Tafadhali anayeuelewa Utangazaji wa Samuel Nathaniel Sasali wa Clouds 360 anieleweshe

Tafadhali anayeuelewa Utangazaji wa Samuel Nathaniel Sasali wa Clouds 360 anieleweshe

Yule baby kabaya aliteuliwa mkuu?

Hakuteuliwa ila Yeye ndiyo alikuwa akila Bata kuliko hata wale Wote walioteuliwa kutokea hapo Kwao CMG Ndugu.

Na katika Watu ambao najua Msiba huu umewauma, umewachoma na kuwagusa hadi Kumoyo ni huyu Mtangazaji Babie Kabae.

Sitaki Maswali yenu ya Kwanini iwe Yeye?
 
Hana mzuto wa kukaa mbele ya kioo. Sijui ni utaratibu upi ulitumika kumpa kipindi cha TV? Huyu angekuwa anatangaza kwenye radio tusikie sauti. Nadhani ni moja ya zao kutoka misitu ya kongo na Kamerunj. Emolo.
 
Huyo Sasali hata kuongea kwake saingine hasikiki vizuri.

Kuna wakati nilikuwa nafuatilia Mafundisho ya yule mwana saikolojia akiwepo huyo Sasali na mwenzie Sasali akiongea sauti yake sijui ikoje haisikiki vizuri sijui ni aina ya besi au nini?!

Inabidi ajirekebishe.
 
Pamoja na Clouds Media (media category) kutokuwa kituo cha habari ila cha burudani kuna wakati wanajisahau sana tena sana.

Niliwahi kuandika sehemu, mojawapo ya usajili wa chombo cha habari hapa nchini unaendana na category unayopewa/omba Kulingana na hitaji lako au eneo unalotaka kuwekeza chombo chako.

Ukija upande wa hao jamaa, wao walikuja kama kituo cha burudani kwa sana na tokea mwanzo ukipiga picha utagundua walijazwa au kuajiliwa waongeaje wenye maneno mengi, utani nk haikuwa taaluma.

Hiyo imeendelea pale ndani kiasi kwamba hata kukiwa na jambo/habari ngumu wao wanaiweka kiburudani, ucheshi, utani nk ili kufikia hadhima ya usajili wao.

Kuna baadhi ya watangazaji wapo kikazi na wengine baada ya kuingia darasani ndiposa utawasikia 'wanajinasibu' kupitia mic "kama mwalimu alivyotufundisha" au utasikia "juzi class tuli tulipewa assignment flani"

👉🏾Tumsamehe tu huyo jamaa maana hajui alitendalo.
 
Pia yule mwana saikolojia akiongea wanamu interrupt mara kwa mara kwa kweli huwa ina boa sana na kuchosha kwanini wasimuache afundishe kwa muda wa kutosha bila kumu interrupt ?

Yawapasa kutafakali na kubadilika.
 
Back
Top Bottom