Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Waziri wa Afya leo ametoa msisitizo kuwa ni marufuku maduka binafsi ya dawa kuwa karibu na viunga vya hospitali za umma hivyo yanapaswa kuwa umbali usiopungua mita 500 kutoka hospitali ilipo. Sababu kuu ni kuwa, huenda maduka hayo ya dawa yanahusika katika kuchochea upungufu wa dawa na vifaa tiba kwenye hospitali za umma hivyo kujenga taswira mbaya kwenye jamii.
Tukija upande wa pili, karibu hospitali zote kuu au kubwa za afya za umma hapa Tanzania zimezungukwa na utitiri wa biashara za kuuza majeneza, sanda na viambatanisho vyote vya mazishi. Hili halina mwongozo wala kauli mpaka sasa, hii ikiwa na maana limekubaliwa, kuhalalishwa na kuzoeleka.
Sasa tutafakari nini mantiki na faida katika yote mawili.
Tukija upande wa pili, karibu hospitali zote kuu au kubwa za afya za umma hapa Tanzania zimezungukwa na utitiri wa biashara za kuuza majeneza, sanda na viambatanisho vyote vya mazishi. Hili halina mwongozo wala kauli mpaka sasa, hii ikiwa na maana limekubaliwa, kuhalalishwa na kuzoeleka.
Sasa tutafakari nini mantiki na faida katika yote mawili.