Tafsiri sahihi ya ubeberu

Tafsiri sahihi ya ubeberu

Amani Msumari

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2016
Posts
1,830
Reaction score
972
Wanajamvi,

Kumekuwa na Upotoshaji mkubwa Kuhusu ubeberu na mabeberu wenyewe. Hili huenda linafanywa makusudi au kwa kutokujua.

Nilipokuwa shule ya msingi nilifundishwa kuwa ubeberu (imperialism) ni ubepari uliokomaa na kuvuka mipaka. Watu waliosoma kipindi changu wanakumbuka hili. Tafsiri hii ni tafsiri rahisi na nzuri.

Wanahistoria wanajua kuwa ukoloni haujaisha ila umebadili fomu kutoka kuwa ukoloni wa kiutawala, kijeshi na kiuchumi mpaka kuwa ukoloni mamboleo (neocolonialism). Njia kubwa ya kueneza ukoloni mamboleo ni kwa kupitia ubeberu.

Ubeberu upo zaidi kiuchumi, yaani baadhi ya matajiri (Filth billionaires) hasa kutoka nchi za magharibi na makampuni makubwa (multinational companies) ambao Wana nguvu ya kuweka viongozi madarakani hutawala uchumi wa dunia kupitia ubeberu hivyo hao ndio wanakuwa "mabeberu".

Ubeberu unatekelezwa zaidi Afrika kutokana na sababu nyingi ikiwemo ukweli kuwa Afrika ndio bara pekee lililobaki na rasilimali nyingi. rejee sababu za ukoloni: kutafuta masoko kwa bidhaa za viwanda vyao, malighafi kwa viwanda vyao, ardhi n.k, Mahitaji hayo yangali hai mpaka sasa. Lakini ubeberu pia unatekelezwa zaidi Afrika kutokana na ukweli pia baadhi ya viongozi wetu ni dhaifu dhhofu li hali huku wakiutukuza umagharibi na kuutweza uafrika wao.

Ili iwe rahisi kwa ubeberu kufanya kazi, kunapandikizwa viongozi vibaraka ambao hao wanakuwa ni "yes sir" mbele ya mabeberu. Akipatikana kiongozi imara ambaye hataki ujinga, huyu atapigwa vita na kusukiwa mipango ya kung'olewa kwani ni hatari kwa uchumi wa mabeberu. Kiongozi huyu ataitwa kila majina. Chukulia mfano ufuatao:

Uko bandari na unapiga dili zako na kila siku unakomba mshiko wa nguvu. Mara paap! anakuja meneja anakata na kuziba mirija you're ya rushwa na ize mane, utampenda? Lazima mtakaa kama kamati ya roho mbaya ili kuona jinsi ya kumshughulikia.

Sisi Kama nxhi tumeamua kulinda rasilimali zetu, hi maana yake ni kuwa tumetangaza vita ya kiuchumi. Kuishinda hii asiwadanganye mtu, Magufuli haiwezi peke yake. Ni lazima tuungane, tuwe wazalendo na kuweka maslahi ya Tanzania mbele.

Mabeberu wananguvu sana lakini wanatafuta chanzo kutoka ndani ya nchi. Tukiwa wamoja, hawawezi penya.

Nahitimisha kwa kusema sio kila utawala, nchi au kampuni za magharibi ni za kibeberu bali zile tuu zinazotenda ubeberu.

#ubeberuupotuwemacho

Amani Msumari
Tanga
 
Naona tafsiri hii inakuja wakati ambapo Bashiru anaenda kuongea na mabeberu!Lumumba mnachekesha sana!Wakati Lissu anaenda kuongea na mabalozi mlipayuka sana kuwa Mabeberu wanakutana na Lissu!Leo ni zamu ya Bashiru,mnakuja na tafsiri kibao.

Aisee! Sio kwa kujitoa ufahamu kwa kiwango hiki aisee!
 
Wakikupa dawa za ukimwi na kukujengea barabara wahisani, wakikueleza kwamba unaminya demokrasia mabeberu, hapo sawa.
Ni wazi kuwa umekurupuka au hujaelewa bandiko langu kwani usingejibu ulivyojibu. Soma kwa kutulia
 
Watanzania tunawakataa vibaraka wa mabeberu.
Mungu walaani vibaraka wote wa mabeberu na mambo yao.
 
