Tabora yarudisha chenji ya Mil. 300 hazina

Tabora yarudisha chenji ya Mil. 300 hazina

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
302
MKOA wa Tabora umerudisha hazina Sh 326,192,517 walizopaswa kulipwa walimu wa Shule za Msingi baada ya kubainika kiasi hicho cha fedha kilizidi ikilinganishwa na madai yao halali. Madai ya walimu hao yalikuwa Sh 1,167,856,406 lakini baada ya kuhakikiwa yalionekana halali kulipwa ni Sh 841,662,889 hivyo fedha zilizobaki zimerudishwa hazina.

My take
Tukio hili ni kuonyesha uaminifu au kujipendekeza,
au wameogopa PCCB wangezifisadi wangejulikana,
au mgao haukueleweka mtu akamwaga unga,
Kama wamezirudisha hazina ina maana Tabora hakuna madai zaidi ya malimbikizo ya mishahara ya walimu
Nani alizidisha madai hayo na je kaadhibiwa?
Je hazina imeridhika kurudishiwa? kama wameridhika kabla ya kuzitoa ilijiridhisha kuwa hakukuwa na udanganyifu wa madai?

Mimi huwa najiuliza kwani tunapozungumzia utawala bora ni nini hasa ni kuona mtu anahubiri utawala bora au kuona matendo, je matukio kama haya yanahusika au hayahusiki na utawala bora elewa huu ni mkoa mmoja tu ambao angalau wamediliki.
Mwisho napenda kuuliza hapa mzembe ni nani aliyepeleka hazina idadi zaidi ya mahitaji au hazina iliyotoa pesa bila kuhakiki.
Ni tukio moja tu lakini tukijibu maswali hapo juu itawakilisha jinsi mali ya umma inavyotumika bila uangalifu, na ukiangalia kwa juu juu utasema kuna tatizo gani wakati pesa imerudi ilikotoka?
 
Madiwani wote wa Tabora wanatakiwa kufutwa kazi mwezi wa kumi kwa kutokuchaguliwa tena mkoa wenyewe uko nyuma kwa kila kitu si wangechimbia bwawa jipya la kuhifadhi maji manake lilopo lilichimbwa wakati wa mkoloni na maji hayatoshelizi katika mji wa tabora au wangenunua madeski kwenye shule zao au basi wanunua ambulance ,ziwasaidie wa mama wajawazito wanapotaka kujifungua badala ya kurudisha fedha hazina ambazo zitatumika kuwaongezea CCM kwenye harambee yao ,Kwanza mwenyekiti wa halmashauri ya Tabora ni nani anaruhusu chenzi zote hizo kurudi hazina kweli maskini ataishia kuwa maskini milele
 
Madiwani wote wa Tabora wanatakiwa kufutwa kazi mwezi wa kumi kwa kutokuchaguliwa tena mkoa wenyewe uko nyuma kwa kila kitu si wangechimbia bwawa jipya la kuhifadhi maji manake lilopo lilichimbwa wakati wa mkoloni na maji hayatoshelizi katika mji wa tabora au wangenunua madeski kwenye shule zao au basi wanunua ambulance ,ziwasaidie wa mama wajawazito wanapotaka kujifungua badala ya kurudisha fedha hazina ambazo zitatumika kuwaongezea CCM kwenye harambee yao ,Kwanza mwenyekiti wa halmashauri ya Tabora ni nani anaruhusu chenzi zote hizo kurudi hazina kweli maskini ataishia kuwa maskini milele


Mkuu waliomba hela za kulipa walimu, wamepewa; zimezidi wanatakiwa kurudisha. Is that simple....
 
Tabora yangu hii walimu wenyewe shule za msingi wa kuhesabu.
 
Habari hii haijakaa sawa madai ya walimu yalichukua muda mrefu kulipwa mpaka yalipohakikiwa hivyo basi pesa iliyopelekwa Tabora ilikua ni kiwango ambacho tayari kimehakikiwa inakuaje pesa zilizopelekwa ni zaid kuliko madai halisi lipo tatizo mahali fulani HAZINA. Serekali hii jamani kila mahali ni tatizo
 
Watanzania bwana
Sasa inaonekana kurudisha kisicho halali ni ujinga, teh teh teh teh.harafu hapo hapo unapiga dhidi ya ufisadi, na kubwata eti unataka viongozi wanaofuata sheria na kanuni teh teh.
 
MKOA wa Tabora umerudisha hazina Sh 326,192,517 walizopaswa kulipwa walimu wa Shule za Msingi baada ya kubainika kiasi hicho cha fedha kilizidi ikilinganishwa na madai yao halali. Madai ya walimu hao yalikuwa Sh 1,167,856,406 lakini baada ya kuhakikiwa yalionekana halali kulipwa ni Sh 841,662,889 hivyo fedha zilizobaki zimerudishwa hazina.

My take
Tukio hili ni kuonyesha uaminifu au kujipendekeza,
au wameogopa PCCB wangezifisadi wangejulikana,
au mgao haukueleweka mtu akamwaga unga,
Kama wamezirudisha hazina ina maana Tabora hakuna madai zaidi ya malimbikizo ya mishahara ya walimu
Nani alizidisha madai hayo na je kaadhibiwa?
Je hazina imeridhika kurudishiwa? kama wameridhika kabla ya kuzitoa ilijiridhisha kuwa hakukuwa na udanganyifu wa madai?

Mimi huwa najiuliza kwani tunapozungumzia utawala bora ni nini hasa ni kuona mtu anahubiri utawala bora au kuona matendo, je matukio kama haya yanahusika au hayahusiki na utawala bora elewa huu ni mkoa mmoja tu ambao angalau wamediliki.
Mwisho napenda kuuliza hapa mzembe ni nani aliyepeleka hazina idadi zaidi ya mahitaji au hazina iliyotoa pesa bila kuhakiki.
Ni tukio moja tu lakini tukijibu maswali hapo juu itawakilisha jinsi mali ya umma inavyotumika bila uangalifu, na ukiangalia kwa juu juu utasema kuna tatizo gani wakati pesa imerudi ilikotoka?

mkuu hata wangeema wameomba milioni moja ya kumalizia takweimu ungesema

nadhani sasa inatosha iwapo tutaishia kuwa stereotypes bila analytical skills etc

come again bro
 
Mkuu waliomba hela za kulipa walimu, wamepewa; zimezidi wanatakiwa kurudisha. Is that simple....

Mkuu, suala ni kwamba kwa nini zilizidishwa in the first place??!! Inavyotakiwa ni kwamba orodha iliyoomba pesa wizarani iwe sawa na ya malipo huko Tabora; na si vinginevyo.
 
Watanzania bwana
Sasa inaonekana kurudisha kisicho halali ni ujinga, teh teh teh teh.harafu hapo hapo unapiga dhidi ya ufisadi, na kubwata eti unataka viongozi wanaofuata sheria na kanuni teh teh.
Mwisho napenda kuuliza hapa mzembe ni nani aliyepeleka hazina idadi zaidi ya mahitaji au hazina iliyotoa pesa bila kuhakiki.
Ni tukio moja tu lakini tukijibu maswali hapo juu itawakilisha jinsi mali ya umma inavyotumika bila uangalifu, na ukiangalia kwa juu juu utasema kuna tatizo gani wakati pesa imerudi ilikotoka?
MkamaP ukisoma para yangu ya mwisho(red) niliitoa makusudi kwa sababu nilijua kuna watu wa type kama yako watahoji hicho unachohoji, tatizo si kurudisha kisicho halali tatizo ni kimepatikanaje nani amesababisha kiwe si halali?
 
Back
Top Bottom