hivi hii tabia ya Watanzania (walio wengi) au jamii yetu kupenda sana tabia ya kuanzisha michango na kuchangia tumeipata wapi? Au ni ile toka enzi za siasa za ujamaa na kujitegemea?

Sipingi kuchangia mambo muhimu, ni jambo jema sana kuchangia mambo muhimu ya maendeleo.

Lakini hivi sasa tabia hii imezidi kwa kweli. Najua kuchangia si lazima ni hiari Lakini imekuwa too much!

Kila group la whatsup likianzishwa, wiki ya kwanza ya pili mchango. Wanasiasa kitu kidogo, wananchi tunaomba mchangie kidogo. Tabia hii mpka serikali kupitia viongozi wake, wanahamasisha michango, huku wakizitafuna kodi bila kujali.

Leo mtu anafungua kesi mahakamani ambayo haina gharama zozote zaidi anahamasisha umma umchangie.

Nina magroup ya whatsup takribani Matano baada ya kuyapunguza sana, lakini bado nikimaliza mchango huu, group lile linaleta michango miwili au zaidi. Matatizo ni yale yale.

Tupunguze haya mambo jamani.
Nimeachana na ujinga wa kujipa umaskini, nachangia kwenye mambo ya msingi kama majanga
 
Katika vitu siviruhusu Ni kupelekeshwa pasipo hiari ya maamuzi yangu (isipokuwa mume tu), kama mtu sitaki kumchangia napiga kimya, Sina group na kwa misimamo yangu sijui mtu kuniunga group bila kunijulisha anakuwa amejiamini nini,

Maisha raha sana ukipuuza kero ndogo ndogo
 
Habari wadau,

Leo nimepata muda kujiuliza hivi hii tabia ya Watanzania (walio wengi) au jamii yetu kupenda sana tabia ya kuanzisha michango na kuchangia tumeipata wapi? Au ni ile toka enzi za siasa za ujamaa na kujitegemea?

Sipingi kuchangia mambo muhimu, ni jambo jema sana kuchangia mambo muhimu ya maendeleo.

Lakini hivi sasa tabia hii imezidi kwa kweli. Najua kuchangia si lazima ni hiari Lakini imekuwa too much!

Kila group la whatsup likianzishwa, wiki ya kwanza ya pili mchango. Wanasiasa kitu kidogo, wananchi tunaomba mchangie kidogo. Tabia hii mpka serikali kupitia viongozi wake, wanahamasisha michango, huku wakizitafuna kodi bila kujali.

Leo mtu anafungua kesi mahakamani ambayo haina gharama zozote zaidi anahamasisha umma umchangie.

Nina magroup ya whatsup takribani Matano baada ya kuyapunguza sana, lakini bado nikimaliza mchango huu, group lile linaleta michango miwili au zaidi. Matatizo ni yale yale.

Tupunguze haya mambo jamani.
Harusi ni mzigo kwa wengine.hasa wale ambao hawachangagi kabisa kwa wenzao wao wanajua kudai hadi kero

Halafu,utakuta kuna gharama za kijinga zinazoongeza mzigo ,mfano ,wewe mwanaume unapewa kadi ya send off halafu mkeo anapewa kadi ya kitchen party.Haya mambo ya kitchen party ni ujinga mtupu.Yaani mtu mwingine ameshakaa na mume na kupata hadi wajukuu kabisa ,anaamua kubariki ndoa naye anataka afanyiwe kitchen party Huu ni ujinga plus
 
Back
Top Bottom