Naona tafsiri hii inakuja wakati ambapo Bashiru anaenda kuongea na mabeberu!Lumumba mnachekesha sana!Wakati Lissu anaenda kuongea na mabalozi mlipayuka sana kuwa Mabeberu wanakutana na Lissu!Leo ni zamu ya Bashiru,mnakuja na tafsiri kibao!
Aisee!Sio kwa kujitoa ufahamu kwa kiwango hiki aisee!
Tatizo mmeamua kuamini mnachoamini ila hicho nilichoandika ndio tafsiri sahihi ya ubeberu na mabeberu
 
Wakisema uchaguzi huru na haki hapo wanakuwa mabeberu!Wakisema haki za binadamu wanakuwa mabeberu!Subiri watoe msaada wa matundu ya vyoo,hapo utasikia ni wadau wa maendeleo!
Hivi nyie vichwa mapambo kuichosha miguu, muambiwe kwa kikara ndio mtaelewa?

Inamaana hamjui au ni kusudi tuu? Hamkumbuku Rais Magufuli alikutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania na akaahidi uchaguzi huru na haki?
 
Hivi nyie vichwa mapambo kuichosha miguu, muambiwe kwa kikara ndio mtaelewa?

Inamaana hamjui au ni kusudi tuu? Hamkumbuku Rais Magufuli alikutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania na akaahidi uchaguzi huru na haki?
Kwa hiyo aliahidi mbele ya mabeberu au?
 
Watanzania tunawakataa vibaraka wa mabeberu.
Mungu walaani vibaraka wote wa mabeberu na mambo yao.
Mpo madarakani miaka kama 60 hivi,hizo raslimali mlianza kuzilinda lini?Je,hawa mnaowaita vibaraka wa mabeberu hawapo CCM/Serikalini?Mnatuaminisha kuwa wapinzani ndiyo vibaraka/mawakala wa mabeberu huku wanaouza raslimali kwa mikataba ya Kimangungo wapo CCM na serikali zake hadi sasa.Tuwaeleweje?Mnaweza kutuonyesha ushahidi kuwa wapinzani ni vibaraka?Watanzania hawawezi kuelewa Haki zao hadi mabeberu wawatetee?Wasema kweli wamepachikwa majina ya vibaraka na wakala halisi akiitwa mzalendo!
 
Hivi nyie vichwa mapambo kuichosha miguu, muambiwe kwa kikara ndio mtaelewa?

Inamaana hamjui au ni kusudi tuu? Hamkumbuku Rais Magufuli alikutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania na akaahidi uchaguzi huru na haki?
Sema alikutana na mabeberu akawaahidi uchaguzi huru na wa haki lakini katika vitendo amekengeuka ndio maana wanataka wamshughulikie!

Kwanza nijibu kwanini huyo magufuli anaruhusu balozi za mabeberu ziwepo nchini ilihali akijua sio watu wazuri? Kwanini anakutana na mabeberu ilihali hawaitakii nchi mema?

Ana mpango gani na mabeberu mpaka akae nao na kuwaahidi kutekeleza matakwa yao?

Nyie CCM awamu hii ni ya mwisho kwenu sababu hamueleweki wala hata sera hamna tofauti na mwenyekiti wenu kubwabwaja kwenye majukwaa na kutamanitamani wanawake weupe huku akiwa na mke mweusi nyumbani
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hivi nyie vichwa mapambo kuichosha miguu, muambiwe kwa kikara ndio mtaelewa?

Inamaana hamjui au ni kusudi tuu? Hamkumbuku Rais Magufuli alikutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania na akaahidi uchaguzi huru na haki?
Tatizo lipo kwenye utekelezaji hiyo ahadi,matendo yaonyesha mipango ya kuiba kura imekamilika kwa kupitia engua engua,Ma DED,WEO,VEO na Tume kiujumla.Matendo wanavyowatendea wapinzani vinadhihirisha kuwa uchaguzi huru ni kwa CCM ila wapinzani wananyimwa hata kusafiria vivuko vya umma,ambapo pia wameikosesha serikali mapato yake halali ya nauli/kodi ya abiria na magari yao halafu aliyeagiza hayo bado yupo ofisini ilhali ni mhujumu uchumi!CCM mshipa wa aibu ulipata electric shortage?
 
Back
Top Bottom