Tabora pagumu kweli.

Wana JF naomba yeyote aliyeko mkoani TABORA anisaidie kutafuta kazi yoyote ile ya kufanya.HATA KAMA NI ULINZI.Elimu yangu ni form six.Nimechoka kunyanyaswa kisa sina kazi.Naomba niwasilishe mada!


:violin: Ndugu maisha makali sana kama unavyozungumza. Kama unataka kufanikiwa usirudi vijijini maana ndio utazidi ku-lost. Komaa hapohapo mjini kama unaweza mwambie huyo father mtata akupe company ununue kamashine ka tofali taratibu mfuko mmoja, miwili, mchanga unabeba wewe mwenyewe, unapiga tofali mwenyewe itafikia hulali njaa. La nunua mkokoteni wa kubebea maji utaanza na mmoja mara unaanza kuajiri mtu mara watu. Mwanzo mgumu. Tabora palikuwa na shida ya maji sasa unaweza take advantage. Ukitafuta kazi ya kuajiriwa utakuwa mtu wa kutumwa kila siku. Wabeja.
 
Wana JF naomba yeyote aliyeko mkoani TABORA anisaidie kutafuta kazi yoyote ile ya kufanya.HATA KAMA NI ULINZI.Elimu yangu ni form six.Nimechoka kunyanyaswa kisa sina kazi.Naomba niwasilishe mada!

changa nauli uje angalau kujaribu boksi unyamwezini.
 
Kila sehemu ni pamugu wala si Tabora tu, mimi nipo hapa jijini Dar na nakuambia amini usiamini usipochacharika lazima urudi kijijini, hali ni ngumu sana, nauli ya kwenda kibaruani juu, chakula juu, kodi ya nyumba juu, umeme juu, maji hayapatikani ni kununua kwa dumu sh. 250.

Nilitamani kulikimbia jiji kama wewe ila nikapiga akili nikaona kukimbia mji utoto, nikagangamala sasa hali kidogo afadhali. kama walivyokushauri wengine kaza msuri, kijana wa kiume ukifika miaka 18 hakuna kulialia - ushakua. Watakucheka watuu....
 
Wana JF naomba yeyote aliyeko mkoani TABORA anisaidie kutafuta kazi yoyote ile ya kufanya.HATA KAMA NI ULINZI.Elimu yangu ni form six.Nimechoka kunyanyaswa kisa sina kazi.Naomba niwasilishe mada!

sisi tuna project ya kupasua mbao za mininga kule sehemu za Inyonga, pia tunavua samaki bwawa la koga na kuvuna asali. Kama wewe si mwenyeji Fuata maelekezo haya ili kufika tulipo.
Panda basi toka uliko hadi Tabora mjini
Nenda stend ya mabasi yaendayo Sikonge hadi kijiji kinaitwa Ipole
Hapa tutakutafutia baskeli ya Kukodi hadi Koga km kama 60 hivi ambako utaungana na vijana wenzako takribani kumi hivi katika hii project.

Ujira ni kutokana na juhudi yako lakini unaweza pata hadi 5,000 kwa siku, na baada ya kuuza mzigo wafanyakazi wote mtapata 10% ya mapato yote then mnagawana. Chakula na malazi kampuni yetu inatoa bure (Mnaishi kambini).

PM, kwa maelekezo zaidi - Changamka, Mtaji unao (Nguvu na Ujana) hakuna haya ya kulialia, kuzaliwa mwanaume....

Fanya kazi kwa mwaka mmoja au miwili then pesa zako zitakusaidia kama unataka kusoma zaidi.
 
Reactions: Aza
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…