The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Mtoto mmoja anayekadiliwa kuwa na umri wa Miaka 15 Ally Amani mkazi wa kijiji cha Igoko ameuawa na kufukiwa porini na watu wasiojulikana kando ya barabara ya Nzega kuelekea Tabora katika kijiji cha Igoko Kata ya Isikizya Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora.
Mwili huo umepatikana Alhamisi January 16 majira ya saa mbili Usiku.
Kwa mujibu wa Familia ya Mtoto Ally Amani mtoto huyo alipotea Jumatano January 15 majira ya Saa 1 jioni alipoenda Kijiji cha Usagari Wilaya ya Nzega na hakuonekana hadi hapo mwili wake ulipokutwa umefukiwa porini.
Jeshi la polisi wilaya ya Uyui lilifika kwenye eneo la tukio na kuufukuwa mwili wa mtoto kisha baada ya taratibu za kidaktari wameruhusu mwili huo kuzikwa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Igoko Mlezi Jumanne amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amewasihi wananchi kuacha vitendo kama hivyo.
T
Mwili huo umepatikana Alhamisi January 16 majira ya saa mbili Usiku.
Kwa mujibu wa Familia ya Mtoto Ally Amani mtoto huyo alipotea Jumatano January 15 majira ya Saa 1 jioni alipoenda Kijiji cha Usagari Wilaya ya Nzega na hakuonekana hadi hapo mwili wake ulipokutwa umefukiwa porini.
Jeshi la polisi wilaya ya Uyui lilifika kwenye eneo la tukio na kuufukuwa mwili wa mtoto kisha baada ya taratibu za kidaktari wameruhusu mwili huo kuzikwa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Igoko Mlezi Jumanne amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amewasihi wananchi kuacha vitendo kama hivyo.