TAFAKARI: Sikukuu ya wakulima 8/8 kufunikwa na mechi kati ya Simba na Yanga, je Watanzania wa leo hawahitaji tena kilimo?

TAFAKARI: Sikukuu ya wakulima 8/8 kufunikwa na mechi kati ya Simba na Yanga, je Watanzania wa leo hawahitaji tena kilimo?

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
9,758
Reaction score
18,431
Wasalaam JF

Nimejaribu kufuatilia vituo vingi vya habari na hata mazungumzo ya baadhi ya maeneo niliyopo na kushtushwa na kupotea kwa umaarufu ya sikukuu ya wakulima 8/8.

Katika fuatiloa yangu nimegundua kuwa mechi ya juzi ya watani wa jadi ni kama nayo imepigilia msumari wamoto kwenye kufichwa kwa sikukuu hii ya wakulima.

Vituo vingi hadi leo bado vinachambua na kuzungumzia mechi ya watani Simba na Yanga. Nimebahatika kusikia jambo moja tu likiongelewa tena ni kauli ya Mheshimjwa raisi wa JMT juu ya gharama za magari ya serikali.

Sijasikia jambo lolote juu ya mbolea za ruzuku, vijana wasomi kutoka vyuo vya kilimo na ufugaji, mipango ya wizara na serikali kwa ujumla wake juu ya miradi ya kilimo au hata mijadala ya kilimo tulipotoka, tulipo na tuendapo.

Mbaya zaidi ukiongelea kilimo na maswala yake unaonekana mtu mshamba usiojua lolote la maana.

Ipo midahalo ya michezo kibiashara mingi sana kwa sasa lakini hata hii wiki ya wakulima imeshindikana wizara kufanya mijadala na kuipa promo kweli?

Nadhani huu ulikuwa muda wa kuona yatokanayo na ule mradi wa wizara kwa vijana lakini nao wapi, umefichwa mbali kabisa na jamii yetu.

Natafakari, hivi kweli kilimo kimetushinda au tumeamua kuachana nacho na kufanya mambo mengine.

Ikizingatiwa karibu 70% ya watanzania wanajishughulisha na shughuli za kilimo.

Nadhani ni muda tuwaze upya tunapoelekea kama taifa, hatari ipo ya Tanzania kuwa taifa lenye watu wa hovyo.Afrika mashariki miaka 20 ijayo, pengine hata tukatawaliwa na wenzetu hawa wa hii jumuiya.
 
Mpira.
Dini.
Siasa.

Huwezi kuwakosa mburula wa kibongo.
 
Sasa 8/8 ndio ukulima?

Usichokijua hayo masikukuu ni siasa tu hayana impact yoyote kwenye uhalisia

Usikaririshwe ujinga.
 
Ukienda duka la pembejeo Kwa Sasa tena kiangazi unaambiwa mbegu mfuko wa kg 2 17000
Lakini sisi tuko bize na Upuuzi
 
Nashauri simba na yanga ziwe zinacheza siku ya may mosi.....kupunguza stress kwa watumishi.
 
Watanzania si mmeamua kushabikia mpira pamoja na Rais wenu? WAKULIMA pambaneni na hali yenu
 
Kitu kimoja tu nikwambie kilimo ni muhimu sio lazima kizungumziwe. Wale wote waliokwenda uwanjani walikuwa wamekula na walipotoka walikula wakalala.
 
Back
Top Bottom